DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha ACT Wazalendo Luhaga Mpina, amesema kuwa uteuzi wake kuwa mgombea urais kupitia chama hicho ni mwanzo rasmi wa safari ya kukiondoa Chama Cha Mapinduzi (CCM) madarakani, akisisitiza kuwa Watanzania wanataka katiba mpya na haki ya kweli ya kuamua hatima ya nchi yao.
Akizungumza mbele ya wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum wa ACT Wazalendo uliofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam muda mchache kabla ya wajumbe hao kumchagua kuwa mgombea wa chama hicho, Mpina alisema: “Mkimpata Luhaga Mpina akawa mgombea wa kuipeperusha hii bendera ya ACT Wazalendo kazi imekwisha, safari ya kwenda kuing’oa CCM itakuwa imeiva leo na leo hii chama hiki kinaenda kuandika historia ya kuwa chama cha pili kuongoza dola nchini Tanzania.”
Mpina alilaani vikali kile alichokiita “danadana zisizo na msingi” kuhusu mchakato wa katiba mpya, akisema serikali iliyopo madarakani inawanyima Watanzania haki yao ya msingi.
Akizungumza mbele ya wajumbe wa Mkutano Mkuu Maalum wa ACT Wazalendo uliofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam muda mchache kabla ya wajumbe hao kumchagua kuwa mgombea wa chama hicho, Mpina alisema: “Mkimpata Luhaga Mpina akawa mgombea wa kuipeperusha hii bendera ya ACT Wazalendo kazi imekwisha, safari ya kwenda kuing’oa CCM itakuwa imeiva leo na leo hii chama hiki kinaenda kuandika historia ya kuwa chama cha pili kuongoza dola nchini Tanzania.”
Mpina alilaani vikali kile alichokiita “danadana zisizo na msingi” kuhusu mchakato wa katiba mpya, akisema serikali iliyopo madarakani inawanyima Watanzania haki yao ya msingi.