Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,190
- 34,526
RIWAYA: C.O.D.EX 4
(A Missing Soldier)
MTUNZI: Frank Masai
MAWASILIANO: 0717 738973
SEHEMU YA KWANZA.
“Tulikuwa ni watu kama watu wengine. Tuliwapenda wazazi wetu kama watoto wengine. Tuliishi na kufurahi kama watu wengine. Na tukapata malezi bora kama watoto wengine. Lakini mambo yalikuja kubadilika baada ya kuingia mikononi mwa Wanasayansi. Watu ambao hawajali uwepo wa nyama miili mwetu na mzunguko wa damu katika mishipa ya damu. Wakapandikiza kemikali zao kwenye damu zetu, wakatengeneza miili yao kwa kutumia nyama zetu. Na hatimaye tukaitwa wanajeshi. Na tena wanajeshi wenye uwezo wa kipekee duniani. Maisha ni kama upepo, ukiamua kubadilika, hubadilika bila kuambiwa ubadilike. Maisha yetu yakabadilikia hapo, na sasa tukaitwa wanajeshi hatari.”
NEW YORK, MAREKANI.
Kulikuwa ndani ya jengo kubwa na lenye mwanga mkali kila mahali. Watu mbalimbali walioenekana ndani ya mavazi ya kitabibu huku wamekamata Ipad za gharama ambazo walionekana wakizichezea chezea na wakati huohuo wakiangalia miili ya watu iliyokuwepo ndani ya majokofu yenye matirio ya kioo na ndani yake kulikuwa na maji yaliyojaa. Binadamu waliokuwepo humo, waliingiziwa mipira midomoni na puani na walibandikwa vitu fulani vifuani mwao kwa ajili ya kupima mapigo yao ya moyo.
“We called them, New Generation Soldiers, Sir (Tunawaita Wanajeshi wa Kizazi Kipya, Mkuu)” Aliongea bwana mmoja ambaye alikuwa nje ya maabara ile lakini aliweza kuona kila kinachoendelea kupitia kioo kikubwa kilichokuwa ndani ya jengo lile.
“Are you sure about your generation? (Unahakika na kizazi chako)” Bwana mmoja mwenye suti na mwenye asili ya Kimarekani, alimuuliza yule tabibu aliyekuwa kasimama pembeni yake akijinadi juu ya wale wanajeshi waliokuwa ndani ya majokofu zaidi ya hamsini.
“Yes Prime Minister. These are the best soldiers we ever created before. They can fight for so long without tired. (Ndio Waziri Mkuu. Hawa ni wanajeshi bora kuliko tuliyowahi kuwatengeneza hapo kabla. Wanaweza kupigana kwa muda mrefu bila kuchoka)” Akajibu yule tabibu ambaye alivaa kitambulisho kilichoonesha sura yake, jina na cheo chake. Bwana mmoja aliyekuwa na asili ya Kimarekani, na ilionekana kuwa kaongozana na Waziri Mkuu, aliangalia kitambulisho hicho kabla hajaongea.
“Tutegemee nini katika wanajeshi wako Dokta Ice Mujo.” Akauliza yule bwana aliyeongozana na Waziri Mkuu kwa lugha ya Kiingereza.
“Maajabu ya dunia. Wanajeshi watano pekee, wanaweza kuingamiza Urusi yote ndani ya saa moja. Tumewapachika uwezo wa kipekee na silaha nzito wanazo vichwani mwao.” Alijibu Dokta Ice.
“Silaha gani hiyo Dokta?” Akauliza tena bwana aliyeongozana na Waziri Mkuu.
“Nyuklia bombs. Kila mwanajeshi hapo, kabla hajaenda mapambanoni, tunampandikiza chip ndogo ambayo inaweza kuruhusu mabomu ya nyuklia yalipuke mahali ambapo yatapandikizwa. Kati ya wanajeshi watano tunaoweza kuwatuma, wawili ni lazima wawe na mabomu ya Nyuklia. Hawa ndio wanauwezo wa kipekee.” Alijibu Daktari.
“Wanauwezo gani?” Akauliza Waziri Mkuu.
“Angalia hii.” Akamsogezea Ipad. Kisha akabonyeza sehemu ya video na hapo wakaanza kuonekana wanajeshi wakifanyiwa majaribio. Picha ambayo iliwafanya wale mabwana waliokuja pale kushangaa, ni mlipuko mkubwa uliotoka kwenye mwili wa mwanajeshi mmoja, halafu baada ya mlipuko huo, yule mwanajeshi alitoka ndani ya moto akiwa anawaka lakini akitembea bila wasiwasi… Baadae moto huo unazima, na mwanajeshi anaoekana hana makovu yoyote ya moto licha ya nguo zake zote kuungua.
