Dalton elijah
JF-Expert Member
- Jul 19, 2022
- 796
- 1,848
Anaadika Baba Askofu Rev.Dr.Benson Bagonza (PhD), Mkuu wa KKKT Dayosisi ya Karagwe.
HAZINA ILIPO NDIPO MOYO WAKO ULIPO: Tunaiuzaje? (Mathayo 6:21).
Wajaluo wana kitu kinaitwa “NYANTAKOLWAKOLWA”, yaani “akiba au hazina maalum isiyoguswa guswa bila utaratibu”.
1. Hazina hii hutunzwa mahali pa siri na panapolindwa kwa umakini mkubwa.
2. Familia inaweza kulala njaa, mgonjwa akakosa matibabu, na hata ng’ombe akauzwa lakini NYANTAKOLWAKOLWA haiguswi.
3. Hazina hii huguswa endapo uhai wa Mkuu wa Kaya umo mashakani au yuko katika hatari ya kupelekwa kifungoni.
4. Hazina hiyo inaweza kuguswa endapo mali nyingine zooote zimeshindwa kutatua tatizo linaloikabili familia au hizo hazina thamani ya kutatua tatizo hilo.
5. Ili kuigusa hazina “ISIYOGUSIKA”, kibali huwa kinatafutwa. Kwa familia sharti Mkuu wa Familia, Mtoto mkubwa kiume, Mke mkubwa endapo kuna zaidi ya mmoja, na rafiki wa damu wa familia (omukago) ili wakubali kuwa NYANTAKOLWAKOLWA “isiyogusika kirahisi” iweze kugusika ili kuokoa uhai wa Mkuu wa Kaya.
6. Endapo imekubalika kuwa hazina hiyo iguswe ili kutatua tatizo la familia, basi wana ukoo hujulishwa na kupewa fursa ya kwanza “kuigusa” ISIYOGUSIKA kabla ya kuwafikiria watu wa nje. Ni hatari mtu wa nje kunufaika na NYANTAKOLWAKOLWA bila ridhaa ya wanaukoo.
7. Hata mwana ukoo ambaye hajazaliwa ana haki ya kukua na kudai na kukomboa NYANTAKOLWAKOLWA ya familia au ukoo.
Lakiniiiiiii
Wajaluo hap hao wanasema, Fimbo uliyo nayo mkononi ndiyo unaitumia kumuua nyoka. Huwezi kuazima fimbo unapokabiliwa na hatari.
Lakiniiiiiii
Ukitumia fimbo ikavunjika au ikaisha, na nyoka wakaendelea kuja, unafanyaje na fimbo zimeisha?
Bwana akamwambia Musa, “una nini mkononi mwako?” Akajibu, “ni fimbo”(Mwanzo 4:2).
Mpaka Musa anakufa katika nchi ya Moabu, fimbo (NYANTAKOLWAKOLWA) alikuwa nayo.
Uamuzi wa kuuza NYANTAKOLWAKOLWA ni shirikishi.
Tusile Mbegu kama mvua haijanyesha.
HAZINA ILIPO NDIPO MOYO WAKO ULIPO: Tunaiuzaje? (Mathayo 6:21).
Wajaluo wana kitu kinaitwa “NYANTAKOLWAKOLWA”, yaani “akiba au hazina maalum isiyoguswa guswa bila utaratibu”.
1. Hazina hii hutunzwa mahali pa siri na panapolindwa kwa umakini mkubwa.
2. Familia inaweza kulala njaa, mgonjwa akakosa matibabu, na hata ng’ombe akauzwa lakini NYANTAKOLWAKOLWA haiguswi.
3. Hazina hii huguswa endapo uhai wa Mkuu wa Kaya umo mashakani au yuko katika hatari ya kupelekwa kifungoni.
4. Hazina hiyo inaweza kuguswa endapo mali nyingine zooote zimeshindwa kutatua tatizo linaloikabili familia au hizo hazina thamani ya kutatua tatizo hilo.
5. Ili kuigusa hazina “ISIYOGUSIKA”, kibali huwa kinatafutwa. Kwa familia sharti Mkuu wa Familia, Mtoto mkubwa kiume, Mke mkubwa endapo kuna zaidi ya mmoja, na rafiki wa damu wa familia (omukago) ili wakubali kuwa NYANTAKOLWAKOLWA “isiyogusika kirahisi” iweze kugusika ili kuokoa uhai wa Mkuu wa Kaya.
6. Endapo imekubalika kuwa hazina hiyo iguswe ili kutatua tatizo la familia, basi wana ukoo hujulishwa na kupewa fursa ya kwanza “kuigusa” ISIYOGUSIKA kabla ya kuwafikiria watu wa nje. Ni hatari mtu wa nje kunufaika na NYANTAKOLWAKOLWA bila ridhaa ya wanaukoo.
7. Hata mwana ukoo ambaye hajazaliwa ana haki ya kukua na kudai na kukomboa NYANTAKOLWAKOLWA ya familia au ukoo.
Lakiniiiiiii
Wajaluo hap hao wanasema, Fimbo uliyo nayo mkononi ndiyo unaitumia kumuua nyoka. Huwezi kuazima fimbo unapokabiliwa na hatari.
Lakiniiiiiii
Ukitumia fimbo ikavunjika au ikaisha, na nyoka wakaendelea kuja, unafanyaje na fimbo zimeisha?
Bwana akamwambia Musa, “una nini mkononi mwako?” Akajibu, “ni fimbo”(Mwanzo 4:2).
Mpaka Musa anakufa katika nchi ya Moabu, fimbo (NYANTAKOLWAKOLWA) alikuwa nayo.
Uamuzi wa kuuza NYANTAKOLWAKOLWA ni shirikishi.
Tusile Mbegu kama mvua haijanyesha.