Access Bank imekuja kutuumiza

Access Bank imekuja kutuumiza

badoo

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2014
Posts
512
Reaction score
249
Katika kufuatilia mabenki mengi yanayotoa mikopo kwa wajasiriamali wadogo ACCESS BANK ni benki moja hatari Sana kwa kuwa na kiwango kikubwa mno cha RIBA.

Na pia ni wasumbufu Sana ikikaribia siku tano kabla ya rejesho,utapigiwa simu na kutumiwa sms kukumbushwa deni utadhani umewaambia hulipi,kwa mfano ukikopa sh milioni mbili na nusu 2500,000/= .

Utalazimika kulipa riba ya milioni moja na elfu mbili 1,002,000/= ni riba kubwa Sana ukitafautisha na mabenki mengine,mamlaka husika mnafuatilia uendeshaji wa mabenki nchini au ndio kuwapa kibali tu na kuwaacha wafanye watakavyo?
 
Mabenki yote Mkuu yanaumiza ile mbaya kupitia riba ingawa yanatofautiana! Kwa ufupi Mkuu karibu huku CRDB "the bank that listen" u-enjoy maisha ya kukopa!

Huku unakopa 5m unarejesha 5.9m kwa maana ya 18% interest! Kurejesha wala hupigiwi simu mpaka zipite siku kadhaa bila kuweka hela kwenye akaunti!!
 
Una uhuru wa kuchagua mabenki yanayotoa mikopo ni mengi sio lazima uende kwao
 
Sitakopa tena Access Bank. PR sio nzuri na lugha yao haizingatii heshima na adabu. Nini masiku! Masaa tuu utatishiwa kufilisiwa.
 
Wanigeria hao unategemea nini? Wameona Bongo watu kama wamelala vile. Pia usimamizi wa BoT sio mzuri. Nchi nyingine hawafanyi upuuzi huo!
 
Dah hawa jamaa nina rafiki zangu wawili wamewapeleka mahkamani.
Tatizo la nchi ni serikali tuu inayoacha biashara huru kila mwenyeubavu anakula kwakamba yake
 
Mkuu badoo hebu funguka hiyo riba uliyosema hapo juu 1,002,000 ni sawa na 40% ni kwa muda gani?
 
Si mchezo
Serikali isiyosimamia utendaji wa taasisi mbalimbali za uchumi nchini ni serikali dhaifu sana.
Na udhaifu mara nyingi unachangiwa na rushwa na ndugu yake ufisadi.
Enewei, wacha tuyaache hayo kwa sasa. Si mmemsikia Rais amekiri kwamba amefeli kwenye kilimo.
Huwezi jua kesho atasema amefeli kwenye nini tena.
Ngoja tumsikilizie
 
Serikali corrupt....refer the late mwl. J.k. Nyerere.

Ahahahahahaha...bora aje mwanaye atusaidie kuirejesha nchi baba yake alipotaka iendee...wasira hoyeeee, wanawake hoyeeeeeeeeeeee. Refer charles makongoro nyerere.
 
kinachotokea Access ni hv ukihitaji mkopo kwao masharti ni nafuu mno na unaupata fasta,sasa watu wengi huwa hawaangalii kabisa kuhusu riba,ukija kushtuka..tayari....washatoboa spika...inakoroma tu
 
amekiri amefeli kwn kilimo? lini hiyo? manake cjaiskia ningecheka sana! lakn kilimo c ndicho kilichompa uprof? kama ni kweli aibu kwa wachina waliomtunuku uprof
 
amekiri amefeli kwn kilimo? lini hiyo? manake cjaiskia ningecheka sana! lakn kilimo c ndicho kilichompa uprof? kama ni kweli aibu kwa wachina waliomtunuku uprof[/QUOTE





Samahani tunazungumzia riba za access bank
 
He hee hee! Mwenzenu mpaka nimeshapata BP kutokana na marejesho. Yan haka kamkopo niliko nako kakiisha, sikopi tena. Mabenki madogo madogo ukichelewa kuwa lipa wana ku demonize. Yan watakutukana matusi yote ya kistaarabu na kukutolea lugha kali, kukukaripia n.k utadhani umefanya dhambi kubwa iliyoje...
 
Jamani mbona riba kwenye hiyo benki haisemwi ni kiasi gani au ndio yale yale chukua 2,500,000 wewe rudisha 6,502,000 kama mleta uzi alivyiowasilisha hapo juu bila kujua riba hapo kama ni 40%?
 
Ndugu ulilosema ni kweli ni mara mia ukope kwenye vicoba kuliko
kwenye hii benki.
Wana utaratibu wao mfano ukiweka gari lako
kama dhamana wanahakikisha wanalikadria kadrio la chini kabisa(namaanisha bei ya hilo gari)
na hivyo kujikuta wanakuhitaji uweke vitu vingi kama dhamana.

Binafsi nashauri kama huna shida kubwa
inayoweza kukugharimu maisha sikushauri
kukopa benki hii.
 
Back
Top Bottom