Afungwa maisha lakini hajakata tamaa

Nancyjoa13

Senior Member
May 18, 2018
167
97
Ernest Bwire aliwasili Kenya kutoka kwao Uganda akiwa na matumaini makubwa ya kujiendeleza kikazi, lakini yote hayo ni ndoto sasa.
Kwa miaka 29 sasa Bwire amekuwa akitumikia kifungo jela.

Kwa sasa yupo gereza la Kamiti liliopo kilomita 16 kutoka katikati mwa jiji la Nairobi ambako anatumikia kifungo cha maisha kwa mauaji.

Kufikia sasa Bwire ndiye aliyetumikia kifungo cha miaka mingi zaidi nchini Kenya. Hata hivyo anasema hana hatia kwani hakuhusika na mauaji.

``Huyo kijana aliyenyongwa Nairobi nilikua rafiki mkubwa wa familia yao, na nisingeweza kufanya tendo hilo, lakini nimeikubali hali yangu ya sasa. Kwanza nilihukumiwa kunyongwa kisha baadae wakanihurumia nikafungwa maisha,'' Bwire anasema alipozungumza na John Nene wa Idhaa ya Kiswahili ya BBC huko Kamiti.

Alianza kifungo chake katika jela kuu ya Naivasha, kilomita 100 kutoka Niarobi.

``Nilipokua huko nilifanya kazi yangu ya ualimu nikifunza wafungwa wenzangu somo la Kiingereza,Kifaransa na Jiografia. Nilikua pia mwenyekiti wa shule ya wafungwa huko,'' anasema Bwire.

Baada ya mwaka mmoja katika jela ya Naivasha, Bwire alihamishwa hadi jela kuu ya Kamiti. Aliendelea na kazi yake ya ualimu katika shule ya msingi na ya upili ya Kamiti.

Hatimaye alipandishwa cheo akawa naibu wa msimamizi wa shule hiyo. Kutokana na bidii na kazi yake nzuri, Bwire sasa ni msimamizi mkuu wa shule hiyo.

``Nina furaha sana kushikilia cheo hiki cha mkuu wa shule. Ni kazi ninayoipenda sana,'' anasema Bwire akiwa mchangamfu na haonyeshi uchungu wowote wa kuwa gerezani. Kiafya yuko sawa, na ni mtu maridadi kwa usafi.

Kwa mavazi, Bwire hana sare za kawaida zenye mistari zinazovaliwa na wafungwa wote. Anavalia sare ya rangi ya samawati (buluu) ya wafungwa waliopandishwa cheo kusimamia wenzao kutokana na nidhamu yao na utiifu gerezani.

`Mimi na wenzangu wengine 15 ni Trustees (wafungwa wanaoaminika). Tunaishi vizuri. Tuko na sehemu yetu ya kulala.Tuna magodoro mazuri, choo kisafi na tunaoga na maji moto pia, sio baridi tu.''

Bwire anapongeza wakuu wa jela ya Kamiti na maaskari wanaowasimamia humo ndani kwa kuwatunza vizuri na kuzungumza nao kama binadamu.

``Siku hizi jela sio kama zamani. Kulikuwa na madai mengi ya wafungwa kuteswa. Tangu Makamu wa Rais wa zamani wa Kenya Moody Awori aanzishe usimamizi bora gerezani mambo yamebadilika. Hamna ukatili tena. Tunakula vizuri na kutazama runinga pia.''

Kuhusu miaka hiyo 29 aliyotumikia gerezani, Bwire anasema:`` Kama si imani yangu na uvumilivu ningekua siko lakini kwa vile nimeokoka na ninamuamini Mungu sana nimeweza kuishi vizuri lakini jela kama mjuavyo sio mahala pa furaha manaake huna uhuru wako ukiwa ndani.
Mbali na ualimu Bwire amesomea ushonaji, na ana vyeti vya masomo ya Bibilia, kompyuta na masuala ya maisha kwa jumla.

``La mhimu zaidi nililojifunza hapa ndani ni kuwa mvumilivu. Naomba nyote ambao mko nje muwe na uvimilivu kwa biashara zenu, ndoa na maisha kwa jumla. Nina imani kuna siku itafika nifunguliwe milango hapa niwe huru kama raia wengine.''
 
Back
Top Bottom