PreGE2025 Absalom Kibanda ahoji CHADEMA kutaka Habari Leo wachukuliwe hatua badala ya Makalla, asema ni kuingilia Uhuru wa Habari

PreGE2025 Absalom Kibanda ahoji CHADEMA kutaka Habari Leo wachukuliwe hatua badala ya Makalla, asema ni kuingilia Uhuru wa Habari

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
2,786
Reaction score
7,567
Yaani hii imenishangaza kwakweli, inakuaje aachwe aliyetamka halafu lawama liende kwenye gazeti? Yaani ni kama vile hawajamuona Makalla kabisaa kwa kwenda kulishukia gazeti.

Au wanakubali alichokisema Makalla, maana hata kusema wanazua taharuki bado hawajakana alichosema Makalla

Pia soma Pre GE2025 - Habari Leo waondoa taarifa ya Makalla kuwatuhumu CHADEMA kutaka kusambaza Ebola, wasema haikuwasilishwa kwa usahihi

===

Kupitia ukurasa wake wa X Absalom Kibanda amendika haya,

"Makosa yafanywe na Katibu wa Uenezi na Mafunzo wa CCM halafu vyombo vya habari ndiyo vibebe mzigo wa lawama. Huku ni kuingilia uhuru wa habari kwa gharama za kukwepa UWAJIBIKAJI wa viongozi wa UMMA. CPA Makalla awajibike kwa kauli yake"

IMG_20250324_002905_931.jpg

Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
 
..mbona sioni popote ambapo Habari Leo wamelaumiwa kutokana na kauli ya Makala?

..pia naamini vyombo vingi vimeripoti madai ya Makala, mbona wanatajwa Habari Leo peke yao?
 
Mzee wa ebola amechemka
Watanzania sio wajinga tena

Anayechelewesha msafara siku zote ni ng'ombe wa mbele ila anachapwa wa nyuma na ndiyo anapiga kelele
 
Baada ya taarifa zilizosambaa kuhusu CPA Makala na siasa uchwara za kutuhumu chadema waziwazi kuwa wanapanga kununua virusi vya MPOX na Ebola Ili kuuwa watanzania sasa moto umeanza kurudi. Ameshindwa kutoka na kudanganya kuwa amenukuliwa vibaya kwakua kila mtu alimsikia na alirekodiwa na vyombo vyote vya habari.

Habari Leo wanajaribu kumbeba lakini inashindikana kwakua hana la kujitetea kwaiyo alichosema ndiyo msimamo wa CCM.

Cha kushangaza Habari Leo wamepewa maelekezo ya kushusha iyo taarifa ya Makala ila it is too late. Habari Leo mnasema mmeshindwa kubalance habari, mlitaka kubalance kitu mashine zenu zilirekodi live? Au mnataka kusema Makala hakusema haya.? Embu watanzania someni hii taarifa ya Habari Leo mseme wanamaanisha nini
 

Attachments

  • VID-20250323-WA0009.mp4
    11.3 MB
  • IMG-20250324-WA0000.jpg
    IMG-20250324-WA0000.jpg
    58.2 KB · Views: 26
Back
Top Bottom