ACT Wazalendo
JF-Expert Member
- May 5, 2014
- 643
- 1,603
Ndugu watanzania wote, tunawasalimu kwa salamu inayoashiria mabadiliko na uwazi.
Katika kusimamia dhana ya uwazi na kuhakikisha kwamba kila anayependa kupata taarifa mbali mbali kuhusu chama cha ACT-Tanzania, anazipata kikamilifu, kwa haraka, kwa ufanisi na bila usumbufu mkubwa, tunawaomba watanzania wote wanaopenda kupata taarifa mbali mbali za chama cha ACT- Tanzania, watutumie barua pepe zao au namba zao za simu.
ACT-Tanzania tunatumia na tutaendelea kutumia mbinu mbali mbali ili kujitahidi kuwafikia watanzania wengi iwezekanavyo (ikiwezekana watu wazima wote na wenye akili timamu), kwa haraka, kwa ufanisi, bila usumbufu mkubwa na kwa kujaribu kutumia njia ambazo ni za gharama nafuu zaidi.
Miongoni mwa mbinu ambazo baadhi tumeanza kuzitumia na tutakuwa tunazitumia kuwafikia watanzania ukiacha mikutano ya hadhara, ni pamoja na hii ya kupitia simu zenu, barua pepe zenu, tovuti ambayo tutaifungua karibuni, vitabu, vipeperushi (brochures), mitandao ya kijamii na kadhalika.Tutakuwa tukiboresha mifumo yetu ya mawasiliano kila mara kulingana na uwezo wetu ili watanzania waweze kuyafaidi matunda ya chama chao wakati wote.
NB. Kwa sasa kuna vijitabu vidogo (Brochures) tunagawa vinavyoeleza mambo muhimu yanayohusiana na ACT-Tanzania kwa muhtasari.Kama mtu anahitaji "soft copy", atatutumia e-mail yake na kama anataka "Hard Copy" atasubiria kidogo hadi tutakapoingia mtaani kwake.
ACT-Tanzania.................Taifa kwanza leo na kesho!,
Mabadiliko na Uwazi.........Chukua Hatua!.
Tuwasiliane kwa acttanzania@yahoo.com au acttanzania@gmail.com.
Katika kusimamia dhana ya uwazi na kuhakikisha kwamba kila anayependa kupata taarifa mbali mbali kuhusu chama cha ACT-Tanzania, anazipata kikamilifu, kwa haraka, kwa ufanisi na bila usumbufu mkubwa, tunawaomba watanzania wote wanaopenda kupata taarifa mbali mbali za chama cha ACT- Tanzania, watutumie barua pepe zao au namba zao za simu.
ACT-Tanzania tunatumia na tutaendelea kutumia mbinu mbali mbali ili kujitahidi kuwafikia watanzania wengi iwezekanavyo (ikiwezekana watu wazima wote na wenye akili timamu), kwa haraka, kwa ufanisi, bila usumbufu mkubwa na kwa kujaribu kutumia njia ambazo ni za gharama nafuu zaidi.
Miongoni mwa mbinu ambazo baadhi tumeanza kuzitumia na tutakuwa tunazitumia kuwafikia watanzania ukiacha mikutano ya hadhara, ni pamoja na hii ya kupitia simu zenu, barua pepe zenu, tovuti ambayo tutaifungua karibuni, vitabu, vipeperushi (brochures), mitandao ya kijamii na kadhalika.Tutakuwa tukiboresha mifumo yetu ya mawasiliano kila mara kulingana na uwezo wetu ili watanzania waweze kuyafaidi matunda ya chama chao wakati wote.
NB. Kwa sasa kuna vijitabu vidogo (Brochures) tunagawa vinavyoeleza mambo muhimu yanayohusiana na ACT-Tanzania kwa muhtasari.Kama mtu anahitaji "soft copy", atatutumia e-mail yake na kama anataka "Hard Copy" atasubiria kidogo hadi tutakapoingia mtaani kwake.
ACT-Tanzania.................Taifa kwanza leo na kesho!,
Mabadiliko na Uwazi.........Chukua Hatua!.
Tuwasiliane kwa acttanzania@yahoo.com au acttanzania@gmail.com.