ACT, CHADEMA wajitosa ugomvi wa CUF

ACT, CHADEMA wajitosa ugomvi wa CUF

Nadhani kuna kitu ambacho kimejificha kidogo na ndo maana wengi hatuingii kukiona. UKAWA ulileta hamasa zaidi kwa wananchi kwa sababu ya ile dhana ya umoja. Kuna usemi usemao; United we stand. Kwa maneno mengine ni kwamba, tulikuwa na kiu ya kuona ccm imeanguka, na ukweli ni kwamba, ccm nao walijua/wanajua, upinzani wakiungana, hakika watawaangusha. Ndo maana huwa wanajitahidi kwa kila mbinu kuitikisa upinzani wasiweze kusimama katika umoja.
Tangu UKAWA ianze kupinga katiba pendekezwa, mambo yalianza kuiendea mrama ccm. Hivyo, kitendo cha kumwingiza tena Lowasa kwao UKAWA ikatia chaji zaidi kwa wananchi kuanza kuamini kuwa, sasa ccm kwa kheri. Mipango ya kuwatikisa CUF na CDM ilivyo wiva hata Profesa na Dr wakaamua kubwaga manyanga tena katikati ya vita iliuua ule mori wa wananchi.
That is why, tunasema, Profesa aendelee kukaa kule kule alikoenda awaache wana CUF wajikongoje wenyewe.
Hata angelipewa ruksa kuingia ofisini leo, hawezi tena ongoza kwa nguvu yake ya kale. Aliiangusha CUF kwa kukimbia vitani. Full Stop.
Kitila is another pathetic. Afanye vyake huko ACT aongeze wabunge, aache kuyatangaza mapungufu ya upinzani. Unapoeleza mapungufu tuuu unauua upinzani.
Tungoje hata kukitokea chaguzi ndogo ACT ipite kwa sera zake. Lakini kwa mtindo huu wa kupambana na upinzani, mtabaki na huyo huyo mmoja. Mkuu kishawaambieni, hatokula pamoja na mpinzani yeyote. Kumbukeni hilo, acheni kutafuta kuvurugana, mvurugeni mbaya wenu ccm si vinginevyo.


Kwani Kitila Mpinzani?

Mtumishi wa umma pekee aliye katika active Opposition politics na bado ni mtumishi wa Umma

Tumieni vichwa kuelewa
 
Hawa wasomi mnaowaamini ndowanao liangamiza taifa hili kama wakina kitilya na lipumba nawengineo wasomi wabongo siowakutegemea
Mbona umemuacha Tundu na genge lake au hao ni wasomi uchwara😀?
 
watajuana huko huko tukutane kwenye sanduku la kura 2020 kama kawaida mpinzani alie na nguvu nampigia kura yangu hata wapinzani wafarakane vipi bado wataambulia kura yangu.
 
Watu wavivu kufikiri na kufanya utafiti wanafikiri ushindi Wa ubunge na madiwani kutoka ukawa ulisababishwa na ujio Wa lowassa na kundi lake !! this pathetic!! ni asilimia ndogo sana!! ushibdi wao au idadi kuongezeka ilitokana na kuchukiwa kwa CCM na wananchi waliyokuwa wamechoka ufisadi ndani ya chama tawala!!na ushindi waliyopata siyo wakujivunia hata kidogo maana ni small percentage ya wabunge compared to the powerful party CCM iliyoweza kushinda vyama vyote 4!Ni aibu ya mwaka Lissu kujisifia ushindi kupitia ukawa!!Nafiri hesabu alifeli mbaya sana!!

Kwa kweli escrow ilikuwa imeshaawachosha wananchi,hata ukiangalia serikali za mitaa walifanya vizuri sana hata bila yule jamaa wanamtukuza
 
Kiukweli mi naona watu walioenda shule ndo wanauwezo wakuwasiniliza na kiwaelewa hawa ma maprofessa lakin nyie oya oya mtaishia kusema sibui mrof uchwara. Kitila amejibu vizur saana bwana tundu yale mashudu alioongea.. SIASA NI UNAFKI WA HALI YA JUU CHADEMA iliokua inasema CUF ni CCM B leo ndo wanawaona kama jiwe kuu la pembeni.. pumbavu
 
Sasa mbaya zaidi jamani huku jimboni kwa lisu hakuna hata kisima kimoja cha maji, nadhani lisu atambue yy ni mbunge anatakiwa atetee zaidi maendeleo jimboni kwake badala ya kulumbana na akina kitila wao sio wabunge hawana cha kupoteza, ila yeye ana cha kupoteza(ubunge). Kama anataka awe hata katibu mwenezi wa Chadema na sio mbunge
 
*MAJIBU YA PROF.KITILA KWA LISSU*



Tundu Lissu: baada nilishalala lakini maandishi hayaozi. Nimekusoma.
Those are simply usual innuendos from a usual and expected you. You did not address any of my major arguments. As usual, ukaishia kutukana na kutoa hogwash allegations kwamba tulipewa hela na CCM ili tugawe kura za ukawa. Sounds familiar evil-intentioned allegation. Unachosahau ni kwamba nyie haohao mliimba miezi mingi kwamba tulipewa hela na Lowassa ili tuanzishe Chama chake na kwamba angegombea kwenye Chama hicho. Alipowafuata mkanywea na kumeza fedheha. Wewe ni mwanasiasa uliyebarikiwa kutokuwa na mshipa wa aibu. Unabahati pia upo katika Jamii ambayo political morals ni kama hazipo. Ndiyo maana akina Chenge hadi leo wanaendelea kutamba.

