Afisa mwanadamizi wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa TAKUKURU katika wilaya ya Ngara mkoani Kagera amejiua kwa kujipiga risasi kidevuni
afisa huyo bw Francis Kitundu amejiua kwa kujipiga risasi leo saa nne asubuhi baada ya kutoka kwenye kikao cha ndani cha kujadili shughuli za taasisi hiyo.
Mkuu wa Takukuru wa wilaya ya Ngara bw. Stewart Kiondo amesema muda mfupi baada ya afisa huyo kutoka kwenye chumba cha mkutano walisikia mlio wa risasi na walipokwenda walimkuta amelala chini baada ya kujipiga risasi kwa kutumia bastola.
Amesema mwenzake huyo ambaye ni mwenyeji wa mkoa wa Iringa amefariki wakati alipofikishwa kwenye hospitali ya Nyamiaga wilayani Ngara ili kujaribu kuokoa roho yake