Adabu zimeshikwa; CCM waliahidi, wametenda

Adabu zimeshikwa; CCM waliahidi, wametenda

Amani Msumari

JF-Expert Member
Joined
Aug 21, 2016
Posts
1,833
Reaction score
979
CCM ipo sana kwenye hatamu za uongozi wa Tanzania.

Kila baada ya muda flani, CCM hujutafakari na kujiunda upya. Hii ni sifa muhimu sana kwa chama cha siasa. Mnayoyaona yanatokea leo, hayatokei kwa bahati mbaya, ni mipango Mahususi kutoka kwa mabingwa wa siasa.

Tuliahidi kushikisha watu adabu na kuleta mgombea anayekubalika. TUMETEKELEZA kwa vitendo. Wala rushwa waliotaka kukinajisi chama wameshikishwa adabu kwa kukatwa majina yao.

Aidha, ilishasemwa, nami nasisitiza; kushinda kura za maoni sio kushinda uteuzi, ni sehemu ya mchakato. Chama kina macho na masikio mengi na ndio sababu kwenye baadhi ya maeneo wameteuliwa watia nia ambao hawakuongoza. Moja ya sababu ni uwezo binafsi wa mgombea kupambana na mgombea wa upinzani katika Jimbo husika.

Kwa safu hii, CCM inaenda kushinda kwa kishindo. Shime wanaCCM popote mlipo, tuungane kuhakikisha chama kinapata ushindi wa kishindo wakihistoria. Wapinzani wetu WAMESHATEPETA.
 
Mkuu, kuna kauli na misemo ya kichama imetolewa mara kwa mara mpaka sasa imeshachosha kusikika tena masikioni mwa Watanzania. Kuiweka awamu hii kama alama yenye kukumbukwa ktk mapambano dhidi ya ukiukwaji wa haki za binadamu na rushwa itakuwa ni kitu cha ajabu mno.

Wana CCM Wana kwa mbwembwe wanajisifu kwa ujenzi wa miundombinu na kuongezeka kwa huduma za afya na elimu, lkn wanasahau jambo moja muhimu kuwa hayo yote hufanyika kwa kupitia kodi na maduhuli mengine yalipwayo katika fuko la hazina, vilevile na mzigo wa madeni makubwa ambao wanatubebesha Watanzania wote yakifanyika kwa usiri mkubwa.

CCM kama chama tawala pekee hapa toka wakati wa uhuru, kimepewa ridhaa ya kuiongoza serikali, hivyo kupata uhalali wa kumiliki fuko la hazina. Kwa hiyo hizo kauli za sijui kujibadilisha, sijui tumeweza kutekeleza, na upuuzi mwingine kama huo zinakerehesha sana.

Ni kutaka kutafuta kiki ili kujipa "ownership" kwa vitu ambayo kimsingi ni vya kawaida kufanywa na serikali yoyote ile duniani. Hzo kauli ndizo huwafanya wana CCM kuwa wavivu ktk kufikiri na hata kuona mambo mengine mazuri nje ya kasha la fikra pana na maono sahihi kwa mustakabali wa Taifa letu.
 
Mkuu, kuna kauli na misemo ya kichama imetolewa mara kwa mara mpaka sasa imeshachosha kusikika tena masikioni mwa Watanzania. Kuiweka awamu hii kama alama yenye kukumbukwa ktk mapambano dhidi ya ukiukwaji wa haki za binadamu na rushwa itakuwa ni kitu cha ajabu mno.

Wana CCM Wana kwa mbwembwe wanajisifu kwa ujenzi wa miundombinu na kuongezeka kwa huduma za afya na elimu, lkn wanasahau jambo moja muhimu kuwa hayo yote hufanyika kwa kupitia kodi na maduhuli mengine yalipwayo katika fuko la hazina, vilevile na mzigo wa madeni makubwa ambao wanatubebesha Watanzania wote yakifanyika kwa usiri mkubwa.

CCM kama chama tawala pekee hapa toka wakati wa uhuru, kimepewa ridhaa ya kuiongoza serikali, hivyo kupata uhalali wa kumiliki fuko la hazina. Kwa hiyo hizo kauli za sijui kujibadilisha, sijui tumeweza kutekeleza, na upuuzi mwingine kama huo zinakerehesha sana.

Ni kutaka kutafuta kiki ili kujipa "ownership" kwa vitu ambayo kimsingi ni vya kawaida kufanywa na serikali yoyote ile duniani. Hzo kauli ndizo huwafanya wana CCM kuwa wavivu ktk kufikiri na hata kuona mambo mengine mazuri nje ya kasha la fikra pana na maono sahihi kwa mustakabali wa Taifa letu.
Mbenge,
Kila mtu ashinde mechu zake na mtu hahukumiwi kwa dhambi ya baba yake.

Kuihukumu serikali ya awamu ya tano kwa ishu za awamu ni kutaka kupoka haki ya serikali hii ambapo watanzania hilo wamelikataa.