“Hatari sana hii.” Aliongea waziri mkuu huku katabasamu.
“Hiyo ndio C.O.D.EX improved chemical.” Daktari alijigamba kwa mbwembwe.
“Kwa hiyo ni ile C.O.D.EX ya wale wanajeshi wengine?” Aliuliza bwana yule aliyeongozana na Waziri Mkuu.
“Ndio Waziri wangu wa Ulinzi.” Kwa tabasamu pana alijibu Dokta Ice.
“C.O.D.EX ni nini?” Akauliza Waziri Mkuu.
“Ni kifupisho cha maneno haya, CINDREX OLTIVIASO DECA ENDROLINE X. Ni chemikali zilizobuniwa miaka kumi nyuma na walitengenezwa wanajeshi kadhaa ambao walisumbua sana CIA na FBI. Baada ya kujua kemikali hizi, CIA waliweza kuharibu maabara yote ya kutengenezea wanajeshi hawa. Sasa hivi ndio tumepewa kibali cha kutengeneza silaha kupitia kemikali hizi.” Alijibu Daktari.
“Kuna tofauti gani kati ya wanajeshi hawa na wale wa miaka kumi iliyopita? Hawawezi kuleta madhara kama yale?” Aliuliza Waziri wa Ulinzi.
“Hapana. Hawawezi fanya hivyo. Tatizo kubwa la wale waliyopita, hawakuwatoa kumbukumbu wale waliowatengeneza, hivyo ilikuwa rahisi kwa zile kemikali kurudisha kumbukumbu baada ya kuanza kuisha. Hilo likaleta tatizo kwa baadhi ya wanajeshi ambao kumbukumbu ziliwarudia.” Akajibiwa.
“Okay. Kwa hiyo hawa hawana kumbukumbu?” Akauliza tena Waziri wa Ulinzi.
“Ndio. Kabla hatujawaingizia C.O.D.EX, tulihakikisha kwanza tunafuta kumbukumbu zao zote za maisha yaliyopita. Tuna uhakika tumefanikiwa katika hilo.” Alijibiwa na daktari.
Waziri wa Ulinzi akaangaliana na Waziri Mkuu kisha kwa ishara fulani walipeana kuonesha kuwa wamekubaliana na ile kazi ya C.O.D.EX.
“Sawa Dokta. Ila kwanza ni lazima tufanye majaribio na silaha zako.” Waziri wa Ulinzi aliongea na kumpa nafasi dokta naye aongeze jambo kama analo.
“Mmepanga wapi kufanya majaribio yenu?” Akauliza Dokta.
“Iraq na Iran.” Akajibiwa na dokta akaonesha kukubaliana na majibu hayo.
“Ila kuna jambo moja ambalo tumelipandikiza kwenye miili yao.” Akakumbusha daktari.
“Lipi hilo?” Akaulizwa.
“Hawana huruma hata kidogo. Kitendo cha huruma kwao kimepita kushoto. Kwa hiyo hayo majaribio, tujaribu kuyafanya mbali na raia.” Akaongea dokta.
“Hamna shida.” Akajibiwa na Waziri wa Ulinzi kwa kifupi.
Baada ya maongezi hayo marefu, wale viongozi wa serikali ya Marekani, walianza kuondoka eneo lile huku nyuma wakifuatiwa na walinzi wao muhimu kabisa.
****
BAADA YA WIKI MBILI.
Vyombo vya habari duniani vilikuwa vinatangaza kuhusu Iran kuvamiwa na mitambo yake ya nyuklia kuharibiwa vibaya na wakati huo mateka wa Iraq walisemekana kuwa wamekombolewa na wanajeshi wa jeshi la Marekani lakini hawatambuliki ni wapi walipo. Habari zilikuwa zimezagaa na kuzusha maswali kadhaa kwenye vichwa vya habari na watu wote kwa ujumla.
Vyombo vya habari viliuliza kuhusu wanajeshi hao na Waziri Wa Ulinzi alithibitisha uwepo wa wanajeshi hao na kuahidi kuwa, Marekani itakuwa na nguvu kubwa kuliko nchi yoyote duniani.
