Afrika Kusini niijuavyo mimi

Afrika Kusini niijuavyo mimi

Untold story: Safari yangu kurudi South 1998
Hiki kipande ni kirefu na sijawahi kukisimulia .. Naona leo nitafanya hivyo.. Get ready
 
Naendelea sasa..!
Mwaka 1998 nilirudi Tz likizo kwa mara ya kwanza.. Ile kumaliza likizo nikaugua malaria na kulazwa siku moja kabla ya safari.. Hivyo shirika la ndege Alliance airline bythen wakakata almost 40% ya ticket na kunidushia pesa iliyobaki

Baada ya kupona nikawa sina nauli ya kutosha kupanda ndege hivyo nikaondoka na treni mpaka Kapiri Mposhi Zambia (hii safari ikawa na vituko vyake vingi sitavisimuia hapa)

Tuliondoka Dar Ijumaa jioni pale Tazara na kufika salama Zambia Mji wa Kapiri Mposhi Jumapili asubuhi
Pale nikachukua basi mpaka Lusaka na kufika mchana.. Nilipata hotel nikalala mpaka kesho yake siku ya Jumatatu

Nilienda stand na kufanikiwa kupata basi la South kupitia Zimmbwe.. Nikiwa ndani ya bus nikakutana na jamaa yangu mkenya naye katoka likizo.. Safari ikaanza
Tulisafiri mchana kutwa mpaka jioni tukafika mpakani mwa Zambia na Zimbabwe
 
Naendelea sasa..!
Mwaka 1998 nilirudi Tz likizo kwa mara ya kwanza.. Ile kumaliza likizo nikaugua malaria na kulazwa siku moja kabla ya safari.. Hivyo shirika la ndege Alliance airline bythen wakakata almost 40% ya ticket na kunidushia pesa iliyobaki

Baada ya kupona nikawa sina nauli ya kutosha kupanda ndege hivyo nikaondoka na treni mpaka Kapiri Mposhi Zambia (hii safari ikawa na vituko vyake vingi sitavisimuia hapa)

Tuliondoka Dar Ijumaa jioni pale Tazara na kufika salama Zambia Mji wa Kapiri Mposhi Jumapili asubuhi
Pale nikachukua basi mpaka Lusaka na kufika mchana.. Nilipata hotel nikalala mpaka kesho yake siku ya Jumatatu

Nilienda stand na kufanikiwa kupata basi la South kupitia Zimmbwe.. Nikiwa ndani ya bus nikakutana na jamaa yangu mkenya naye katoka likizo.. Safari ikaanza
Tulisafiri mchana kutwa mpaka jioni tukafika mpakani mwa Zambia na Zimbabwe
Enheee..! 👂
 
Naendelea..
Pale mpakani Chirundu ukaguzi wa mizigo na nyaraka za safari ukaanza kwa abiria wote
Sasa tukiwa kwenye bus kabla ya kufika boda yule jamaa yangu alinitambulisha kwa kijana mwingine mkenya akasema tuko naye safari moja

Sasa tukiwa kwenye foleni ya ukaguzi nyuma yangu alikuwa yule mkenya mwingine na jamaa yangu akawa kama mtu WS a tano nyuma

Kwenye ukaguzi nikakutwa na kanda 5 za kaseti za mziki... Kea kipindi hicho ukiwa na kitu ambacho unaingia nacho Zimbabwe on transit unakilipia ushuru kabisa na ukitoka nacho kuingia South unarudishiwa prsa yako

Enzi hizo zawadi kubwa ya kuwapelekea wabongo south ni kanda za mziki wa Kongo.. Bongo fleva haikuwepo.. Kama huna hela ya kulipia vitu unaviacha boda
Vilevile kulikuwa na sharti la kuwa na pesa ya Zimbabwe Zimdollar 50+.. Yule mkenya nyuma yangu akawa kapungukiwa 30 akaniomba nimuongezee tukifika South atanirudishia... Nilimpatia lakini lilikuwa bonge la kosa!

Sisi tukavuka lakini jamaa yangu akapata shida
Kwanza alitaka kuwahonga maafisa ili apitishe mzigo wake bila kulipa ushuru .. Alikuwa na kanda kama 20 hivi
Pili hakuwa na Zimdollar za kutosha kuonesha pale boda..

Walimruhusu kupita hivyohivyo lakini kumbe ulikuwa ni mtego kwani tulipofika boda ya kuingia South alikamatwa na police tukamuacha hapo

Sasa ndio nikaja kujua yule mkenya mwinginen hiyo ndio ilikuwa safari yake ya kwanza kwenda South na alikuwa boonge la mbutika.. Hata Nairobi kafika wakati anakuja South

Kutoka Zimbabwe sasa kwenda South nikakaa naye siti moja. Alikuwa anashangaa almost kila kitu.. Mbutika.. ! Mbutika kweli😂 mpaka kiswahili chake cha msukuma kinasubiri.😀🙌🏿

Tulisafiri siku nzima mpaka usiku wa saa moja ndio tunaingia Pretoria. Mimi ilikuwa nishukie hapo lakini nikashindwa kwakuwa huyu mbutika nilikuwa namdai na amesema tukifika ndugu yake anayekuja kumpokea atanirejeshea pesa yangu

Mwendo wa kama nususaa hivi tukaingia Johannesburg kitongoji cha Hillbrow ilipo stand ya mwisho!

Hillbrow ndio ilikuwa inaongoza duniani kwa usalama mdogo.. Yaani kila aina ya ubaya iko hapo
Ujambazi
Wizi
Uporaji
Utapeli
Umalaya
Ushoga
Mauaji
Nknk..
Nitaendelea..
 
Back
Top Bottom