Kuhusu Kodi elewa kuwa hata Sudani ya kusini na Somalia pia wanakusanya Kodi. Ishu hapa ni matumizu sahihi ya kodi hiyo

CCM chini ya Rais Magufuli imefanya kwa vitendo. Ndugu yangu, kura yako ni ya thamani sana, kura yako mpe John, mpe mbunge na diwani wa CCM kwasababu mwaka huu tumewaletea kile kilicho bora kabisa, ile kitu roho inasuhuzika
 
kweli magu kafanya makubwa 😁😁
 

Attachments

  • 2471622_IMG-20200728-WA0016.jpeg
    2471622_IMG-20200728-WA0016.jpeg
    41.1 KB · Views: 5
Mbenge,
Kila mtu ashinde mechu zake na mtu hahukumiwi kwa dhambi ya baba yake.

Kuihukumu serikali ya awamu ya tano kwa ishu za awamu ni kutaka kupoka haki ya serikali hii ambapo watanzania hilo wamelikataa.

Kuhusu Kodi elewa kuwa hata Sudani ya kusini na Somalia pia wanakusanya Kodi. Ishu hapa ni matumizu sahihi ya kodi hiyo

CCM chini ya Rais Magufuli imefanya kwa vitendo. Ndugu yangu, kura yako ni ya thamani sana, kura yako mpe John, mpe mbunge na diwani wa CCM kwasababu mwaka huu tumewaletea kile kilicho bora kabisa, ile kitu roho inasuhuzika
Unajidanganya wewe

Sent from my Nokia 2.3 using JamiiForums mobile app
 
Mbenge,
Kila mtu ashinde mechu zake na mtu hahukumiwi kwa dhambi ya baba yake.

Kuihukumu serikali ya awamu ya tano kwa ishu za awamu ni kutaka kupoka haki ya serikali hii ambapo watanzania hilo wamelikataa.

Kuhusu Kodi elewa kuwa hata Sudani ya kusini na Somalia pia wanakusanya Kodi. Ishu hapa ni matumizu sahihi ya kodi hiyo

CCM chini ya Rais Magufuli imefanya kwa vitendo. Ndugu yangu, kura yako ni ya thamani sana, kura yako mpe John, mpe mbunge na diwani wa CCM kwasababu mwaka huu tumewaletea kile kilicho bora kabisa, ile kitu roho inasuhuzika
Amani,
Suala la uthamani wa kura yangu nalitambua sana, ndiyo maana nataka kwanza kusikiliza sera za vyama vilivyopo ktk kinyang'anyiro na pia kupima umakini na uthabiti wa hoja wa wagombea mbalimbali ambao wameaminiwa kuzipeperusha bendera za vyama vyao.

Jukumu langu ni kuwapima, kuwachuja na hatimaye kujridhisha kuwa nani hasa ambaye nipaswa kumtendea haki kwa kumpa kura yangu. Kwa nafasi ya uraisi nitazingatia ubora wa kunadi sera zao bali kwa mbunge na diwani nitaangalia wasifu wao wa utendaji kwa kwa nafasi ambazo walikwisha wahi kuzitumikia.

Rais ni mtu ambaye anaweka matumaini ya kesho ya Watanzania kupitia kuitii, kuitunza na kuilinda katiba ya nchi yetu, sheria, kanuni na taratibu zake kama vile zinavyoainishwa. Sitegemei kumsikia mgombea wa nafasi ya urais akijinadi kwa kutaja majukumu yake ya kila siku kama ndiyo "benchmark" ya mafanikio yake.

Zaidi tunatarajia kuwasikia wakinadi sera za kuleta mageuzi makubwa ya kijamii na kiuchumi na huku wakijipambanua kwa kudumisha umoja wa Taifa letu. Watanzania wanahitaji haki wala siyo utulivu ambao umefichwa ndani ya neno "AMANI"
 
Amani,
Suala la uthamani wa kura yangu nalitambua sana, ndiyo maana nataka kwanza kusikiliza sera za vyama vilivyopo ktk kinyang'anyiro na pia kupima umakini na uthabiti wa hoja wa wagombea mbalimbali ambao wameaminiwa kuzipeperusha bendera za vyama vyao.

Jukumu langu ni kuwapima, kuwachuja na hatimaye kujridhisha kuwa nani hasa ambaye nipaswa kumtendea haki kwa kumpa kura yangu. Kwa nafasi ya uraisi nitazingatia ubora wa kunadi sera zao bali kwa mbunge na diwani nitaangalia wasifu wao wa utendaji kwa kwa nafasi ambazo walikwisha wahi kuzitumikia.

Rais ni mtu ambaye anaweka matumaini ya kesho ya Watanzania kupitia kuitii, kuitunza na kuilinda katiba ya nchi yetu, sheria, kanuni na taratibu zake kama vile zinavyoainishwa. Sitegemei kumsikia mgombea wa nafasi ya urais akijinadi kwa kutaja majukumu yake ya kila siku kama ndiyo "benchmark" ya mafanikio yake.

Zaidi tunatarajia kuwasikia wakinadi sera za kuleta mageuzi makubwa ya kijamii na kiuchumi na huku wakijipambanua kwa kudumisha umoja wa Taifa letu. Watanzania wanahitaji haki wala siyo utulivu ambao umefichwa ndani ya neno "AMANI"
Sawa. Hayo yote unayoyataja, mgombea wetu anayo
 
Back
Top Bottom