Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 3,119
- 1,428
ADV. STEPHEN BYABATO AMPIGIA CHAPUO KWA WANANCHI ENG. MUTASINGWA, UBUNGE BUKOBA MJINI
Salaam sana ndugu zangu
Naomba tusambaze ujumbe huu
Leo jumatatu ni siku ya tatu tangu Halmashauri Kuu ya CCM Taifa iteue wagombea Ubunge na Bukoba Mjini ikatuletea ndugu yetu Eng Johnston Johansen Mutasingwa, tumempokea kwa mikono miwili kama ilivyo jadi yetu katika Chama chetu.
Wakati wa mchakato kila mtia nia alipata kuungwa mkono na watu kadhaa, mwisho wa mchakato maamuzi ya H/Kuu yametupatia jina moja ambavyo kwa vyovyote ilitakiwa mwisho apatikane mmoja katika wale makada wetu wazuri 5, Mwenyezi Mungu kampa nafasi Eng. Mutasingwa.
Kwa siku mbili hizi kumekuwa na furaha au masikitiko au kuwa kawaida kwa watu mbalimbali kulingana na mapokeo ya uteuzi, hili lazima litokee, lakini halitakiwi kudumu. Kitaalamu wanasema ukiwa na jambo ndani ya moyo inabidi ulitoe ili upone nafsi lakini lisipitilize kiasi na kuleta madhara.
Ni kwa mantiki hiyo, mimi Adv. Stephen Byabato (Mbunge niliyemaliza muda wangu Jimbo la Bukoba Mjini) nawaomba wana CCM na wana Bukoba wote sasa tuungane kumpa ushirikiano mteule wetu ili turudi kazini mapema na kuijenga Bukoba yetu. Kwa sasa naamini kila mtu amepumua na hatujafika kwenye madhara, na tusifike huko na atakayetaka kutupeleka huko tumkatae na tumuone ni adui wa Bukoba yetu na sasa sote tuwe tayari kushirikiana kwa pamoja kuhakikisha Mgombea kwa tiketi ya CCM anapata ushindi wa kishindo ili Bukoba tuzidi kusonga mbele.
Ninawaomba na kuwasihi wapenzi wa kila upande sasa tuwe wamoja, tuvumiliane, tukubaliane, tushirikiane na ni kwa ajili ya maslahi mapana ya kuleta maendeleo ya Bukoba Mjini.
Asanteni sana. Ndimi kijana wenu
Adv. Stephen Byabato
Bukoba Mjini
25/07/2025