Wakati hayo yanaendelea, daktari mkuu wa ile maabara alikuwa anatazama na kusikiliza vyombo vya habari kila kukicha. Jambo ambalo hakuwaambia wale viongozi, ni uwezo wa wale wanajeshi kuchukua matukio yote kwenye chipu iliyokuwa imepandikizwa vichwani mwao kwa ajili ya kuwatuma wafanye mambo fulani.
“Wajinga sana hawa. Niliwaambia wasifanye majaribio kwenye makazi ya raia wema. Matokeo yake wamewaua mateka wote. Washenzi sana. Natakiwa kufanya jambo moja muhimu sana kabla sijaondoka hapa.” Alijiwazia Dokta Ice na hapohapo akaifata kompyuta yake iliyokuwa katika ofisi ndogo kwenye chumba chake na kuanza kusoma mambo kadhaa kwenye mafaili yaliyokuwepo kwenye kompyuta hiyo.
Kesho yake ilikuwa Asubuhi ya Jumapili yenye bashasha nyingi sana. Dokta akiwa anajua wazi kabisa kuwa siku hiyo ni ya mapumziko kwake, alitoka ndani ya nyumba yake akiwa kakamata mkoba wenye makaratasi kadhaa, kisha akapanda gari lake la gharama na kuelekea zilipo ofisi zao.
Huko aliamrisha baadhi ya wafanyakazi waondoke kwa sababu alikuwa na kazi nyeti ya kufanya bila wao kuijua. Alipofanikiwa kuwatoa, akafungua jokofu moja ambalo lilikuwa tofauti na yale mengine. Lenyewe lilikuwa halioneshi na lilifanana na lile la kuhifadhia maiti. Alipolifungua, akaonekana muafrika mmoja aliyekuwa kafumba macho yake kama marehemu na mvuke ukimtoka kwa sababu ya kuganda kwa mwili wake.
Ice Mujo, akabofya vitufe kadhaa kwenye lile jokofu nalo likaanza kuvia maji ambayo yalikuwa ya moto. Maji hayo yakayayusha barafu iliyopo mwilini mwa muafrika yule na kumfanya awe laini na mwenye hali ya umoto.
Akabofya tena vitufe kadhaa kwenye ipad yake. Vitu fulani vikatokea angani na kisha vikashuka hadi kwenye lile jokofu. Vikazama ndani ya maji na kumkamata yule bwana, kisha vikatoka naye na kumuweka kwenye lile jokofu lingine ambalo lilikuwa linauwezo wa kujazwa maji pamoja mitambo ya kumuwezesha binadamu kupumua.
Dokta Ice, akambandika vile vifaa vya mapigo ya moyo pamoja na mipira maalumu kwa ajili ya kupumulia. Alipomaliza, akafunga lile jokofu na kufungulia maji yaliyoanza kujaa ndani yake.
Akasogea kwenye kompyuta inayoonesha hali ya yule binadamu muafrika. Akaanza kuruhusu kemikali aina ya C.O.D.EX ianze kuingia mwilini mwa yule bwana. Kilikuwa ni kitendo cha dakika kumi pekee kukamilisha tendo lile na lilifanikiwa kwa sababu muafrika yule alianza kupumua akiwa ndani ya jokofu lile.
Kwa haraka, akabonyeza tena vitufe kwenye kompyuta na hapohapo maji yakaanza kupungua na baada ya kuisha yote, yule bwana alijikuta akisogezwa nyuma kwa kasi na kisogo chake kikagota nyuma ya kidirisha kidogo ambacho kilifunguka na hapohapo mwanga fulani mwekundu ukaanza kupitia sehem hiyo ya kisogoni. Kisogo cha yule bwana kikafunuliwa kidogo kwa kutumia ule mwanga ambao ulitumika kukata sehemu hiyo.
Kiasi kidogo cha ubongo kikatolewa, na baada ya hapo, Dokta Ice alifungua mkoba wake na kutoa Diskette na kuchomeka kwenye sehemu maalumu ya kwenye komyuta aliyokuwa anaitumia. Ikaanza kusoma harakahara na baadaye ikaandika ‘loading succefully, 100%’. Dokta akashusha pumzi na kisha akabofya kitufe cha Enter. Hapo kule kwenye kisogo cha yule bwana, ikapandikizwa chipu na kisha ile ngozi iliyotolewa kisogoni, ikapachikwa na kupitiwa na mwanga ule mwekundu. Pakarudi vilevile.
