KERO Abood mnatukosea sana Abiria wenu

KERO Abood mnatukosea sana Abiria wenu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
ABOOD tokea zamani inatoka Arusha kwenda moro hawana shida wale .kazi yao nikupatisha watu ajali akuna jingine
 
Mdogo wangu alikatiwa Abood ya kutoka Dar-Mwanza asubuhi. Kumbe hakuna hata route hiyo ya asbh siku hizi. Anafika stendi alfajiri anaambiwa hilo bus halipo kuna la jioni tu. Yeye na abiria wengine wakapelekwa Isamilo.
 
Kampuni ya Mabasi ya Abood mnatukosea sana Abiria wenu,haiwezekani tumekata tiketi ya bus la kwenda Mbeya lililotakiwa kuondoka saa Tisa na nusu lakini mpaka muda huu hakuna bus.

Wafanyakazi wenu wa hapa Magufuli wanatujibu hovyo yaani wanatuona sisi kama takataka.

Huu ni upuuzi wa kiwango Cha juu,kama biashara imewashinda kafanyeni shughuli zingine

Wafanyakazi wenu hawajui kuongea vyema na wateja.

View attachment 3392779
Hata abood ya tunduma jana ilichelewa sana kutoka Dar, nadhani saa 11 kasoro hivi ndio ilitoka mlogoro ikaingia saa tano za usiku😅😅😅, uyole ikaingia saa nne kama na dk 40 hivi...
 
Kampuni ya Mabasi ya Abood mnatukosea sana Abiria wenu,haiwezekani tumekata tiketi ya bus la kwenda Mbeya lililotakiwa kuondoka saa Tisa na nusu lakini mpaka muda huu hakuna bus.

Wafanyakazi wenu wa hapa Magufuli wanatujibu hovyo yaani wanatuona sisi kama takataka.

Huu ni upuuzi wa kiwango Cha juu,kama biashara imewashinda kafanyeni shughuli zingine

Wafanyakazi wenu hawajui kuongea vyema na wateja.

View attachment 3392779
Kwa mbeya siku nyingine panda
FIRST PRIORITY
1. Katarama
2. NewForce/Golden Dear
3. ABC
4. Achimwene

SECOND PRIORITY
1. Hai Travelaz
2. New Songo
3. Luwinzo
4. Sweet Africa
5. Kimbinyiko
6. Happy Nation

THIRD PRIORITY
1. Rungwe Express
2. Green Line
3. Abood
4.
 
Binafsi nikitaka kusafiri naenda stand tiketi nakatia mlangoni kwenye gari.
Wiki hii ilioisha kuna mtu nilimsindikiza anaenda Tanga mbona tulikaa masaa ma4 mpaka nikamuacha tunapiga stori tu tangu saa8 gari ikaondoka saa 12 Abiria hamna
 
Abood kale katabia ka mkifika pale Moro mnaingia mule gereji kwao wanakaa almost 30 minutes to 1 hour ni ka kifala.

First time nikahisi bahati mbaya. Second time nikajiuliza au ni mimi nina bahati mbaya?

Kutoka hapo ikawa ni ABC Upper Class tu.
 
Back
Top Bottom