Acheni serikali ishugulike na dk Mwaka.!

Acheni serikali ishugulike na dk Mwaka.!

Na sangoma nao wapigwe ban au kwa sababu hawana kipato ndio maana hamna shida nao?
 
Hivi ni kweli kwa akili zako zote maji marefu na Dr Mwaka wanafanana

Maji marefu yeye hutibu Kwa nguvu za Giza lakini dr mwaka yy hutibu Kwa mbinu za kijanja janja hivyo tofauti Yao ni ndogo sana.
 
halafu na yule kubwa jinga anamtetea dk mwaka bila hata chembe ya aibu

Le mutuz yeye kazi yake ni kujipendekeza Kwa watu kuchukua pesa zao ili awatetee hata Kama ni jambo la Hatari .
 
Sio siri nashangaa kinachotokea, hawa jamaa sijui wanatibuje ila watu wanajaa sana. Mi nashauri wapigwe ban tu
 
Mbona wengi nchini bafo wanaenda kutibiwa kwa waganga wa jadi na hao waliosoma udaktari wapo.

Muache watu waamue wanataka tiba gani ni miili yao.

Naona unawabeep Membe , January na mwigulu kwani hao ndiyo vinara wa kamati za Ufundi wanamiliki kamati za Ufundi hadi America kusini huko misitu ya Amazon , Asia na Afrika magharibi huko Gambia , sasa waganga wa kienyeji wapo busy na wabunge kibao wakiwania zile wizara zilizosalia , Membe anaamini atapewa Ubunge Kisha kupewa wizara yenye Ulaji mwingi ili aweze kurejesha gharama zake baada ya kutumia pesa nyingi toka kwenye Yale Mabilioni ya marehemu Gadafi.
 
Bado Wengine Wengi Nchi Hii Wanaofanana Na Mwaka. Kila Siku Kwenye TVs Matangazo Ya Kitapeli

Hao wengine wapo tena wana bei kubwa sana lakini watakuwa wanalindwa sana kutokana ni wao wamemchongea Dr mwaka apotezwe wao wafanye biashara .
 
Watu type za akina Mwaka wadhibitiwe maana sheria zipo. Ila tiba mbadala ipewe uzito unaostahili. Mitishamba mingi ni mizuri tu

Umenena, kama miti shamba itakwenda kwa tafiti za kisayansi hatutakuwa na shida, ndio maana pale chuo kikuu kuna kituo au taasisi ya Tiba za asili(ITM-MUHAS) na vilevile taasisi ya uchunguzi wa magonjwa ya binadamu (NIMR) INA IDARA YA TIBA ZA ASILI ILIYOKO MABIBO, sasa hawa waganga wakitaka dawa zao zitambuliwe zipite kwenye hizi taasisi kwa ajili ya kutengeneza dawa halisi na dozi halisi, na wao faida wataipata, kuliko kufanya usanii wa mwaka, taratibu na sharia za kufanya hivyo zipo, ni kuzifuata tuu.
Tatizo la mwaka, na akina ndodi, rahabu rubago, mandai, lupimo sanitarium na kadhalika ni kujifanya wajuaji na kupingana na sharia,wakiongozwa na kubwa la wasanii,na tapeli,jizi, uaji mwaka.
 
Back
Top Bottom