ACT-Tanzania yang'ara vijijini zaidi

ACT-Tanzania yang'ara vijijini zaidi

Nyakarungu

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2011
Posts
472
Reaction score
377
ACT-Tanzania Vijijini na thabiti.

Chama cha Tanu kilifanikiwa haraka kwa sababu kilijikita vijijini zaidi kuwaelimisha wananchi kukijua na kulitambua taifa lao, nimeanza ziara rasmi maeneo tengevu ya nchi yetu kueneza chama chetu cha ACT-Tanzania,
Nimefarijika sana kuona chama cha ACT-Tanzania kimemea na kuanza kuchipua maeneo tengevu (remote areas) tunaungwa sana mkono maeneo ya kando kuliko vyama vyote ikiwemo chama tawala,
Tuna wagombea wengi zaidi maeneo ya kando kuliko mijini,
Yapo maeneo tunawagombea wanaopambana na ccm wala hakuna wagombea wa vyama vingine.
Na kwa sababu chama chetu kimeanza na misingi sio malengo na madhumuni kama vingine ndio sababu ya sisi kukubalika haraka na kueleweka vyema.

Idara ya ITIKADI, UENEZI NA MAHUSIANO YA JAMII inawapongeza wanachama wote wa ACT - Tanzania na watanzania wote kwa kazi nzuri ya kueneza chama.
Idara ya uenezi inawaasa kuhakikisha juhudi hizi zinazaa matunda, nahimiza tujitokeze kupiga kura na kuzilinda.
Nyakarungu Grayson
Katibu Itikadi,Uenezi na mahusiano ya jamii.
+255 755 023 503




 
Pambaneni kisayansi ila mkitaka kudumaa ni kujenga ushoga na chama tawala .Kama hamuamini waulize hao kina mzirai tlp nk maana kuna makundi mawili moja ni chama tawala la pili vyama pinzania hakuna (tawala pinzani)unategemea tawala wakusaidieje? nilisikitika kiongozi act kuwa jukwaa la chama tawala you erodd your image kama ni kweli
 
Mkuu, Prof. Mkumbo unamtimua lini? Au "gamba"limegomea kiunoni?

Au zilikuwa ni mbwembwe za kutishia nyau ili ujulikane kuwa wewe ndie muhasisi wa ACT? Unacheza na ZE PROF. WEWE!!
 
Wanapambana na CHADEMA hawa mashosti wa ccm
 
Umeshiba mchembe ukaja kuhara JF. Wasaliti mtalubalikaje?
 
Hebu taja hayo maeneo uliyozuru (maeneo tengevu!!!!!!), huu uandishi wa kikanjanja hauna maana, maeneo haya yana majina.
 
Haya shost wa magamba endelea na maeneo tengevu!!
 
Wanapambana na CHADEMA hawa mashosti wa ccm

ACT inapambana na cdm+ccm
CDM inapambana na ccm-bara
CUF inapambana na ccm-znz

hakuna haja ya kutukana wewe na wenzako boresheni sera zenu kwa wapiga kura.
Ivi wewe unadhani CDM ndio inahati miliki ya kuwa chama cha upinzani? Tumia akili zako acha mihemko na jaziba.

Act inaonekana inawatesa kwa strategy zao
 
vijiji vya wapi?

Vijiji vya FB,Twitter,JF,MF na Michuzi vyote vipo kata ya Internet..

BTW, Hivi ZZK kwenye uchaguzi huu wa serikali za mitaa anapiga kampeni kwa chama kipi?jimbo lipi?au amepotezea na escrow?
 
Mkuu Nyakarungu, Pole na majukumu ya kazi ngumu ya kueneza chama!

Baada ya salamu ninayo maswali mawili mkuu naomba unijibu kiufasaha!

1. kwann hujagraduate mwaka huu mzumbe university, tatizo nn?

2. Wiki iliyopita kanda ya ziwa mratibu wenu wa kanda ya ziwa ameonekana akiambatana mwigulu ktk mikutano akihutubia kwa kuisifu ccm na mwigulu pia, Je mlimtuma au utashi wake, Je alichokifanya ni sahihi? Hatua gani mmechukua?(Muumini wa dini yeyote kumsafia shetani ni swala la kushtua sana)

Nyie ni tawi dogo la ccm? au nyie jumuiya mojawapo ya ccm kama ilivyo uvccm, uwt, n.k
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom