Uchaguzi 2020 ACT Wazalendo, Time is making ability tuleteeni Membe sasa, hakuna muda tena wa kupoteza

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,502
51,098
Tumebakisha miezi mitano ya uchaguzi. Muda haupo upande wenu, wananchi tunangoja kwa hamu kuona mnatuletea mgombea bora, makini, mzalendo, mweledi na anayeweza kurekebisha makosa makubwa mno yaliyofanywa na serikali ya awamu hii ili. kuirudisha nchi katika msitari sawasawa kstika nyanja za kiuchumi na kisiasa. Katika muktadha huu mnapaswa kufanya maamuzi magumu, bila kuchelewa, Muda wa kusimama na kufanya maamuzi ni sasa, kesho mtakuwa mmechelewa.

1. Ipo haja ya kumchallenge rais Magufuli kwa nguvu zote kwenye uchaguzi wa october 2020

Si vyema kumpa rais Magufuli ushindi wa mezani, ushindi lainilaini ushindi wa kupewa, Ni lazima awekwe mtu mwenye charisma zaidi, mwenye historia ya kutukuka zaidi katika utumishi wa wananchi ili ashindane naye, Ili raisi Nagufuli naye aumize kichwa, atumie muda wake kutafuta kura za wananchi, aende kwa wananchi awaangalie machoni na kuwaambia kuwa niliahidi kadha wa kadha na nimetekeleza moja, mbili, tatu. Kutomchallenge Magufuli ni kumfanya ajihisi invinsible na hii inaweza kuathiri utendaji wake iwapo atashinda uchaguzi kwa kuamini kuwa alikuwa entitled kwenye uraisi badala ya kujua kuwa yeye kuwa hapo ni kwa sababu ya ridhaa za watu. Kwa sasa sioni mtu aliyejiandaa kumkabili raisi Magufuli kwenye sanduku la kura kuliko Membe

2. Upo umuhimu wa kupata uungwaji mkono wa kimyakimya kutoka kwa makundi yasiyomkubali Magufuli ndani ya CCM (Latent support)

Rais Magufuli anao mahasimu wake wa kisiasa ndani na nje ya CCM. The best thing cha kufanya sasa hivi ni kuunganisha nguvu hizi mbili, moja ya dhahiri na nyingine ya siri. Ili kuerode cohesion ya CCM katika kuelekea uchaguzi mkuu, ipo haja ya kukifanya chama kizima kisiwe united firm chini ya Magufuli, kuna haja ya kuwa na support ya mtandao wa kimya kimya, Kwa sasa sioni hata kidogo mtu kutoka upinzani anayeweza kuexploit ufa huu ndani ya CCM zaidi ya mtu aliyekuweko ndani ya CCM, anayeijua CCM na ambaye ameonyesha nia ya kuchallenge status quo. Katika hili sioni mtu mujarrabu anayeweza kuifanya kazi hii kuliko Membe

3. Msiogope Lowasa precedence (kuhama kisha kurudi CCM)

Lowasa na Membe ni stori mbili tofauti, mmoja alikatwa kugombea urais, hakufukuzwa chamani akaamua kukimbilia upinzani kutafuta urais, huyu wa pili kafukuzwa humohumo ndani ya Chama kwa hila kisa tu kasimama kidete kumchallenge bwana mkubwa na pia kaonyesha nia thabiti ya kugombea uraisi ili aje awatumikie Watanzania. Kwa hiyo katika kumuevaluate Membe inabidi mumuone kama mtu shujaa aliyekuwa tayari kusimama na kumwambia mfalme kuwa hautoshi, umetukwamisha sana, umetuingiza chaka sana, umetupeleka maboya sana, sasa tunataka kuingia hapo ulipo ili turekebishe mambo. Huyu mtu ni mtu jasiri, ameonyesha ujasiri hata pale ndani ya chama chake walipoufyata, kwa hiyo huyu mtu siyo wa kuacha hivi hivi. Huyu mtu anafaa kushika bendera ya ACT na kuipeperusha vyema kumng'oa bwana mkubwa. Msiogope kelele za hofu kuwa akija Membe itakuwa kama ilivyokuwa Lowasa alipohamia CHADEMA. Lowasa na Membe kihulka ni watu wawili tofauti

4. ACT Wazelendo ni chama cha Wahanga wa kisiasa, Ni Tanga la kunusuru waliotoswa baharini kionevu

Kuanzia kuondoka kwa Kiongozi mkuu wa Chama mheshimiwa Zitto Kabwe kwenye chama chake cha awali, Kuja kwa Maalimu Seif na wengineo, Kwa nini iwe nongwa kumchukua Membe?. Membe siyo liability, Membe ni assett, Na asset yake kubwa ni uzalendo na utumishi uliotukuka kwa nchi hii. Membe hana hela, lakini ana plan ya kuwaondoa wananchi katika mserereko wa uchumi, katika limbwi la siasa za hofu, siasa za kununua watu utafikiri tupo kwenye slave trade, kufeli kwa diplomasia, kuonea watu, kudhalilisha watu na siasa za one man show

