Freeland
JF-Expert Member
- Jan 24, 2012
- 14,481
- 10,233
Nadhani kuna kitu ambacho kimejificha kidogo na ndo maana wengi hatuingii kukiona. UKAWA ulileta hamasa zaidi kwa wananchi kwa sababu ya ile dhana ya umoja. Kuna usemi usemao; United we stand. Kwa maneno mengine ni kwamba, tulikuwa na kiu ya kuona ccm imeanguka, na ukweli ni kwamba, ccm nao walijua/wanajua, upinzani wakiungana, hakika watawaangusha. Ndo maana huwa wanajitahidi kwa kila mbinu kuitikisa upinzani wasiweze kusimama katika umoja.
Tangu UKAWA ianze kupinga katiba pendekezwa, mambo yalianza kuiendea mrama ccm. Hivyo, kitendo cha kumwingiza tena Lowasa kwao UKAWA ikatia chaji zaidi kwa wananchi kuanza kuamini kuwa, sasa ccm kwa kheri. Mipango ya kuwatikisa CUF na CDM ilivyo wiva hata Profesa na Dr wakaamua kubwaga manyanga tena katikati ya vita iliuua ule mori wa wananchi.
That is why, tunasema, Profesa aendelee kukaa kule kule alikoenda awaache wana CUF wajikongoje wenyewe.
Hata angelipewa ruksa kuingia ofisini leo, hawezi tena ongoza kwa nguvu yake ya kale. Aliiangusha CUF kwa kukimbia vitani. Full Stop.
Kitila is another pathetic. Afanye vyake huko ACT aongeze wabunge, aache kuyatangaza mapungufu ya upinzani. Unapoeleza mapungufu tuuu unauua upinzani.
Tungoje hata kukitokea chaguzi ndogo ACT ipite kwa sera zake. Lakini kwa mtindo huu wa kupambana na upinzani, mtabaki na huyo huyo mmoja. Mkuu kishawaambieni, hatokula pamoja na mpinzani yeyote. Kumbukeni hilo, acheni kutafuta kuvurugana, mvurugeni mbaya wenu ccm si vinginevyo.
Kwani Kitila Mpinzani?
Mtumishi wa umma pekee aliye katika active Opposition politics na bado ni mtumishi wa Umma
Tumieni vichwa kuelewa