Mmeshaanza kutubu wakati mlisema Bora Magufuli afe aje yeyote yule kutakuwa safi .
Ndio maana
Kiranga alisema wabongo wanaangalia simple solution kwenye ishu ngumu ambazo hazihitaji shortcut na wengi hawana principlees wanaangalia mtu .
Hawa hawaelewi kuwa kuna mengi yanayoendelea sasa yasingewezekana bila kuwekewa msingi na Magufuli.
Hawaelewi uongozi wa CCM ni kama mbio za kupokezana kijiti, na unachoona kinatokea sasa kisingeweza kutokea hivi bila ya hao wa awali kuweka mazingira ya haya kutokea.
Wananikumbusha kuna wakati nilikaa na rafiki zangu, tukawa tunauchambua uongozi wa Kikwete. Mmoja akasema Kikwete ni rais dhaifu sana, mbovu sana, hatakuja kamwe kutokea rais mbaya kama Kikwete Tanzania.
Mimi nikawaambia tulieni tu, mtaona zaidi.
Nilijua kuwa, ubaya wowote atakaoufanya Kikwete, ataufanya uwe wa kawaida kwa anayemfuatia, na anayemfuatia atafanya ubaya zaidi, kwa sababu Kikwete atakuwa kashashusha standards. Kaweka "the new normal" ya standards za chini zaidi. Ni kama viongozi wanashindana kuharibu.
Na kweli, baada ya Kikwete akaja Magufuli akafanya vilevile nilivyosema. Mpaka watu wakawa wanamtamani Kikwete arudi kipindi cha Magufuli.
The same thing is happenning now. Magufuli kashusha standards, Samia kaziondoa kabisa.
Watu wanamuona Magufuli afadhali, lakini hawaelewi haya madudu ya Samia yasingewezekana kama Magufuli asingeshusha standards.