Acheni utani, maisha ni magumu sana

Acheni utani, maisha ni magumu sana

Pain killer

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2017
Posts
14,365
Reaction score
21,743
Habari wakuu,

Kila nikiangalia pande zote za dunia naona kabisa kama kijana ndoto zote nilizokuwa naota enzi niko shuleni na chuoni zitabaki kuwa ndoto tu.

Sijajua wengine wanawezaje kupataje pesa za kujenga, kulisha familia, na kuendesha gali, hili swala nikiliangalia naona kama ndoto kabisa.

Tunapambana huku nakule ila kupata pesa ni ngumu mno asikwambie mtu, labda kwa vile tumezungukwa na duara la umasikin kwan unapambana weeee ukiangalia nyuma mjomba, shangazi, Mzee, kaka, Dada yaani ukoo wote ni hoi hai, mpaka unaona kabisa nurke's theory of poverty ipo real yaan "if you born poor you will be poor and poor forever"

Kama umezaliwa masikin kujitoa kwenye hill duara, lazima nguvu ya ziada itumike (ikiwezekana nguvu za Giza kabisa ) kwa hali ya kawaida you can't.

Duara la umasikin linanguvu sana, usiombe kuzaliwa humoo.
 
Kazia hapo hapo mkuu

Sasa bora nini? Kuacha kupambana au kuendelea?

Ukiendelea una options 3, kupata, kukosa au kati.

Ukiacha huna options zaidi ya umaskini.
 
Hiv bado kuna watu wenye mawazo ya hiv!!!? Yaan kuna watu wanafanya kazi saa 20/7 lakn bado maisha wanayoyaishi ni kusema tu bora uzima!
Maisha bhana!.Kuna jamaa muuza mkaa.kauza miaka 16,lakini Bado Yuko nyumba ya kupanga na maisha Bado ni magumu.ukifikiri Sana waweza kufuru.
 
Ndoto zako ukiwa mwanafunzi ni zipi mkuu au ulikuwa unasema ukiwa mkubwa utasaidia maskini ? Ukitazama kulia na kushoto unajikuta wewe ndio maskini wa kutupwa.

Anyway bado kijana mdogo una nguvu ya kupambana na kutimiza baadhi ya ndoto chache kama sio zote. Kufika level ya kutimiza ndoto zako ni vita sio mchezo mchezo mkuu..inahitaji uwe na moyo mkubwa wa kupambana, kuvumilia, kutokukata tamaa na shauku ya kufikia lengo.
 
Endelea kupambana mkuu, Wala usijilinganishe na raia wengine sababu huwezi jua wamepitia wapi kupata nyumba na magari- kuwa mpole subiri wakati wako na bidii ya kazi.
 
Labda mambo yatabadilika, wacha tuone
 
Wengi wa waliofanikiwa walishawahi kupitia hiyo stage ya mawazo unayoyawaza.

Trust me ukiona umefikia hatua ya kukaa chini na kuwaza hivyo basi jua the breakthrough is on the door.

So just fasten your seat belt and look at the world straight in the eyes

I mean, don't give up
 
Wewe ndo wakuokoa familia mzee wangu! Nakuelewa lakini dont give up mzee. Sio tu usali jichanganye kwenye mishe itakayokuja mbele yako piga ila iwe halali make money ata kwa mwaka mmoja then fungua kabiashara unachokaamini anza mdogo mdogo usiogope kuchekwa kwasababu una degree jamaa.

Kutoka kimaisha sio mchezo nakwambia haya cuz mimi ma wewe story inafanana kuna kipindi miaka ya 2012 ndo naanza life aisee nilikuwa najifungia geto nalia sana nakumlaumu Mungu kwanini mimi.

Lakini now nimesahau izo mashida mkuu na namiliki kampuni sasa na maisha yapo imara sana. Usiogope kujifunza ambavyo huvijui kaa na waliofanikiwa wawe ndo marafiki zako jitume uku ukiangalia wenzio walifanyaje utatoboa. Nikuombe ukiweza usilalamike tena jikaze kiume piga kazi jipange kuwa na mikakati mizuri utafanikiwa mkuu.

Mimi sikusoma kama wewe lakini now nina watumishi wasomi kama wewe. Hold on BE strong no matter what you're goin through. You know its gon be okay today!!! Even when the earth quakes.
 
Back
Top Bottom