5. Membe ana sifa, vigezo na uwezo wa kuwa raisi mzuri kwa nchi yetu

Hapa tulipo tunahitaji mtu atakayeunganisha Taifa, kuponya majeraha, kurekebisha uchumi wa nchi na kuturudishia siasa za utu. Kwa kweli sioni mtu nje na ndani ya CCM mwenye uwezo huu kwa sasa isipokuwa Membe

ACT Wazalendo, tuleteeni Membe aturekebishie nchi yetu, Tunaweza kumvumilia Membe kuja Upinzani na kutuongoza kumg'oa Magufuli kuliko kuendelea na miaka mingine mitano ya aina ya uongozi wa utawala huu uliofeli wa awamu ya tano!
 
Mimi sina shida kabisa na Act wala ccm





Chadema , is the political party which power belongs to the people
 
Da mwaka huu ,naanza kuyaona Yale mungu alinena nami siku ya mwaka mpya 2020 japo nina mda sijafika kanisani ,asante mungu kwa kunikumbuka mimi nilie kiumbe dhaifu kwako na nipe afya njema niyashuhudie kwa macho yangu
 
Kifo cha nyenzi kinaenda kutoa fursa kwa membe kupata nguvu yake ndani ya chama!!

Angekuwa na advantage miezi mitano iliyopita lakini sasa hivi hata akirudi ndani ya Chama mchakato utakuwa ni mkubwa mpaka awe cleared, kisha achukue fomu ni too late.

Hapa Membe anapaswa apande kwenye jahazi la ACT safari iendelee
 
Kati ya vipindi Vyote vya kugombea Uraisi Kwa Vyama vingi vya Upinzani Tanzani ambapo wagombea Uraisi watashindwa na Chama cha CCM kupitia mgombea wake JPM alimaarufu Brudoza, Tingatinga ni Temu hii

Nahisi Vyama na wapinzani kupitia wagombea wao, haki ya mjomba historia itaandika kuwa, hakuna kipindi ambacho wapinzani walishindwa Kwa Kura nyingi na kuingia aibu kubwa ya miaka na miaka Kwa wagombea Uraisi Upinzani ni Temu hii,

Ni Bora Kwa mbaaali awepo mh Lisu, atabebwa na zile huruma za Watanzania wachache Kwa kuumia kwake, Lakini pia hoja ya MIGA ndio itakayopunguza uwingi wa Kura kwake, ila itakuwa angalau, sio hao kina Membe

Ni mara Mia angalau Kinana sio huyo
 
Mimi nafikiri bila kuifumua Tume huru ya uchaguzi tuna mlima mrefu wa kukwea...cha msingi kabisa ni kuanzisha vuguvugu la kudai Tume Huru, mataifa yatatuelewa na watanzania watatuelewa.
 
Aje Membe, Lissu, awe nani. Kwa mazingira haya tuliyonayo sasa ni ndoto ya mchana kumong'oa Magufuli. Mazingira ya leo hayathamini kura na matakwa ya raia. Kwa hiyo haiwezekani CCM ishindwe hata raia waichukie vipi. Mteua wagombea ni CCM; refa ni CCM; kamisa ni CCM; mtangazaji matokeo ni CCM; mlinda usalama ni CCM; na katiba inakataza matokeo ya rais kulalamikiwa mahakamani. Reference - uchaguzi wa serikali za mitaa. Ninatabiri yatajirudia yaleyale.
 
Mimi nafikiri bila kuifumua Tume huru ya uchaguzi tuna mlima mrefu wa kukwea...cha msingi kabisa ni kuanzisha vuguvugu la kudai Tume Huru, mataifa yatatuelewa na watanzania watatuelewa.
Mnadhani kwa jinsi hii mnavyodai mtafanikiwa?
Nawashauri mjiandae kuingia ulingoni na tume hiihii, msipoteze muda eti mnadai tume huru.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kukata tamaa is not an option, Anything can happen katika human affairs. Magufuli siyo Mungu. He can be defeated!

Wakati mwingine siku ya kufa nyani miti yote huteleza na nyani huyo mkongwe akajiona hivi hivi anakwenda na Maji.

Magufuli lastly naye anategemea watu "wamtetee", siku hao anaowaamini watamtetea wakikataa kumtetea au wakimess up basi ana nguvu gani tena za zaidi?

Ndiyo maana nasema Membe asirudi nyuma yeye aende ACT, aombe kusimama kwa tiketi ya chama hicho na apambane.

