Afande mabawa

Afande mabawa

engmtolera

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2010
Posts
5,149
Reaction score
1,441
Jeshi la Uchina limetangaza kutoa ajira kwa njiwa elfu kumi.
080625mensajeras400a.jpg


Njiwa akibebeshwa ujumbe


Njiwa hao wameajiriwa ili waweze kutimika kwa ajili ya mawasiliano, iwapo itatokea siku ambayo njia za kawaida za mawasiliano zitaharibika, au kukwama. Kituo cha televisheni cha Uchina CCTV kimesema ajira hiyo imetolewa na Jeshi la Ukombozi la watu wa China.

Taarifa zinasema tayarinjiwa hao wameanza kupewa mafunzo, katika jiji moja katikati ya Uchina.
100927160547_pigeon_medal_226x170_nocredit.jpg




Afande..

Jeshi hilo la njiwa litatumika katika siku ambayo mawasiliano yataharibika, na kazi yao itakuwa kuwasilisha ujumbe muhimu. Maafande hao wenye mabawa pia watakuwa wakipewa kazi nyeti za kijeshi. Njiwa wamekuwa wakifanya kazi katika jeshi la Uchina tangu miaka ya hamsini, ingawa sio kwa kiasi kikubwa kama hawa walioajiriwa sasa.
 
Hii ni techolojia ya siku nyingi sana, naona Wachina wameamua kuiendeleza tu.

Pitia HAPA
 
Back
Top Bottom