DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
TAARIFA KWA UMMA
TUME YA AFRIKA YAKUBALI AZIMIO KUHUSU HALI YA HAKI ZA BINADAMU NCHINI TANZANIA
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinakaribisha na kupongeza kwa dhati kupitishwa kwa Azimio ACHPR/Res.640 (LXXXIV) 2025 na Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (ACHPR), wakati wa Kikao chake cha 84 cha Kawaida kilichofanyika kwa njia ya mtandao kuanzia tarehe 21 hadi 30 Julai 2025.
Azimio hili, lililopitishwa katika ngazi ya bara, linaakisi wasiwasi mkubwa wa chombo kikuu cha haki za binadamu barani Afrika kuhusu kuzorota kwa hali ya haki za binadamu nchini Tanzania, hususan kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Katika uamuzi wake, ACHPR imesisitiza wajibu wa kisheria wa Tanzania chini ya Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu pamoja na mikataba mingine ya kimataifa ya haki za binadamu iliyoidhinishwa na nchi, na kueleza wasiwasi mkubwa kuhusu:
1. Matumizi ya nguvu kupita kiasi kuvunja mikutano na maandamano ya amani, ikiwemo tukio la tarehe 9 Aprili 2025 kufuatia kukamatwa kwa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Mh. Tundu Lissu, na tukio la tarehe 24 Aprili 2025 katika Mahakama ya Kisutu ambapo viongozi na wafuasi wa upinzani walizuiwa kuhudhuria kesi hiyo.
2. Tuhuma za kupotezwa kwa watu kwa nguvu (enforced disappearances), mateso na kukamatwa kiholela, ambazo zimelaaniwa kimataifa na wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa na Bunge la Ulaya.
3. Kufukuzwa na kukamatwa kwa viongozi wa kigeni na wanaharakati wa haki za binadamu, wakiwemo aliyewahi kuwa Waziri wa Sheria na aliyewahi kuwa Jaji Mkuu wa Kenya pamoja na timu yake (tarehe 18 Mei 2025), na siku iliyofuata wanaharakati kutoka Uganda na Kenya, bila kupitia mchakato wa mahakama.
4. Vikwazo dhidi ya uhuru wa vyombo vya habari na upatikanaji wa taarifa, ikiwemo kufungiwa kwa mtandao wa X (zamani Twitter) tarehe 4 Juni 2025, kuwekwa kwa vikwazo kwenye YouTube, na kutofikika kwa majukwaa ya Clubhouse na Telegram bila kutumia VPN.
---
WITO WA ACHPR KWA SERIKALI YA TANZANIA
Kupitia Azimio hili, ACHPR imeitaka Serikali ya Tanzania:
1. Kuheshimu na kutekeleza viwango vya haki za binadamu katika mchakato wa uchaguzi.
2. Kufanya uchunguzi na kukomesha vitendo vya kupotezwa kwa watu kwa nguvu, mateso, kukamatwa kiholela, na kukandamiza mikutano ya amani.
3. Kuhakikisha uhuru wa kujieleza na upatikanaji kamili wa mtandao bila vizuizi.
4. Kuhakikisha uchaguzi huru, wa haki, wa amani na wenye uwazi bila vitisho na vurugu.
5. Kuwalinda watetezi wa haki za binadamu na kuwawajibisha wahusika wa ukiukaji.
6. Kufanya uchunguzi na kutoa fidia kwa waathirika wa ukiukaji, wakiwemo wanaharakati wa kigeni walioteswa na kufukuzwa Mei 2025.
7. Kutekeleza maamuzi ya lazima ya Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu, ikiwemo kuruhusu wagombea binafsi na kurejesha mamlaka ya mahakama za ndani kusikiliza mashauri ya uchaguzi.
---
MSIMAMO WA CHADEMA
CHADEMA inaona Azimio hili kama uthibitisho wa kihistoria wa hoja ambazo tumekuwa tukizitolea wito kwa muda mrefu kuhusu kudorora kwa haki za binadamu, nafasi ya kidemokrasia, na utawala wa sheria nchini Tanzania.
Azimio hili linatuma ujumbe wazi na usiopingika kwa Serikali: dunia inatazama, na mfumo wa haki za binadamu wa Afrika hautakaa kimya mbele ya ukandamizaji.
Tunazihimiza mamlaka za Tanzania kusikiliza na kutekeleza mara moja wito wa ACHPR, na kuchukua hatua za haraka kufanya mabadiliko ya sheria na kanuni za uchaguzi ili kuhakikisha mazingira bora ya uchaguzi wa kuaminika, wa amani, na wa kidemokrasia mwezi Oktoba 2025.
---
Imetolewa leo, Ijumaa, 08 Agosti 2025
................