Yule muafrika akatoka kule alipobananishwa na kusogezwa katikati ya lile jokofu. Dokta akabonyeza tena vitufe kadhaa kwenye kompyuta yake, yule bwana akaanza kuzunguka taratibu kwenye lile jokofu kw a dakika zipazo kumi. Aliposimama, kompyuta ikaongea kwa sauti ya kike, ‘upgrade complete’. Kisha maji yakajazwa ndani ya jokofu na dokta akawa kamaliza kazi ambayo alipanga kuifanya jana yake.
Dakika ishirini mbele, akamtoa mtu yule kwenye jokofu na kumuingiza kwenye mashine nyingine iliyoanza kuupembua mwili wa muafrika yule hadi ikaridhika na kutamka maneno mengine ya kiingereza, ‘Scan Complete’.
Dokta Ice akatabasamu baada ya kufungua mashine ile na yule muafrika kusimama mwenyewe na kumtazama Dokta.
“Nipo tayari kukutumikia mkuu.” Aliongea bwana yule kwa Kiingereza na kumfanya Dokta kuzidi kutabasamu.
ITAENDELEA.
(A Missing Soldier)
MTUNZI: Frank Masai
MAWASILIANO: 0717 738973
SEHEMU YA KWANZA.
“Tulikuwa ni watu kama watu wengine. Tuliwapenda wazazi wetu kama watoto wengine. Tuliishi na kufurahi kama watu wengine. Na tukapata malezi bora kama watoto wengine. Lakini mambo yalikuja kubadilika baada ya kuingia mikononi mwa Wanasayansi. Watu ambao hawajali uwepo wa nyama miili mwetu na mzunguko wa damu katika mishipa ya damu. Wakapandikiza kemikali zao kwenye damu zetu, wakatengeneza miili yao kwa kutumia nyama zetu. Na hatimaye tukaitwa wanajeshi. Na tena wanajeshi wenye uwezo wa kipekee duniani. Maisha ni kama upepo, ukiamua kubadilika, hubadilika bila kuambiwa ubadilike. Maisha yetu yakabadilikia hapo, na sasa tukaitwa wanajeshi hatari.”
NEW YORK, MAREKANI.
Kulikuwa ndani ya jengo kubwa na lenye mwanga mkali kila mahali. Watu mbalimbali walioenekana ndani ya mavazi ya kitabibu huku wamekamata Ipad za gharama ambazo walionekana wakizichezea chezea na wakati huohuo wakiangalia miili ya watu iliyokuwepo ndani ya majokofu yenye matirio ya kioo na ndani yake kulikuwa na maji yaliyojaa. Binadamu waliokuwepo humo, waliingiziwa mipira midomoni na puani na walibandikwa vitu fulani vifuani mwao kwa ajili ya kupima mapigo yao ya moyo.
“We called them, New Generation Soldiers, Sir (Tunawaita Wanajeshi wa Kizazi Kipya, Mkuu)” Aliongea bwana mmoja ambaye alikuwa nje ya maabara ile lakini aliweza kuona kila kinachoendelea kupitia kioo kikubwa kilichokuwa ndani ya jengo lile.
“Are you sure about your generation? (Unahakika na kizazi chako)” Bwana mmoja mwenye suti na mwenye asili ya Kimarekani, alimuuliza yule tabibu aliyekuwa kasimama pembeni yake akijinadi juu ya wale wanajeshi waliokuwa ndani ya majokofu zaidi ya hamsini.
“Yes Prime Minister. These are the best soldiers we ever created before. They can fight for so long without tired. (Ndio Waziri Mkuu. Hawa ni wanajeshi bora kuliko tuliyowahi kuwatengeneza hapo kabla. Wanaweza kupigana kwa muda mrefu bila kuchoka)” Akajibu yule tabibu ambaye alivaa kitambulisho kilichoonesha sura yake, jina na cheo chake. Bwana mmoja aliyekuwa na asili ya Kimarekani, na ilionekana kuwa kaongozana na Waziri Mkuu, aliangalia kitambulisho hicho kabla hajaongea.
“Tutegemee nini katika wanajeshi wako Dokta Ice Mujo.” Akauliza yule bwana aliyeongozana na Waziri Mkuu kwa lugha ya Kiingereza.
“Maajabu ya dunia. Wanajeshi watano pekee, wanaweza kuingamiza Urusi yote ndani ya saa moja. Tumewapachika uwezo wa kipekee na silaha nzito wanazo vichwani mwao.” Alijibu Dokta Ice.
