Ahsante Simba kwa kushiriki ligi ya Mabingwa

Madibira 1

JF-Expert Member
Jan 6, 2023
340
734
Mechi za ushindi Kwa timu ya Simba zimemalizika rasmi Leo Kwa ushindi mnono dhidi ya vipers. Mechi hivyo imeifanya Simba kuwa nafasi ya pili Kwa alama sita nyuma ya vinara Raja club athletic. Timu ya Simba inachuana vikali na Horoya katika nafasi ya pili hivyo yeyote kati Yao atafuzu.

Kwa namna Simba ilivyocheza dhidi ya vipers ni dhahiri kuwa mwendo wameumaliza yaani horoya watamuua nyumbani Kisha kule Kwa Raja ataenda kukamilisha ratiba. Licha ya kushindwa dhidi ya Raja, Horoya wanaubora na ari kuliko Simba.

Ahsante Simba Kwa kushiriki, karibu super league Kwa hapa mwendo umeumaliza.
 
Hata mlipoambiwa simba itapata points 6 kutoka Vipers mlibisha. Mechi dhidi ya horoya vs simba kule guinea ni mechi ambayo simba hakustahili kufungwa. Umeandika kutabiri ambavyo shabiki maandazi yoyote anaweza kutabiri.
Umewatazama horoya Leo!?
 
Mechi za ushindi Kwa timu ya Simba zimemalizika rasmi Leo Kwa ushindi mnono dhidi ya vipers. Mechi hivyo imeifanya Simba kuwa nafasi ya pili Kwa alama sita nyuma ya vinara Raja club athletic. Timu ya Simba inachuana vikali na Horoya katika nafasi ya pili hivyo yeyote kati Yao atafuzu.

Kwa namna Simba ilivyocheza dhidi ya vipers ni dhahiri kuwa mwendo wameumaliza yaani horoya watamuua nyumbani Kisha kule Kwa Raja ataenda kukamilisha ratiba. Licha ya kushindwa dhidi ya Raja, Horoya wanaubora na ari kuliko Simba.

Ahsante Simba Kwa kushiriki, karibu super league Kwa hapa mwendo umeumaliza.
Mpira una mambo mengi,mfano Horoya akidroo na Simba,Horoya 5 points huku Simba 7 points,Horoya anamalizia Kwa Kwa Vipers,akishinda atakuwa na point 8,Simba hawezi mfunga Raja

Hivyo Simba ashinde mechi yake dhidi ya Horoya,kinyume na hapo ni kilio na kusaga meno kama Horoya atamnywa Vipers
 
Mpira una mambo mengi,mfano Horoya akidroo na Simba,Horoya 5 points huku Simba 7 points,Horoya anamalizia Kwa Kwa Vipers,akishinda atakuwa na point 8,Simba hawezi mfunga Raja

Hivyo Simba ashinde mechi yake dhidi ya Horoya,kinyume na hapo ni kilio na kusaga meno kama Horoya atamnywa Vipers
Inawezekana Simba akatoa sare kwa Raja hata kama atakuwa katoka sare na Horoya kwa Mkapa na bado akafuzu kwa goal difference
Unaweza kushangaa Vipers anashinda kwa Horoya au anatoa sare
 
Mpira una mambo mengi,mfano Horoya akidroo na Simba,Horoya 5 points huku Simba 7 points,Horoya anamalizia Kwa Kwa Vipers,akishinda atakuwa na point 8,Simba hawezi mfunga Raja

Hivyo Simba ashinde mechi yake dhidi ya Horoya,kinyume na hapo ni kilio na kusaga meno kama Horoya atamnywa Vipers
hao horoya ni wakawaida tu wanatumia xana nguvu kuliko akili, leo kama raja wasingekosa penati wangekula 4-1, halafu kusema horoya atamfunga vipers ni ushamba wa mpira, huu ni mpira sio maandazi, hata raja anaweza kufungwa nyumbani na simba,
 
Hata mlipoambiwa simba itapata points 6 kutoka Vipers mlibisha. Mechi dhidi ya horoya vs simba kule guinea ni mechi ambayo simba hakustahili kufungwa. Umeandika kutabiri ambavyo shabiki maandazi yoyote anaweza kutabiri.
Vijana wa mangungu uwa mnapenda kujipa matumaini hewa kweli yani, mkiambiwa ukweli mnapanic kiboya, Kwa mpira huu unaona kabisa uko kwenye right way? Uyo horoya unayemsema kwa sasa hivi sio horoya yule uliyekutana nae akakuzaba bao moja bila, horoya uyu kaboresha kiwango chake tofauti na timu yako kila uchwao inazidi kuporomoka kiwango, kwa maana iyo horoya kwa mkapa kama atapata matokeo mabaya basi ni sare na sio kumfunga, na yeye anakwenda kuchukua point za vipers nyumbani kwao kama na wewe ulivyozichukua uku ukienda moroco kukamilisha ratiba
 
Inawezekana Simba akatoa sare kwa Raja hata kama atakuwa katoka sare na Horoya kwa Mkapa na bado akafuzu kwa goal difference
Unaweza kushangaa Vipers anashinda kwa Horoya au anatoa sare
wanaangalia head to head kwanza mkuu kabla ya goal difference, japo simba kwanamna yeyote anahitaji xana ushindi waaina yeyote ile kujihakikishia kufuzu dhidi ya horoya
 
hao horoya ni wakawaida tu wanatumia xana nguvu kuliko akili, leo kama raja wasingekosa penati wangekula 4-1, halafu kusema horoya atamfunga vipers ni ushamba wa mpira, huu ni mpira sio maandazi, hata raja anaweza kufungwa nyumbani na simba,
🤣🤣🤣🤣 hizi bangi za kuvutia chooni ni mbaya kwakweli, kwamba simba hii ikamfunge Raja nyumbani kwake🤔🤔🤔duuuh,,,aya bwana shabiki!
 
Back
Top Bottom