[h=2]Aina tatu za wanawake ambazo manamume hukolea nazo[/h]
Mimi sio mtaalamu kwa sana ila leo nitawaletea nini ninakijua nanyi mupate kuchangia
Mwanamke mcheshi
Mwanamke ambaye hupenda kutabasamu(mcheshi) humfanya mwanamme asisite kutaka kuongea naye au hata kutaka mahusiano zaidi. We fikiria wale akina dada ambao muda wote wao wameuchuna, kabla ya
kwenda unafikiria uanzie wapi. Siku moja baada ya kazi tukawa katika majadiliano kuhusu masuala ya mahusiano. Binafsi nikataka kujua sababu ambayo inawafanya akina dada wengi weusi kuwa serious muda mwingi kitu kinachopelekea wanamme wengi weusi kuamua kutoka na akina dada weupe au wa kiasia kutokana na hurka yao ya kuwa wacheshi kwa wanamme. Yeye alijibu kwa kusema ukijichekesha kwa mwanamme mweusi inamaanisha unampa nafasi hivyo basi ni heri kuwa ngangari. Nimekuwa nikisoma sehemu nyingi mno wakisema wanawake weusi wana hurka ya kutokuwa na ucheshi kwa wanamme labda awe amevutiwa sana.Sijui munaonaje hili?
Mwanawake msikivu.
Amini usiamini, wanamume wengi hupenda wanawake wasikivu, sina maana mwanamke anatakiwa kumsikiliza na kumkubalia mwanamme kwa kila anachosema,la hasha. Nina maanisha pindi unapokuwa pamoja na mwanamme (mume,rafiki au hata mchumba) jaribu kumpa nafasi ya kuongea. Kuna siku nilikuwa naangalia kipindi kimoja cha kutafuta wachumba, Katika kipindi hicho mwanamme hupata nafasi ya kukutana na warembo watano, baada ya maongezi machache huchagua watatu ambao wataenda date kwa mida tofauti. Basi kidume kilikutana na mrembo mmoja ambaye muda wote alikuwa anamgonga maswali jamaa na kumfanya asipate hata muda wa kuongea alichotaka. Yule jamaa alitosa palepale.Wanaume wengi huchukia warembo wanaochonga sana.
Chukulia siku unakutana na mrembo anayesikiliza kwa kutumia macho yake,kuitikia kwa kichwa na ishara tofauti. Ni dhahiri mwanamume atakolea ipasavyo na kutaka muda wote kuongea na wewe.
[FONT=Arial, Helvetica, sans-serif]
Mwanamke anayevutia kimavazi[/FONT]
Amini usiamini,wanamume wengi hupenda wanawake wanaopendeza na kuvutia kimavazi. Kuna baadhi ya wanawake husema mwanamme hawezi kuvutiwa na mwanamke ambaye sio chaguo lake. Hii si kweli kwani wanamume wengi huanza kuvutiwa machoni halafu mambo mengine huendelea. Chukua mfano wamekaa vidume vitatu halafu akapita binti aliyevalia vyema(simaanishi lazima awe kavaa kimtego), ni lazima wawili kama sio wote watageuza macho(si unakumbuka ile picha ya Obama na Santosi?), kutathmini halafu kuendelea na hatua inayofuata ni hulka ya wanamume.
hayo ndio niliyotaka kuwaambia dada zetu kwa leo.
[FONT=Arial, Helvetica, sans-serif]Source: Ughaibuni.com[/FONT]
Mimi sio mtaalamu kwa sana ila leo nitawaletea nini ninakijua nanyi mupate kuchangia
Mwanamke ambaye hupenda kutabasamu(mcheshi) humfanya mwanamme asisite kutaka kuongea naye au hata kutaka mahusiano zaidi. We fikiria wale akina dada ambao muda wote wao wameuchuna, kabla ya
kwenda unafikiria uanzie wapi. Siku moja baada ya kazi tukawa katika majadiliano kuhusu masuala ya mahusiano. Binafsi nikataka kujua sababu ambayo inawafanya akina dada wengi weusi kuwa serious muda mwingi kitu kinachopelekea wanamme wengi weusi kuamua kutoka na akina dada weupe au wa kiasia kutokana na hurka yao ya kuwa wacheshi kwa wanamme. Yeye alijibu kwa kusema ukijichekesha kwa mwanamme mweusi inamaanisha unampa nafasi hivyo basi ni heri kuwa ngangari. Nimekuwa nikisoma sehemu nyingi mno wakisema wanawake weusi wana hurka ya kutokuwa na ucheshi kwa wanamme labda awe amevutiwa sana.Sijui munaonaje hili?
Amini usiamini, wanamume wengi hupenda wanawake wasikivu, sina maana mwanamke anatakiwa kumsikiliza na kumkubalia mwanamme kwa kila anachosema,la hasha. Nina maanisha pindi unapokuwa pamoja na mwanamme (mume,rafiki au hata mchumba) jaribu kumpa nafasi ya kuongea. Kuna siku nilikuwa naangalia kipindi kimoja cha kutafuta wachumba, Katika kipindi hicho mwanamme hupata nafasi ya kukutana na warembo watano, baada ya maongezi machache huchagua watatu ambao wataenda date kwa mida tofauti. Basi kidume kilikutana na mrembo mmoja ambaye muda wote alikuwa anamgonga maswali jamaa na kumfanya asipate hata muda wa kuongea alichotaka. Yule jamaa alitosa palepale.Wanaume wengi huchukia warembo wanaochonga sana.
Chukulia siku unakutana na mrembo anayesikiliza kwa kutumia macho yake,kuitikia kwa kichwa na ishara tofauti. Ni dhahiri mwanamume atakolea ipasavyo na kutaka muda wote kuongea na wewe.
[FONT=Arial, Helvetica, sans-serif]
Amini usiamini,wanamume wengi hupenda wanawake wanaopendeza na kuvutia kimavazi. Kuna baadhi ya wanawake husema mwanamme hawezi kuvutiwa na mwanamke ambaye sio chaguo lake. Hii si kweli kwani wanamume wengi huanza kuvutiwa machoni halafu mambo mengine huendelea. Chukua mfano wamekaa vidume vitatu halafu akapita binti aliyevalia vyema(simaanishi lazima awe kavaa kimtego), ni lazima wawili kama sio wote watageuza macho(si unakumbuka ile picha ya Obama na Santosi?), kutathmini halafu kuendelea na hatua inayofuata ni hulka ya wanamume.
hayo ndio niliyotaka kuwaambia dada zetu kwa leo.
[FONT=Arial, Helvetica, sans-serif]Source: Ughaibuni.com[/FONT]