Adhabu za wanajeshi

Kaka usimalize maneno... Wako watu watata na wanajua mchezo ya hatari.. Ila ukiyaingia kwa wanajeshi Kua mpole
Wana nini? Kama bunduki hata sisi tunazo Tena Kwa kibali maalum, wakimwaga mboga namwaga ugali, nitahakikisha nakufa na wawili au watatu kama hamza na hawatokaa wanisahau Kwa ushenzi ntakao wafanyia

Tatizo lenu wabongo mnaasili ya uoga wa kifala, jaribuni kuchanganya dam mzae hata na waarabu na wasomali mjaze kizazi Cha majasiri na wenye kujitoa mhanga
 

Jambo la ajabu Sana
 

Aisee kabisa tena mambo mengine ya ajabu

Kuna siku pale machava niliona Mzee anarushwa kichura et kisa ametema mate eneo la jeshi
 
Watu Kama wewe ndiyo mnakuwaga wapole Kama mmemwagiwa maji mkiwaona bakabaka. Ila kwa background mnaandika kishujaa Kama hivi.

Keyboard warrior.
Mimi Nina damu ya kiarabu, Nasemeje Kuna haja ya wabongo kuzaa na waarabu na wasomali tupate wapambanaji walio tayari kujitoa muhanga kwaajili ya kutetea haki, wabongo mnaasili ya kauoga, Mimi sipo hivo, Mimi Nina dam ya kiarabu nipo Razi kuvaa bomu nikafe na washenzi buku kuokoa taifa
 
Sahihi.
 
Kijana utajaa tu siku moja ndio utajua wajenda ni vichaa zaidi yako. Utanyooshwa na jamaa ukimshtaki afukuzwi kazi
 
Tena wewe ndiyo utakuja kuumizwa kabisa ukileta ujinga huo. Kule kuna watu wameshindikana na zaidibya wahuni, ukitaka ukae nao wale kwa amani punguza ujuaji
Muache mjuaji huyo akojaa18 atakubali mziki.
 
Nasemaje!, usije kutana na hao watu ukaleta ujuaji, utaumia mzee baba!. Nasema utaumia sababu hakuna atakayeajibishwa kwa wajeshi wa nchi hii. Bro wangu mmoja hivi alikutana na kisanga pale makongo kipindi anasoma pale Tumaini bachelor of laws, alileta ujuaji wa sheria lkn kilichokuja kumpata hatasahau maisha yake yote.
Wale wana wanatumia neno AMRI, zingatia sana hilo neno usije jichanganya aisee...
 
Acha uoga ww jambo lakwanza ww kamata ile number yake kwisha habari yake akikuamrisha chochote kilicho na element ya udhalilishaji usifanye.
 
Dogo acha ujinga we na huyo bro wako wazazi walipoteza ada wakapeleka ng'ombe shuleni unatoa mfano wa bro wakati mimi binafsi nimeshawaonya hao wanajeshi kufanya vitendo ambavyo viko kinyume na maadili ya jeshi na kuvunja sheria? Hivi unajua kosa lolote la jinai ikiwepo kumshambulia mtu ni kosa la kufukuzwa kazi kwenye majeshi ya ulinzi?

Sasa kawatishe wajinga wenzako mtaani usituletee utoto hapa
 
Acha uoga ww jambo lakwanza ww kamata ile number yake kwisha habari yake akikuamrisha chochote kilicho na element ya udhalilishaji usifanye.
Rejea hiyo story yangu kisha mengine jiongeze. Huyo bro wangu alifanya kila ujanja, kilichomtokea hakisimuliki ww.
Jamaa baada ya kwenda kwa viongozi kaongezewa adhabu nyingine.
Haya mambo tuyaache tu
 
Sina cha kukujibu kaka mkubwa maana naona tutadhalilishana tu
 
tanga nini hii
 
Rejea hiyo story yangu kisha mengine jiongeze. Huyo bro wangu alifanya kila ujanja, kilichomtokea hakisimuliki ww.
Jamaa baada ya kwenda kwa viongozi kaongezewa adhabu nyingine.
Haya mambo tuyaache tu
Hakuna mtu ambaye Yuko juu ya Sheria. Panda mbele mahakamani kafungue kesi,
 
Rejea hiyo story yangu kisha mengine jiongeze. Huyo bro wangu alifanya kila ujanja, kilichomtokea hakisimuliki ww.
Jamaa baada ya kwenda kwa viongozi kaongezewa adhabu nyingine.
Haya mambo tuyaache tu
Alitakiwa apande juu zaidi baada ya aliekwenda kumshatakia kutomsikiliza lao lilikuwa moja

kuna rafiki yangu aligongewa bajaji yake nagari yao ya jeshi kosa lilikuwa la mjeda na driver bajaji aliogopa kwahizo amri zao. Driver akampigia bosi wake ambae ndo rafiki yangu wakati mm nipo nikamwambia fukuzia na boda chukua hiyo plate number.

Unafikiria tuliangaika sana waliitengeneza hiyo bajaji kwahela zao zamfukoni baada yakujua walipo.

Hayo mambo yalikuwa zamani kuhalalisha kosa lao kuwa haki kwao.
 
Ukiwa ndezi,ndo utazidi kuumia zaidi
Jaribu uende kuleta ujuaji wako, utasimulia hadi wajukuu kitakachokupata. Wanajeshi epuka sana akiwa yupo eneo la kazi na hapo ulimkuta alipangiwa jukumu fulani, kazi ikiharibika anaadhibiwa na kuliko litokee hilo ndiyo anakuzingua. Kama huyo wa lori aliyekutana na MP, wale kituo chao cha kazi ni hapo getini kama angekutwa na wakubwa geti limezibwa hivyo angezinguliwa na ndiyo hapo aliamua kumzingua yeye.

Cheza na mwanajeshi sehemu zingine zote ila si eneo lake la kazi, wanaadhibiwa adhabu mbaya sana wale jamaa au kutukanwa kabisa na wakubwa kama mambo yakienda hovyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…