bwege nazi
JF-Expert Member
- Sep 25, 2018
- 700
- 901
Aisee we jamaa una chuki za wazi wazi na imani za watu wengine.. ukiambiwa uthibitishe huo uchawi aliorogwa utathibitisha? Mbona unakuwa na kashfa zisizokuwa na mpango! Au chukulia kafa baba yako mzazi kisha mtu kaja kaleta uzi kama huu vipi utajifeel! Kuwa mstaarabu, id fake na kusema nyuma ya keyboard isikufanye ukaandika vitu vinavyowakwaza watu wengine. Aliekwambia kuwasomea watu dua unakuwa tajiri mpaka wamroge marehemu kamanda ni nani? Hayo mambo yapo upande wenu unaanzisha kanisa lako unauza vitambaa vya upako, maji ya upako, mafuta ya upako etc. Hebu niambie shehe gani hapa bongo kazi yake kusoma dua kawa tajiri kumshinda mzee wa upako, gwajima, kakobe, mwamposa etc. Hayo mambo huku kwetu hakuna.. huyo kamanda r.ip alikuwa akisoma kwa mapenzi ya mwenyezimungu na wala si kutafuta chochote.Wachawi nawajua kama mi ndo nimewaumba vile. Kitaa nnachotoka mimi uswazi ni nyumba mganga, nyumba mchawi, nyumba mganga nyumba mchawi.
Mjomba mganga Shangazi mchawi. Mama mganga, mama wa Kambo mchawi.
Watoto wadogo vbaka machokoraa, dada zao malaya, Kaka zao majambazi.
Chimba fukia vunja Nazi nuia ndo daily life style.
Saikolojia ya Wachawi naifahamu kama samaki wanavyo Jua kuogelea.
Kuna kitu kimoja ambacho ni common karibu Kwa Wachawi wote. Wachawi wanapenda Sana Comouflage. Wanapo piga tukio la kichawi huwa Wana dress up the scene to make it look like something else.
Mfano wake ni kama kisa cha Yusufu na nduguze.
Baada ya Ndugu WA Yusufu kumuuza utumwani ndugu yao walichinja kondoo damu ya kondoo waka paka kwenye kanzu ya Yusufu kisha wakaenda kumpiga sound Mzee Yakobo kwamba mwanae ameuwawa na Simba.
Mzee alipo tazama kanzu ya mwanawe ilivyo chanwa chanwa na kuloa damu kweli aka amini mwanae ameuwawa na Simba.
Babu WA watu akamwaga chozi aki amini mtoto wake ameuwawa na Simba kumbe yupo kachukuliwa kapelekwa utumwani kama watu wengi Leo hii mnavyo walilia ndugu zenu mkiamini wamekufa kumbe wamechukuliwa utumwani usukuleni.
Mwaka 93 when I was still a Lil Bow Wow. Nilikuwa darasa la pili. Kuna Jamaa aliitwa Kobelo huyu alikuwa amemaliza la Saba tayari and he was like 18.
Jamaa alikuwa anaupiga mpira Mwingi hatari Kwa walio kuwa wanamfahamu Huyu Jamaa ambae kitaani alipewa jina Kipese akifananishwa na Thomas Kipese, na ambao walifariki at around 92 au 93 before December , basi huko mbinguni walipo watakuwa wanajua Huyu Jamaa huku duniani atakuwa ana chezea Barcelona au Real Madrid.
Mwaka Huo Pamba ya Mwanza walikuja Darusalama kucheza na Simba. Mjomba wa Kobelo akaenda kuongea na viongozi wa Pamba ya Mwanza Kobelo afanye nao mazoezi. Pamba ya kina Alphonce Modest.
Viongozi wakakubali na kweli Kobelo akaenda kufanya mazoezi na Pamba. Unaambiwa kiwango alicho kionyesha wazee wakamuelewa Sana wakaomba kuondoka nae Mwanza ili asaini Pamba msimu wa mwaka 94
Ilikua ni siku ya Jumatano. Mechi ya Pamba na Simba Jumamosi jumatatu Kobelo anatakiwa kusafiri na Pamba Hadi Mwanza.
Kwa kiwango cha Kobelo kama aangesaini Pamba basi msimu uliokuwa unafuata lazima Ange saini Simba au Yanga.
Habari zikatapakaa kitaani.
Jumamosi kukawa na harusi. Hizi harusi zetu za Kiswahili za watu kuoana bila dating. Kobelo alikuwa ni mmoja wa walio hudhuria harusi hiyo. Ilikua ni ya ndugu wa ukoo wake. He was lured to attend.
On the fateful day Kobelo anaenda kwenye harusi, Kobelo anakula Pilau baadae anarejea nyumbani kwao masaa kabdhaa badae tumbo kichwa kinaanza kumu Uma.
Maumivu yanaendelea kidogo kidogo. Joto linapanda Kwa Kasi ya ajabu Sana kiasi ungeweka sufuria la maji ya baridi kichwani kwake na baada ya dakika kadhaa maji yangechemka kama maji ya kunyonyolea kuku.
Kobelo anakimbizwa hospital. He dead on the arrival. Kumbe they didn't know he was gone toka enzi za Pontyo wa Pilato.
Safari ya Kobelo ikaishia hapo.
Back kwa Afande Ustaadh. Kifo chake kinaweza kuwa the handwork of his village people
Kwanini wamroge?
Kwa sababu ya kipaji chake cha kuhifadhi Aya za Qur'aan Tukufu.
Kwanini?
Kwa sababu ni utajiri. MTU mwenye karama hiyo Hawezi kuwa masikini hata siku moja.
Watu walishaanza kumuona na Alisha Anza kuwa maarufu. Na kama angekuwepo basi bila Shaka baada ya muda mfupi angeanza kupata mialiko ya ndani na Nje ya nchi kwenda kuwasomea watu dua. Baada ya muda mfupi sana.huyu Jamaa angekuwa milionea.
So Kuna uwezekano mkubwa Sana Huyu Jamaa akawa ametupiwa mdudu na watu WA nyumbani kwao.