Endelea mkuu...hizi story za kusafiri zinanimalizia sana mabando yangu kule youtube....nazipenda sana yan
Basi nikiwa bado na kihoro cha lile tukio nikaendelea kuwasiliana na mtu aliyekuwa anakuja kunipokea ..Alikuwa ni raia wa nje
Akanieleza kwamba hapo nilipo ndio palikuwa kitovu cha matukio yote mabaya na ya kutisha, hivyo tukapeana muda kwamba exactly baada ya dk 10 nikamate briefcase yangu nitoke nje
Hapo atakuwa amefika, then nitapanda na tutaondoka! Pale kwenye simu upande wa pili kwenye kona walikuwepo watu wawili, ni kama walikuwa wananilia radar hivi
Basi dakika 9 na nusu nilikamata briefcase na kutoka nje kwa kasi.. Nafika nje kuna VW Jetta inasimama
Nilifungua mlango nikaingia kwa kasi na dereva akaamsha kwa spidi
Ninachokumbuka ni kuwaona wale jamaa wameshafika mlangoni mwa ile hotel na kubali kuninyooshea vidole huku wakitikisa vichwa😂
Mwenyeji wangu alikuwa mwanamke mwenye stamina nzuri na usukani. Akaniambia mumewe ana mwezi tangu auliwe viunga vya huo mji
Akaniambia mtu mwingine asingejaribu kufika pale nilipokuwa tens usiku kakini yeye alijitoa mhanga ili kuokoa maisha yangu kwakuwa pale nilipokuwa nisingepona
Tulifika kwake salama nikapata huduma zote muhimu nikalala vizuri na kesho yake akanipeleka chuoni
Yule Mkenya classmate wangu hakuwahi tena kufika south bali baada ya kumalizana na uhamiaji walimrudisha boda akarudi Kenya lakini baadae alijilopua tens na kukimbilia Sweden anapoishi mpaka Leo
Yule niliyemuacha pale hotelini sijawahi kujua chochote tena kumhusu..!
Sasa hiyo ilikuwa 1998 imagine sasa hivi South pakoje!