Abiria kadhaa wanusurika kuungua baada ya gari kuwaka moto

GM7

JF-Expert Member
Jun 26, 2009
492
24
Wakati Tanzania kukiripotiwa matukio mbalimbali hasa ya ajali za moto, leo nimenasa tukio lingine majira ya saa 8:50 mchana (2:50PM) katika eneo la Iyunga karibu na kituo cha garimoshi cha TAZARA Mbeya ambapo basi la abiria aina ya Hiace liliwaka moto kama linavyoonekana kwenye picha.

Kwa mujibu wa walikuwa karibu kabisa na tukio abiria wote wamenusurika na hakuna aliyejeruhiwa.

Muda mfupi kabla ya kupatwa na tukio hilo basi hilo lilisimamishwa na trafiki waliokuwa eneo la TAZARA Mbeya na baada ya tu kuruhusiwa kupita gari lilienda mbele kama mita 100, na kusimama pembeni na kuamriwa kutelemka mara moja na ndipo baada ya dakika chache gari likashika moto na kuanza kuungua.

Mwenye swali anaweza kuniuliza kuhusiana na tukio hili maana nilikuwepo karibu kabisa na tukio.

Tumwombe Mungu atuepushe na majanga haya na mengine yote. Amina


attachment.php


attachment.php


attachment.php
 

Attachments

  • Image004.jpg
    Image004.jpg
    29.2 KB · Views: 250
  • Image015.jpg
    Image015.jpg
    26.6 KB · Views: 235
  • Image017.jpg
    Image017.jpg
    25.6 KB · Views: 236
duh humo ndani ya basi kulikua na abiria? kama wamenusurika wakachinje kuku na kufanya ibada kumshukuru mungu wao kwa kuwanusuru na kifo kibaya cha moto
 
duh humo ndani ya basi kulikua na abiria? kama wamenusurika wakachinje kuku na kufanya ibada kumshukuru mungu wao kwa kuwanusuru na kifo kibaya cha moto
Abiria wote wamenusurika. Na bahati nzuri gari lilianza kuwaka likiwa limesimama, sijui lingekuwa kwenye mwendo sipati picha ingekuwaje. Kwa kweli wamshukuru Mungu na wafanye ibada ya kushukuru Mungu akiwemo na dereva mwenyewe ambaye mara baada ya kugundua tatizo kwenye gari lake aliamua kusimamisha gari pembeni na kuamuru abiria wote kushuka mara moja.
 
kila kukicha majanga nini kilisababisha moto huo??
Sina hakika sana na chanzo cha moto huo, ila baadhi ya mashuhuda wanasema maji ya kupoozea injini hiyo yalikwisha na wengine wanasema iliishiwa mafuta hivyo dereva alikuwa anaikaanga.
 
madereva jamani, pls kagueni magari kabla ya kuanza safari, msiyaweke rehani maisha ya watu, chonde chonde,
 
Back
Top Bottom