Air Tanzania na mabadiliko ya muda wa safari bila taarifa kwa wateja

masatujr1985

JF-Expert Member
Oct 27, 2011
1,980
780
Kwanza nitoe pongezi kwa serikali kufufua shirika hili la Ndege la Taifa.

Baada ya pongezi, nieleze masikitiko juu ya utaratibu mbovu wa uahirishaji wa muda wa safari za abiria bila kutoa taarifa.

Abiria wanaosafiri kutoka Mwanza, baadhi wanatoka mikoa ya jirani kama Mara, Simiyu, na Shinyanga. Wengi hulazimika kutafuta malazi hapo Mwanza ili kuwahi safari hasa za asubuhi. Ajabu ni kuwa Shirika bila kujali usumbufu na gharama wanazoingia abiria wake, linaahirisha muda wa safari mfano kwa leo toka saa 3 asubuhi kwenda saa 7 mchana. Mtu aliyejihimu saa 12 anafika airport na kukuta mabadiliko haya, anapata usumbufu mkubwa sana. Wengine wana wagonjwa, watoto wadogo na hata wengine wanawahi katika shughuli zao mbalimbali.

Nadhani ni busara, kwa ustawi wa Shirika, basi inapotokea kuna mabadiliko ya safari, wateja wataarifiwe. Hii ishanitokea sasa mara ya pili na mara zote nimeingia gharama zisizo za lazima sababu ya kukosekana kwa taarifa.

Air Tanzania tafadhalini sana, hii kero tunayokutana nayo abiria wenu inatupatia shida sana. Tuondoleeni kero hii na boresheni kitengo cha mawasiliano maana kila mteja mna mawasiliano yake.

Lingine ambalo ni la maboresho nadhani Lugha inayoanza kutumika kwenye system nashauri tuanze na Kiswahili kisha ndiyo Kiingereza na Kichina vifuatie.

Mungu Ibariki Tanzania
 
Hizi kero naoma zimezidi sasa Mzee Mwanakijiji alishakuja na mada hii hii juzi kati.
 
Tumeshaiomba serikali imuondoe mkuu wa shirika hilo na kumpangia kazi nyingine maana ameshindwa kuliendesha kwa ufanisi... (Miaka mitatu aliyokaa inamtosha. Kama hajachuma vya kutosha, atajiju).
Wako bize kuanzisha safari za nje wakati za ndani zinawashinda. They do a paint job kumhadaa muheshimiwa kuwa wako vizuri wakati wanaboronga tu kila kukicha.
Just wait... Vuta Subra.
 
We unafikiria waliwaza nini kuiletea fastjet figisu ..!

Huwezi survive ikiwa huna ushindani na wasipokua makini watu wataamua watumie mabasi tu.

Saa7 mchana mtu anaitafuta Singida kwa basi we upo mwanza na ulipaswa uondoke sa3 asbh.
 
Sure mkuu. Na hapo nimelala Mwanza ili niwahi safari ya asubuhi. Si bora wangetuma ujumbe mapema jana nikalala nilikotoka na kuja asubuhi Mwanza! Quite unfair...halafu na watoto wadogo wanalala na kushangaa shangaa tu Airport hapa.
We unafikiria waliwaza nini kuiletea fastjet figisu ..!

Huwezi survive ikiwa huna ushindani na wasipokua makini watu wataamua watumie mabasi tu.

Saa7 mchana mtu anaitafuta Singida kwa basi we upo mwanza na ulipaswa uondoke sa3 asbh.
 
Pole sana mkuu, ila nimeona mahali kuwa fastjet wamemalizana na madeni yao kwenye mamlaka ikitokea wakifanikiwa kurudi basi hao ATCL watakubali show!
Sure mkuu. Na hapo nimelala Mwanza ili niwahi safari ya asubuhi. Si bora wangetuma ujumbe mapema jana nikalala nilikotoka na kuja asubuhi Mwanza! Quite unfair...halafu na watoto wadogo wanalala na kushangaa shangaa tu Airport hapa.
 