Na Kazi ya Kupambana na Magufuli kwenye jukwaa la kisiasa ni nyepesi tu, ni kuwakumbusha wananchi jinsi vyuma vilivyokaza katika wakati huu wa awamu ya tano kisha uje uone hasira kali waliyonayo wananchi dhidi ya awamu hii!
 
Membe anatosha,ni mtu wa system anaaminika haitaji vetting ya wana usalama hivyo ni rahisi sana kumkabidhi nchi. Watu wa system wenyewe wamemchoka huyo mzee wa one man show,anaamrisha watu utafikiri watoto wake wadogo,meuruga uchumi,mevuruga diplomasi
 
Siku Membe akitangaza tu kugombea uraisi kupitia chama cho chote chote ,siku ya pili TAKUKURU watamyaka.
 
Aje Membe, Lissu, awe nani. Kwa mazingira haya tuliyonayo sasa ni ndoto ya mchana kumong'oa Magufuli. Mazingira ya leo hayathamini kura na matakwa ya raia. Kwa hiyo haiwezekani CCM ishindwe hata raia waichukie vipi. Mteua wagombea ni CCM; refa ni CCM; kamisa ni CCM; mtangazaji matokeo ni CCM; mlinda usalama ni CCM; na katiba inakataza matokeo ya rais kulalamikiwa mahakamani. Reference - uchaguzi wa serikali za mitaa. Ninatabiri yatajirudia yaleyale.

Upinzani Mwaka 2020:
1. URAIS _ CCM 98.85%, NCCR 0.15, CHADEMA 0.95,
2. MAJIMBO- CCM 95% , NCCR 2%,CUF 0.65%, CHADEMA O.OO5%,
3. MADIWANI - CCM 97% , NCCR 1%, CHADEMA 1%, ACT 0.65, CUF 0.35%.

Hii itategemea . Kuna uwezekano wa nafasi za uwakilishi zikawa 100% kwa Bara kuwa CCM.

Sababu: Wapinzani wanaishi kwa kuwatukuza Wakoloni na CCM wameenda kinyume nayo na baadae kugundulika CCM ndo walikuwa sahihi kuliko mbinu za Mabeberu zilizokuwa zikiungwa Mkono na upinzani hali ambayo imeababisha kutoaminika tena na kila wanachokifanya kuonekana ni utapeli na CCM kuonekana ndiye Mkombozi pekee wa Afya na Maisha yao . Lakini Wakoloni badae wanafanya utafiti na kugundua kuwa CCM wako sahihi na wao walikuwa hawajafanya utafiti ipasavyo.

Nyingine ni udikteta wa Freeman Mbowe umesababisha Wananchi kutoamini tena kinachohubiriwa na Chadema kuhusu Demokrasia na udikteta maana tayari wamegundulika ni matapeli.

Sababu nyingine: upinzani kuvifanya vyama kama vyanzo vya Mapato ya Watu binafsi na siyo taasisi, Jambo ambalo limewakela Wananchi wengi na kusababisha kujikatia tamaa, na kuamua kuungana na Sera za JPM.
Nitaendelea ku update Mengine mengi
 
Upinzani Mwaka 2020:
1. URAIS _ CCM 98.85%, NCCR 0.15, CHADEMA 0.95,
2. MAJIMBO- CCM 95% , NCCR 2%,CUF 0.65%, CHADEMA O.OO5%,
3. MADIWANI - CCM 97% , NCCR 1%, CHADEMA 1%, ACT 0.65, CUF 0.35%.
Hii itategemea . Kuna uwezekano wa nafasi za uwakilishi zikawa 100% kwa Bara kuwa CCM.
Sababu: Wapinzani wanaishi kwa kuwatukuza Wakoloni na CCM wameenda kinyume nayo na baadae kugundulika CCM ndo walikuwa sahihi kuliko mbinu za Mabeberu zilizokuwa zikiungwa Mkono na upinzani hali ambayo imeababisha kutoaminika tena na kila wanachokifanya kuonekana ni utapeli na CCM kuonekana ndiye Mkombozi pekee wa Afya na Maisha yao . Lakini Wakoloni badae wanafanya utafiti na kugundua kuwa CCM wako sahihi na wao walikuwa hawajafanya utafiti ipasavyo.
Nyingine ni udikteta wa Freeman Mbowe umesababisha Wananchi kutoamini tena kinachohubiriwa na Chadema kuhusu Demokrasia na udikteta maana tayari wamegundulika ni matapeli.
Sababu nyingine: upinzani kuvifanya vyama kama vyanzo vya Mapato ya Watu binafsi na siyo taasisi, Jambo ambalo limewakela Wananchi wengi na kusababisha kujikatia tamaa, na kuamua kuungana na Sera za JPM.
Nitaendelea ku update Mengine mengi

Siyo rahisi kihivyo
Kumbuka law of unintended consequences
 
Back
Top Bottom