“Silaha gani hiyo Dokta?” Akauliza tena bwana aliyeongozana na Waziri Mkuu.
“Nyuklia bombs. Kila mwanajeshi hapo, kabla hajaenda mapambanoni, tunampandikiza chip ndogo ambayo inaweza kuruhusu mabomu ya nyuklia yalipuke mahali ambapo yatapandikizwa. Kati ya wanajeshi watano tunaoweza kuwatuma, wawili ni lazima wawe na mabomu ya Nyuklia. Hawa ndio wanauwezo wa kipekee.” Alijibu Daktari.
“Wanauwezo gani?” Akauliza Waziri Mkuu.
“Angalia hii.” Akamsogezea Ipad. Kisha akabonyeza sehemu ya video na hapo wakaanza kuonekana wanajeshi wakifanyiwa majaribio. Picha ambayo iliwafanya wale mabwana waliokuja pale kushangaa, ni mlipuko mkubwa uliotoka kwenye mwili wa mwanajeshi mmoja, halafu baada ya mlipuko huo, yule mwanajeshi alitoka ndani ya moto akiwa anawaka lakini akitembea bila wasiwasi… Baadae moto huo unazima, na mwanajeshi anaoekana hana makovu yoyote ya moto licha ya nguo zake zote kuungua.
“Hatari sana hii.” Aliongea waziri mkuu huku katabasamu.
“Hiyo ndio C.O.D.EX improved chemical.” Daktari alijigamba kwa mbwembwe.
“Kwa hiyo ni ile C.O.D.EX ya wale wanajeshi wengine?” Aliuliza bwana yule aliyeongozana na Waziri Mkuu.
“Ndio Waziri wangu wa Ulinzi.” Kwa tabasamu pana alijibu Dokta Ice.
“C.O.D.EX ni nini?” Akauliza Waziri Mkuu.
“Ni kifupisho cha maneno haya, CINDREX OLTIVIASO DECA ENDROLINE X. Ni chemikali zilizobuniwa miaka kumi nyuma na walitengenezwa wanajeshi kadhaa ambao walisumbua sana CIA na FBI. Baada ya kujua kemikali hizi, CIA waliweza kuharibu maabara yote ya kutengenezea wanajeshi hawa. Sasa hivi ndio tumepewa kibali cha kutengeneza silaha kupitia kemikali hizi.” Alijibu Daktari.
“Kuna tofauti gani kati ya wanajeshi hawa na wale wa miaka kumi iliyopita? Hawawezi kuleta madhara kama yale?” Aliuliza Waziri wa Ulinzi.
“Hapana. Hawawezi fanya hivyo. Tatizo kubwa la wale waliyopita, hawakuwatoa kumbukumbu wale waliowatengeneza, hivyo ilikuwa rahisi kwa zile kemikali kurudisha kumbukumbu baada ya kuanza kuisha. Hilo likaleta tatizo kwa baadhi ya wanajeshi ambao kumbukumbu ziliwarudia.” Akajibiwa.
“Okay. Kwa hiyo hawa hawana kumbukumbu?” Akauliza tena Waziri wa Ulinzi.
“Ndio. Kabla hatujawaingizia C.O.D.EX, tulihakikisha kwanza tunafuta kumbukumbu zao zote za maisha yaliyopita. Tuna uhakika tumefanikiwa katika hilo.” Alijibiwa na daktari.
Waziri wa Ulinzi akaangaliana na Waziri Mkuu kisha kwa ishara fulani walipeana kuonesha kuwa wamekubaliana na ile kazi ya C.O.D.EX.
“Sawa Dokta. Ila kwanza ni lazima tufanye majaribio na silaha zako.” Waziri wa Ulinzi aliongea na kumpa nafasi dokta naye aongeze jambo kama analo.
“Mmepanga wapi kufanya majaribio yenu?” Akauliza Dokta.
“Iraq na Iran.” Akajibiwa na dokta akaonesha kukubaliana na majibu hayo.
“Ila kuna jambo moja ambalo tumelipandikiza kwenye miili yao.” Akakumbusha daktari.
“Lipi hilo?” Akaulizwa.
“Hawana huruma hata kidogo. Kitendo cha huruma kwao kimepita kushoto. Kwa hiyo hayo majaribio, tujaribu kuyafanya mbali na raia.” Akaongea dokta.
“Hamna shida.” Akajibiwa na Waziri wa Ulinzi kwa kifupi.