Kwanza nitoe pongezi kwa serikali kufufua shirika hili la Ndege la Taifa.

Baada ya pongezi, nieleze masikitiko juu ya utaratibu mbovu wa uahirishaji wa muda wa safari za abiria bila kutoa taarifa.

Abiria wanaosafiri kutoka Mwanza, baadhi wanatoka mikoa ya jirani kama Mara, Simiyu, na Shinyanga. Wengi hulazimika kutafuta malazi hapo Mwanza ili kuwahi safari hasa za asubuhi. Ajabu ni kuwa Shirika bila kujali usumbufu na gharama wanazoingia abiria wake, linaahirisha muda wa safari mfano kwa leo toka saa 3 asubuhi kwenda saa 7 mchana. Mtu aliyejihimu saa 12 anafika airport na kukuta mabadiliko haya, anapata usumbufu mkubwa sana. Wengine wana wagonjwa, watoto wadogo na hata wengine wanawahi katika shughuli zao mbalimbali.

Nadhani ni busara, kwa ustawi wa Shirika, basi inapotokea kuna mabadiliko ya safari, wateja wataarifiwe. Hii ishanitokea sasa mara ya pili na mara zote nimeingia gharama zisizo za lazima sababu ya kukosekana kwa taarifa.

Air Tanzania tafadhalini sana, hii kero tunayokutana nayo abiria wenu inatupatia shida sana. Tuondoleeni kero hii na boresheni kitengo cha mawasiliano maana kila mteja mna mawasiliano yake.

Lingine ambalo ni la maboresho nadhani Lugha inayoanza kutumika kwenye system nashauri tuanze na Kiswahili kisha ndiyo Kiingereza na Kichina vifuatie.

Mungu Ibariki Tanzania
👂
 
Pole sana mkuu, ila nimeona mahali kuwa fastjet wamemalizana na madeni yao kwenye mamlaka ikitokea wakifanikiwa kurudi basi hao ATCL watakubali show!
Wamemalizana bado kuna figisu za vibari na isitoshe Masha hana senti hata tano ameshindwa hata kulipa mishahara
 
Kama ATCL wamekuwa hovyo kiasi hiki kwenye safari za hapa nchini kwenye hizo za kimataifa wakifanya kama hapa si ndio watakosa hata msafiri mmoja??
 
Kwanza nitoe pongezi kwa serikali kufufua shirika hili la Ndege la Taifa.

Baada ya pongezi, nieleze masikitiko juu ya utaratibu mbovu wa uahirishaji wa muda wa safari za abiria bila kutoa taarifa.

Abiria wanaosafiri kutoka Mwanza, baadhi wanatoka mikoa ya jirani kama Mara, Simiyu, na Shinyanga. Wengi hulazimika kutafuta malazi hapo Mwanza ili kuwahi safari hasa za asubuhi. Ajabu ni kuwa Shirika bila kujali usumbufu na gharama wanazoingia abiria wake, linaahirisha muda wa safari mfano kwa leo toka saa 3 asubuhi kwenda saa 7 mchana. Mtu aliyejihimu saa 12 anafika airport na kukuta mabadiliko haya, anapata usumbufu mkubwa sana. Wengine wana wagonjwa, watoto wadogo na hata wengine wanawahi katika shughuli zao mbalimbali.

Nadhani ni busara, kwa ustawi wa Shirika, basi inapotokea kuna mabadiliko ya safari, wateja wataarifiwe. Hii ishanitokea sasa mara ya pili na mara zote nimeingia gharama zisizo za lazima sababu ya kukosekana kwa taarifa.

Air Tanzania tafadhalini sana, hii kero tunayokutana nayo abiria wenu inatupatia shida sana. Tuondoleeni kero hii na boresheni kitengo cha mawasiliano maana kila mteja mna mawasiliano yake.

Lingine ambalo ni la maboresho nadhani Lugha inayoanza kutumika kwenye system nashauri tuanze na Kiswahili kisha ndiyo Kiingereza na Kichina vifuatie.

