GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 7,646
- 10,859
Afrika ni ara zuri. Limebarikiwa rasimali kede kede, lakini haziwanufaishi wananchi wake.
Afrika ni bara kubwa. Lina mchango mkubwa sana kwa mataifa mengi ya Magharibi, hasa katika suala zima la malighafi na nguvu kazi.
Katika miaka ya hivi karibu, kumeibuka baadhi ya watu walioonesha dharau za wazi kwa bara la Afrika.
Madhalani, mwaka 2018, aliyekuwa Rais wa Marekani, Donald Trump, alizitukana nchi za Kiafrika kwa kuziita SHITHOLE COUNTRIES.
AU ilielezea kuchukizwa na hilo na kumtaka Trump kuomba msamaha. Sijui kama "agizo" lao lilitekelezwa au lilichochea matusi zaidi.
Kwa tusi hilo, Afrika haikuwa na uwezo wa kuchukua hatua zaidi ili kuonesha ulimwengu kuwa siyo Shithole countries kama Trump alivyoudanganya ulimwengu?
Kioja kingine ni kile kilichofanywa na Mwafrika kutokea nchini Ghana mnamo mwaka 2022. Mfanyabiashara huyomaarufu, Dr. Kofi Asamoah, "alizua" taharuki kwa kumshauri Elon Musk alinunue bara la Afrika na kisha "kuwadelete" viongozi wake wote.
Sikusikia kama AU ilitoa tamko kumkemea Dr. Kofi, au hata nchi yake "kumshikisha" adabu.
Inamaana kwamba Afrika ilishindwa "kumshughulikia" hata raia wake aliyeikejeli? Au tuseme alichosema huyo mfanyabiashara tajiri kina "kaukweli" ndani yake?
Afrika ilishadharauliwa na Wazungu, lakini ni sawa na Waafrika nao kujidharau? Hizo dharau mpaka lini?
Afrika ni bara kubwa. Lina mchango mkubwa sana kwa mataifa mengi ya Magharibi, hasa katika suala zima la malighafi na nguvu kazi.
Katika miaka ya hivi karibu, kumeibuka baadhi ya watu walioonesha dharau za wazi kwa bara la Afrika.
Madhalani, mwaka 2018, aliyekuwa Rais wa Marekani, Donald Trump, alizitukana nchi za Kiafrika kwa kuziita SHITHOLE COUNTRIES.
AU ilielezea kuchukizwa na hilo na kumtaka Trump kuomba msamaha. Sijui kama "agizo" lao lilitekelezwa au lilichochea matusi zaidi.
Kwa tusi hilo, Afrika haikuwa na uwezo wa kuchukua hatua zaidi ili kuonesha ulimwengu kuwa siyo Shithole countries kama Trump alivyoudanganya ulimwengu?
Kioja kingine ni kile kilichofanywa na Mwafrika kutokea nchini Ghana mnamo mwaka 2022. Mfanyabiashara huyomaarufu, Dr. Kofi Asamoah, "alizua" taharuki kwa kumshauri Elon Musk alinunue bara la Afrika na kisha "kuwadelete" viongozi wake wote.
Sikusikia kama AU ilitoa tamko kumkemea Dr. Kofi, au hata nchi yake "kumshikisha" adabu.
Inamaana kwamba Afrika ilishindwa "kumshughulikia" hata raia wake aliyeikejeli? Au tuseme alichosema huyo mfanyabiashara tajiri kina "kaukweli" ndani yake?
Afrika ilishadharauliwa na Wazungu, lakini ni sawa na Waafrika nao kujidharau? Hizo dharau mpaka lini?