Naendelea sasa..!
Mwaka 1998 nilirudi Tz likizo kwa mara ya kwanza.. Ile kumaliza likizo nikaugua malaria na kulazwa siku moja kabla ya safari.. Hivyo shirika la ndege Alliance airline bythen wakakata almost 40% ya ticket na kunidushia pesa iliyobaki
Baada ya kupona nikawa sina nauli ya kutosha kupanda ndege hivyo nikaondoka na treni mpaka Kapiri Mposhi Zambia (hii safari ikawa na vituko vyake vingi sitavisimuia hapa)
Tuliondoka Dar Ijumaa jioni pale Tazara na kufika salama Zambia Mji wa Kapiri Mposhi Jumapili asubuhi
Pale nikachukua basi mpaka Lusaka na kufika mchana.. Nilipata hotel nikalala mpaka kesho yake siku ya Jumatatu
Nilienda stand na kufanikiwa kupata basi la South kupitia Zimmbwe.. Nikiwa ndani ya bus nikakutana na jamaa yangu mkenya naye katoka likizo.. Safari ikaanza
Tulisafiri mchana kutwa mpaka jioni tukafika mpakani mwa Zambia na Zimbabwe