Mungu Ibariki Tanzania
Yaani, kwa ALIYEKO JF na huku hajawahi kusafiri au jamaa yake hajawahi kusafiri kwa ndege za ATC anaweza abishe.... Lakini ndo ukweli... Kama ya Mwanza nayo mambo no hayo, YA MTWARA NAYO NI BALAA.... WANABADILI SAFARI HUKU UPO WAITING LOUNGE NA UNA BOARDING PASS...

Inaonyesha ni tatizo la kutaifa
 
Sure mkuu. Na hapo nimelala Mwanza ili niwahi safari ya asubuhi. Si bora wangetuma ujumbe mapema jana nikalala nilikotoka na kuja asubuhi Mwanza! Quite unfair...halafu na watoto wadogo wanalala na kushangaa shangaa tu Airport hapa.
Kuna siku pale Dar, watu tunasubiria ku-board, kimyaaa .... Muda wa ku-board ilipopita nikaanza kuhusi nimeachwa. Kumbe tulikuwa wengi na kila mmoja alikuwa anahisi hivyo. Kwenda kuuliza kumbe ndege imefutwa mpaka kesho yake. Na kesho yake ilipofika tukafaulidhiwa PRECISIONAIR....

YAANI TAARIFA ZA NDEGE KUFUTWA NI MPAKA TULIPOILIZIA VINGINEVYO SIJUI TUNGEKAA MPAKA SAA NGAPI
 
Infromation to passengers prior to postponement,hili wanapaswa kulitilia mkazo sana,sijawahi kusafiri na ATCL,ila iliwahi kunikuta Mwanza na ni Precision Air,unaweza kulichukulia ni poa,lakini usumbufu unakuwa ni mkubwa sana,nimeshafungasha vilago vyangu,Mwanza mimi sio mwenyeji,unafika aiport saa 12 unaambiwa safari imeahirishwa mpaka saa 7,sasa huna pa kwenda unabaki kuranda randa tu airport...
 
Airbus moja leo imeruka kwenda Chato kumpereka mkulu na wasaidizi wake mapunzikoni!... haya ni matumizi ya hovyo ya mali za wadanganyika.
 
Sio air Tanzania peke yake, hata Precision air wanayo tabia hii mbaya hata kuzidi airtz. Muda huu 22:22 tunadubiria kuondoka bila mafanikio na muda wa kuondoka ulikuwa 21.30
Kwanza nitoe pongezi kwa serikali kufufua shirika hili la Ndege la Taifa.

Baada ya pongezi, nieleze masikitiko juu ya utaratibu mbovu wa uahirishaji wa muda wa safari za abiria bila kutoa taarifa.

Abiria wanaosafiri kutoka Mwanza, baadhi wanatoka mikoa ya jirani kama Mara, Simiyu, na Shinyanga. Wengi hulazimika kutafuta malazi hapo Mwanza ili kuwahi safari hasa za asubuhi. Ajabu ni kuwa Shirika bila kujali usumbufu na gharama wanazoingia abiria wake, linaahirisha muda wa safari mfano kwa leo toka saa 3 asubuhi kwenda saa 7 mchana. Mtu aliyejihimu saa 12 anafika airport na kukuta mabadiliko haya, anapata usumbufu mkubwa sana. Wengine wana wagonjwa, watoto wadogo na hata wengine wanawahi katika shughuli zao mbalimbali.

Nadhani ni busara, kwa ustawi wa Shirika, basi inapotokea kuna mabadiliko ya safari, wateja wataarifiwe. Hii ishanitokea sasa mara ya pili na mara zote nimeingia gharama zisizo za lazima sababu ya kukosekana kwa taarifa.

Air Tanzania tafadhalini sana, hii kero tunayokutana nayo abiria wenu inatupatia shida sana. Tuondoleeni kero hii na boresheni kitengo cha mawasiliano maana kila mteja mna mawasiliano yake.

Lingine ambalo ni la maboresho nadhani Lugha inayoanza kutumika kwenye system nashauri tuanze na Kiswahili kisha ndiyo Kiingereza na Kichina vifuatie.

Mungu Ibariki Tanzania
 
Back
Top Bottom