Aina mpya ya wizi Vodacom

Aina mpya ya wizi Vodacom

Voda mi nshaachana nao kitambo coz wanajiongeza sana hadi wanabore
 
Saa nyingine system yao inakuwa hovyo kwa hyo mpaka ije kurespond inakamilisha miamala yote uliyofanya.

Nakushauri,ukifanya muamla mmoja tulia kwanza na wala usifanye muamala mwingine mpaka utakaporudishiwa majibu.
Mbona kununua salio m-pesa system hairuhusu kufanya muhamala zaid ya mmoja?.kama kuna tatatizo la system utaambiwa ombi lako la kwanza bado linashughulikiwa.hata ufanye muhamala mara 20 ikija kukubali utapata moja tu.lkn hii ya kununua kifurushi itakataa na badae itanunua vifurushi vyote kulingana na idadi ya mihamala uliyofanya.somethng is wrong
 
Vodacom wezi, yaani wanakata airtime wakati una bundle na haijaisha, nimeweka 2 500 ili nijiunge ilisalia saa moja kabla bundle nyingine haijaisha nimekuta 667 nili mind sana... Nilikuwa nimeachana miezi nimerudi juzi baada ya kupoteza line nawaacha tena
 
Wanachofanya kukuibia ni hivii:-
Ukinunua "bando" i.e la internet kwa M-Pesa hawakupi majibu ya ukamilifu wa muamala, ukiangalia salio unakuta lipo vile vile.

Muda ukipita utajaribu mara ingine kununua, pia hutapewa report ya kufanikiwa, kwa kuwa salio halitakatwa, utaridhika kuwa muamala haujakamilika.

Utajaribu mara ya tatu au hata nne, ukiisha kata tamaa na kuacha baada ya nusu saa au zaidi kidogo wanakuuzia miamala ya bando zooote ulizojaribu kununua na mbaya zaidi uwe ulinunua bando za siku, unaweza kujikuta umeibiwa hadi 10,000/ kwa staili hii walioibuni hawa vodacom.

Natafuta njia bora kabisa ya kuachana nao maana tazama wanatumia mabilioni ya shilingi kutafuta wateja kwa matangazo ya biashara yao, lakini wanashindwa kutumia mtaji mdogo kabisa kuendelea kunipa huduma niwe sehemu ya kuwaingizia faida iliyokusudiwa na matangazo ya kuwalipa kina daimond kusaka wateja.

Piga costomer care yao uone majibu yao ya kukariri, AIBU.
Kumbe naepuka mengi kutotumia Sim card yangu ya voda. Mkuu pole sana. Karibu airtel.
 
Mie juzi nmetuma elfu kumi kimakosa kwenda namba nyingine, nikapiga customer care, majibu walonipa ni kuwa wao hawana msaada wowote kwa kuwa niliyemtumia amekwishazitoa.

Nikawauliza mbona mie niliwahi tumiwa pesa kimakosa nikazitoa ,mkafungia account yangu?

Wakaniambia ilikuwa zamani, au niende polisi.

Nilchokipanga kwa sasa ni kuwa pesa yoyote itakayoingia kimakosa ,mtumaji ahesabu maumivu
 
Pole! hii njia ya kununua vifurushi kwa mpesa niliukataa mara ileile walipouleta! ni sawa na ule wa kununua muda wa hewani kwa simbanking, utalia!
 
Watu wanawekeza mihela miiingi kwenye matangazo badala ya kuboresha huduma..sehem nyingi dar nikiwa temeke...ilala....ubungo...kinondoni....internret yao inasoma edge 'E' kibaya zaidi hata hiyo edge haina nguvu kbsaaaa...unakaa nusu saa kusubiri msg ya whatsap..cha ajab hawasikii hili kampuni
 
Nikweli kuna wizi mkubwa. Unanunua bando la MB 500 lakini data meter ya tablet yako ikisoma unetumia MB 420 tuu wao wanakuonyesha kuwa unemaliza MB 500.
Sasa wizi huu mpaka lini? Na kama ni kwa nchi nzima wanatuibia kiasi gani kwa siku,mwezi hadi mwaka?
TCRA waliangalie hili, huu ni ukibaka kana mwingine wowote
TCRA imevunjwa haipo
 
Wameniliza jumapili mimi kila nikiweka mb dkk tatu wameshapita nazo nikapiga simu huduma kwa wateja wakanijibu uliacha data wazi nikawajibu mbona miaka yote hamkati!? Utanikata vipi mb 1500 kwa mara moja pasipo kutumia data !? Nikaweka elfu moja nayo wakapita nayo!! Nikaamua kurudi airtel.
Ndugu Kambagasa, tunaweza kuwasiliana kupitia DM ili kukufahamisha zaidi matumizi yako. Uishaji wa kifurushi unatokana na matumizi.
 
Voda ni kweli wamejisahau sana huko tuendako watabaki na matajiri tuu
 
caf8ca6b58b0e8cdf37f0390531ed473.jpg

Mkuu hili hutokea endapo pesa uliyotumiwa au kuweka kwa wakala bado ipo katika "authorized status". Pia hutokea endapo ulitumiwa pesa kimakosa, tafadhali tupatie namba yako kupitia DM.
 
Vodacom sasa hivi ni wezi sana. Sasa hivi Halotel ndio maisha yangu katika huduma ya data. Punde nita achana nao hata kwenye Voice call. Maana nako ni wizi mtupu.
 
Hawa wamechoka, Jana nimenunua bando Ka 1500 mpaka Leo sijalipata nimeongea na customer care , majibu yako tunashughulikia sh*nzi zao kabisa.
 
Nyie Vodacom tuleteeni najaribuni kuboresha Huduma zenu huku vijijini kasi ya internet hakuna kabisa mnatubore kweli tutawahama.
 
Habari Bongolala, unapata tatizo gani kwenye Dabo Bando?
Hakuna ujumbe wowote wa kusema bando la halali limeisha sasa unaanza kutumia la dabo au zawadi.Wizi mtupu na ukichunguza hakuna cha dabo yaani hata zile za halali wanaiba muda
 
Nimetuma pesa kwa mtu wa tigo, pesa ikakatwa lakini nimepokea ujumbe mhamala haukufanyika kila nikiwapigia nakuwaeleza customer care wa vodacom wananiambia pesa niliyotuma ipo hewani itarudi kwangu. Haya ni majipu, tcra wawe wakali huku
 
Back
Top Bottom