Nimelisoma tamko la Barrick, wamezungumza kuwa kutakuwa na FIFTY-FIFTY split ya economic benefits. Na Barrick hawakumung'unya maneno wakasema kuwa ile FIFTY yetu itatokana na royalties, kodi na asilimia 16 nyingine ( free carry interest).
Unaweza kulisoma tamko la Barrick hapa:
Barrick Gold Corporation - Barrick Comments on Proposed Framework for Acacia Mining plc Operations in Tanzania
Kwa hiyo ni dhahiri, tamko la Barrick liko wazi na linajieleza, hata hivyo, kwa mujibu wa uwekezaji katika madini as far as I know mpaka june mwaka huu , Kodi zifuatazo zilikuwa zikitozwa katika sector ya madini
1. Coprorate Income tax (Kwa kampuni ya madini hii ni kodi katika faida nzima inayopatikana katika madini) ambayo ni 30%
2. Huwa kuna Mirahaba (Royalties) kwa mujibu wa sheria ya zamani ilikuwa 4%, Lakini kwa sheria ya sasa itakuwa 6% kwa madini ya dhahabu.
Ukiachilia mbali na hizo:
(1) Bado kuna duties and levies
(2) Bado kuna free carried Interest ya asilimia 16%(Yaani hizi ni share za bure kwa serikali ambazo serikali hata bila ya kuchangia mtaji ni za kwake):
ukiangalia hizo percentage : Ukichukua 30% ya Income Tax + 16% ya Free carried Interest =
46%
(Hii ni baada ya sheria ya madini kufanyiwa marekebisho mwaka 2017, kwa kupandisha Free carried Interest mpaka 16% kutoka ile 10%).
Laiti tungetumia sheria ya zamani economic benefit yetu ingekuwa 30% Income tax +10% Free carried Interest =
40%, yaani utaona kuwa imepanda kwa 6% tu baada ya sheria mpya
Halafu ukichukulia zile 6% za mrahaba Plus Duties and levies bila shaka kwa jinsi ninavyoona roughly itakwenda Kucover zile
4% iliyobaki ili kutengeneza
50% ambayo Barrick wao wanaita economic benefit. I see kwamba kabla ya dili hili na Barrick halali yetu ingekuwa roughly ni 40% +4% =
44%
So as far as I see na kwa jinsi nilivyowaelewa maelezo ya Barrick ni kwamba, Deal jipya na Barrick limetuwezesha kupanda kutoka roughly 44% hadi 50%, Ongezeko la Takriban 6% tu!