Kuhusu uimara au udhaifu wa CUF. Utafanikiwa kuwadanganya wana CUF wajinga tu kwamba kura na wabunge waliopata ni kazi ya miezi miwili baada ya Lipumba kuondoka na malaika Lowassa kuingia ukawa. CUF werevu hutawapata na wapo wengi na Ndiyo maana wenzako wanafanyia vikao Vuga. CUF werevu wanajua kwamba walifanya kazi miaka mitano kuvuna walichokivuna. CUF werevu wanajua mlituma watu wenu wachukue fomu hata Katika majimbo mliyokubaliana kuachiana. CUF werevu wanajua kwamba mlimwambia Anatropia kamwe asitoe jina lake huku Segerea na ndiyo maana mkamzawadia ubunge wa Viti maalumu. Endeleeni kuwadanganya CUF wajinga lakini CUF werevu wapo tele!
Sina mpango wa kuwa Profesa kama hali ndo hii, degree yangu inatosha sana zaidi ya hawa Maprofesa.
 
Kama ushindi wa CUF ulitokana na kuchukiwa kwa Ccm kwa nini na ACT nao wasipate hivyo viti kadhaa ukizingatia nao walisimamisha mgombea kila jumbo?
Kitila kesha julikana kuwa analinda kibarua chake serikalini
Zitto alituambia kuwa ndio chama cha pili baada ya chama chetu tawala ccm, kusimamisha wagombea ubunge katika majimbo 219. Lakini cha ajabu walipata mbunge mmoja tu. Sasa kwanini kama ccm ilichukiwa wao wasingepata idadi kubwa ya wabunge?
 
Nadhani kuna kitu ambacho kimejificha kidogo na ndo maana wengi hatuingii kukiona. UKAWA ulileta hamasa zaidi kwa wananchi kwa sababu ya ile dhana ya umoja. Kuna usemi usemao; United we stand. Kwa maneno mengine ni kwamba, tulikuwa na kiu ya kuona ccm imeanguka, na ukweli ni kwamba, ccm nao walijua/wanajua, upinzani wakiungana, hakika watawaangusha. Ndo maana huwa wanajitahidi kwa kila mbinu kuitikisa upinzani wasiweze kusimama katika umoja.
Tangu UKAWA ianze kupinga katiba pendekezwa, mambo yalianza kuiendea mrama ccm. Hivyo, kitendo cha kumwingiza tena Lowasa kwao UKAWA ikatia chaji zaidi kwa wananchi kuanza kuamini kuwa, sasa ccm kwa kheri. Mipango ya kuwatikisa CUF na CDM ilivyo wiva hata Profesa na Dr wakaamua kubwaga manyanga tena katikati ya vita iliuua ule mori wa wananchi.
That is why, tunasema, Profesa aendelee kukaa kule kule alikoenda awaache wana CUF wajikongoje wenyewe.
Hata angelipewa ruksa kuingia ofisini leo, hawezi tena ongoza kwa nguvu yake ya kale. Aliiangusha CUF kwa kukimbia vitani. Full Stop.
Kitila is another pathetic. Afanye vyake huko ACT aongeze wabunge, aache kuyatangaza mapungufu ya upinzani. Unapoeleza mapungufu tuuu unauua upinzani.
Tungoje hata kukitokea chaguzi ndogo ACT ipite kwa sera zake. Lakini kwa mtindo huu wa kupambana na upinzani, mtabaki na huyo huyo mmoja. Mkuu kishawaambieni, hatokula pamoja na mpinzani yeyote. Kumbukeni hilo, acheni kutafuta kuvurugana, mvurugeni mbaya wenu ccm si vinginevyo.
Naiona act kama chama kitakachokuwa kigoma na Dar tu pekee. Huku kwingine wafuasi kama wapo washachoka. Na kazi ya mkuu wa nchi hii nadhani wataambulia tena mbunge mmoja huko mbeleni. Na ikifikia hapo basi chama kitakuwa kama kile cha Cheyo. One man show.
 
Kitila atabaki na mbunge wake mmoja maana no siasa no mikutano ya siasa cjui cjama lake litakuwa he huku mitaani. Alafu anamtetea prof muhanga mwenzie
 
Back
Top Bottom