Age discrimination (ubaguzi wa umri)

Age discrimination (ubaguzi wa umri)

bnhai

JF-Expert Member
Joined
Jul 12, 2009
Posts
2,846
Reaction score
2,401
Katiba ya nchi inatoa haki sawa kwa Watanzania wote katika kuabudu, kufanya kazi, uhuru wa kuamua na kuchagua. Hivi karibuni kumekuwepo na tabia ya tume ya ajira au mashirika ya serikali kubagua watu wa makundi fulani kutokana na Umri. Hii haina tofauti na ubaguzi wa kijinsia au wa rangi na kinyume na katiba ya nchi. Cha kushangaza asasi za kijamii, kisheria na kiraia zimekuwa kimya katika hili.
Ni wakati wa kulipigia kelele hili ili kutokomeza ubaguzi wa kila aina katika nchi yetu.
Mungu Ibariki Tanzania!
 
start from there if you've seen that wenzetu USA ipo hivi unatambulika kama mtu mzima ambaye una uwezo wa ku vote pale ukiwa na miaka 21
lakini jeshini miaka 18
so kulinda nchi miaka 18 mkubwa na kupiga kura miaka 21 ndo mkubwa
 
we kama ni kikongwe unalilia nini?

Dogo nina qualify na uzoefu wa kutosha saana. Na wala sina haja na mchakamchaka wa kazi. Ila kikubwa kuna watu wanauzoefu, wamehama kutoka sekta binafsi au nje ya nchi na wanaweza kuchangia maendeleao ya taifa na familia zao. Wamelipa kodi na ni Watanzania ambao wanastahiki haki zote kutoka kwa serikali yao, kwanini wanyimwe fursa hizo? Hizi dhana za kuacha vitu vidogo hukawii kusikia waajiri wakisema ninataka watu wa mikoa fulani tu wafanye kazi kwangu. Tusiruhusu watu kubaguliwa. Kuna nchi watu wanaajiriwa wana miaka 60+ hii ni kuchukua uzoefu na kuachana na dhana ya kikongwe.
 
Wana maana yao mara nyingi hua wanaangalia angalau ukae miaka 15 kazini ukiwa unacontribute kwny mfuko ww na mwajiri wako
apo sasa itategemea kama ukifikisha miaka 60 ya kustaafu na haujafikisha miaka 15 ya ku make contributions ni ngumu kukuchukua kwa ajira ambazo ni permanent
Kwaio hua wanaangalia mbele zaidi ndio mana wanaweka limit ya umri.
Pia kuna baadhi ya senior position age inatakiwa iwe juu na huo sio ubaguzi .
 
[TABLE="width: 500"]
[TR]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[TR]
[TD][/TD]
[TD][/TD]
[/TR]
[/TABLE]
Wana maana yao mara nyingi hua wanaangalia angalau ukae miaka 15 kazini ukiwa unacontribute kwny mfuko ww na mwajiri wako
apo sasa itategemea kama ukifikisha miaka 60 ya kustaafu na haujafikisha miaka 15 ya ku make contributions ni ngumu kukuchukua kwa ajira ambazo ni permanent
Kwaio hua wanaangalia mbele zaidi ndio mana wanaweka limit ya umri.
Pia kuna baadhi ya senior position age inatakiwa iwe juu na huo sio ubaguzi .


Mkuu nakubaliana na mleta maada hasa kundi linalonyanyaswa ni vijana ambao wako under 40 pindi wanapoomba Senior position umri unakuwa umewekwa juu sana kama kigezo cha kuwaondoa wasiajiriwe japo kiuhalisia ni kwamba unapokuja kwenye Private Sector vijana wanashikilia senior position nyingi zaidi as compared na wazee au 40+ cadre. Lakini ukienda mbali zaidi kuna uwakilishi wa wananchi bungeni kupitia majimbo ya uchaguzi, utakuona umri ni kuanzia miaka 21 sasa najiuliza huku kwenye maofisi ya umma kuna kitu gani mpaka nafasi ya ukurugenzi tu mtu kuajiriwa wanataka awe angalau na umri wa miaka 45+ ambao hata ni zaidi ya umri wa mtu anaequalify kuwa rais wa nchi kwa mujibu wa katiba yetu? Mie nashauri mtu akifikisha miaka 30 au hata 28 kama anazo sifa ni bora aajiriwe hata kuwa chief executive officer. Mfano DSE ukiangalia inaongozwa na vijana watupu na naona inafanya vizuri sana kiutendaji.
 
Mfano mzuri fursa zilizotoka uhamhaji mwezi huu mwanzoni 2meshindwa kuombo coz umri tena 28yrs najikuta sina haki inakera sana.
 
Back
Top Bottom