Brenda Rupia
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi
TUME YA AFRIKA YAKUBALI AZIMIO KUHUSU HALI YA HAKI ZA BINADAMU NCHINI TANZANIA
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kinakaribisha na kupongeza kwa dhati kupitishwa kwa Azimio ACHPR/Res.640 (LXXXIV) 2025 na Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu (ACHPR), wakati wa Kikao chake cha 84 cha Kawaida kilichofanyika kwa njia ya mtandao kuanzia tarehe 21 hadi 30 Julai 2025.
Azimio hili, lililopitishwa katika ngazi ya bara, linaakisi wasiwasi mkubwa wa chombo kikuu cha haki za binadamu barani Afrika kuhusu kuzorota kwa hali ya haki za binadamu nchini Tanzania, hususan kuelekea Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025.
Katika uamuzi wake, ACHPR imesisitiza wajibu wa kisheria wa Tanzania chini ya Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu pamoja na mikataba mingine ya kimataifa ya haki za binadamu iliyoidhinishwa na nchi, na kueleza wasiwasi mkubwa kuhusu:
1. Matumizi ya nguvu kupita kiasi kuvunja mikutano na maandamano ya amani, ikiwemo tukio la tarehe 9 Aprili 2025 kufuatia kukamatwa kwa Mwenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, Mh. Tundu Lissu, na tukio la tarehe 24 Aprili 2025 katika Mahakama ya Kisutu ambapo viongozi na wafuasi wa upinzani walizuiwa kuhudhuria kesi hiyo.
2. Tuhuma za kupotezwa kwa watu kwa nguvu (enforced disappearances), mateso na kukamatwa kiholela, ambazo zimelaaniwa kimataifa na wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa na Bunge la Ulaya.
3. Kufukuzwa na kukamatwa kwa viongozi wa kigeni na wanaharakati wa haki za binadamu, wakiwemo aliyewahi kuwa Waziri wa Sheria na aliyewahi kuwa Jaji Mkuu wa Kenya pamoja na timu yake (tarehe 18 Mei 2025), na siku iliyofuata wanaharakati kutoka Uganda na Kenya, bila kupitia mchakato wa mahakama.
4. Vikwazo dhidi ya uhuru wa vyombo vya habari na upatikanaji wa taarifa, ikiwemo kufungiwa kwa mtandao wa X (zamani Twitter) tarehe 4 Juni 2025, kuwekwa kwa vikwazo kwenye YouTube, na kutofikika kwa majukwaa ya Clubhouse na Telegram bila kutumia VPN.
---
WITO WA ACHPR KWA SERIKALI YA TANZANIA
Kupitia Azimio hili, ACHPR imeitaka Serikali ya Tanzania:
1. Kuheshimu na kutekeleza viwango vya haki za binadamu katika mchakato wa uchaguzi.
2. Kufanya uchunguzi na kukomesha vitendo vya kupotezwa kwa watu kwa nguvu, mateso, kukamatwa kiholela, na kukandamiza mikutano ya amani.
3. Kuhakikisha uhuru wa kujieleza na upatikanaji kamili wa mtandao bila vizuizi.
4. Kuhakikisha uchaguzi huru, wa haki, wa amani na wenye uwazi bila vitisho na vurugu.
5. Kuwalinda watetezi wa haki za binadamu na kuwawajibisha wahusika wa ukiukaji.
6. Kufanya uchunguzi na kutoa fidia kwa waathirika wa ukiukaji, wakiwemo wanaharakati wa kigeni walioteswa na kufukuzwa Mei 2025.
7. Kutekeleza maamuzi ya lazima ya Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu, ikiwemo kuruhusu wagombea binafsi na kurejesha mamlaka ya mahakama za ndani kusikiliza mashauri ya uchaguzi.
---
MSIMAMO WA CHADEMA
CHADEMA inaona Azimio hili kama uthibitisho wa kihistoria wa hoja ambazo tumekuwa tukizitolea wito kwa muda mrefu kuhusu kudorora kwa haki za binadamu, nafasi ya kidemokrasia, na utawala wa sheria nchini Tanzania.
Azimio hili linatuma ujumbe wazi na usiopingika kwa Serikali: dunia inatazama, na mfumo wa haki za binadamu wa Afrika hautakaa kimya mbele ya ukandamizaji.
Tunazihimiza mamlaka za Tanzania kusikiliza na kutekeleza mara moja wito wa ACHPR, na kuchukua hatua za haraka kufanya mabadiliko ya sheria na kanuni za uchaguzi ili kuhakikisha mazingira bora ya uchaguzi wa kuaminika, wa amani, na wa kidemokrasia mwezi Oktoba 2025.
---
Imetolewa leo, Ijumaa, 08 Agosti 2025
................
Brenda Rupia
Mkurugenzi wa Mawasiliano na Uenezi