Baada ya maongezi hayo marefu, wale viongozi wa serikali ya Marekani, walianza kuondoka eneo lile huku nyuma wakifuatiwa na walinzi wao muhimu kabisa.
****
BAADA YA WIKI MBILI.
Vyombo vya habari duniani vilikuwa vinatangaza kuhusu Iran kuvamiwa na mitambo yake ya nyuklia kuharibiwa vibaya na wakati huo mateka wa Iraq walisemekana kuwa wamekombolewa na wanajeshi wa jeshi la Marekani lakini hawatambuliki ni wapi walipo. Habari zilikuwa zimezagaa na kuzusha maswali kadhaa kwenye vichwa vya habari na watu wote kwa ujumla.
Vyombo vya habari viliuliza kuhusu wanajeshi hao na Waziri Wa Ulinzi alithibitisha uwepo wa wanajeshi hao na kuahidi kuwa, Marekani itakuwa na nguvu kubwa kuliko nchi yoyote duniani.
Wakati hayo yanaendelea, daktari mkuu wa ile maabara alikuwa anatazama na kusikiliza vyombo vya habari kila kukicha. Jambo ambalo hakuwaambia wale viongozi, ni uwezo wa wale wanajeshi kuchukua matukio yote kwenye chipu iliyokuwa imepandikizwa vichwani mwao kwa ajili ya kuwatuma wafanye mambo fulani.
“Wajinga sana hawa. Niliwaambia wasifanye majaribio kwenye makazi ya raia wema. Matokeo yake wamewaua mateka wote. Washenzi sana. Natakiwa kufanya jambo moja muhimu sana kabla sijaondoka hapa.” Alijiwazia Dokta Ice na hapohapo akaifata kompyuta yake iliyokuwa katika ofisi ndogo kwenye chumba chake na kuanza kusoma mambo kadhaa kwenye mafaili yaliyokuwepo kwenye kompyuta hiyo.
Kesho yake ilikuwa Asubuhi ya Jumapili yenye bashasha nyingi sana. Dokta akiwa anajua wazi kabisa kuwa siku hiyo ni ya mapumziko kwake, alitoka ndani ya nyumba yake akiwa kakamata mkoba wenye makaratasi kadhaa, kisha akapanda gari lake la gharama na kuelekea zilipo ofisi zao.
Huko aliamrisha baadhi ya wafanyakazi waondoke kwa sababu alikuwa na kazi nyeti ya kufanya bila wao kuijua. Alipofanikiwa kuwatoa, akafungua jokofu moja ambalo lilikuwa tofauti na yale mengine. Lenyewe lilikuwa halioneshi na lilifanana na lile la kuhifadhia maiti. Alipolifungua, akaonekana muafrika mmoja aliyekuwa kafumba macho yake kama marehemu na mvuke ukimtoka kwa sababu ya kuganda kwa mwili wake.
Ice Mujo, akabofya vitufe kadhaa kwenye lile jokofu nalo likaanza kuvia maji ambayo yalikuwa ya moto. Maji hayo yakayayusha barafu iliyopo mwilini mwa muafrika yule na kumfanya awe laini na mwenye hali ya umoto.
Akabofya tena vitufe kadhaa kwenye ipad yake. Vitu fulani vikatokea angani na kisha vikashuka hadi kwenye lile jokofu. Vikazama ndani ya maji na kumkamata yule bwana, kisha vikatoka naye na kumuweka kwenye lile jokofu lingine ambalo lilikuwa linauwezo wa kujazwa maji pamoja mitambo ya kumuwezesha binadamu kupumua.
Dokta Ice, akambandika vile vifaa vya mapigo ya moyo pamoja na mipira maalumu kwa ajili ya kupumulia. Alipomaliza, akafunga lile jokofu na kufungulia maji yaliyoanza kujaa ndani yake.
Akasogea kwenye kompyuta inayoonesha hali ya yule binadamu muafrika. Akaanza kuruhusu kemikali aina ya C.O.D.EX ianze kuingia mwilini mwa yule bwana. Kilikuwa ni kitendo cha dakika kumi pekee kukamilisha tendo lile na lilifanikiwa kwa sababu muafrika yule alianza kupumua akiwa ndani ya jokofu lile.
Kwa haraka, akabonyeza tena vitufe kwenye kompyuta na hapohapo maji yakaanza kupungua na baada ya kuisha yote, yule bwana alijikuta akisogezwa nyuma kwa kasi na kisogo chake kikagota nyuma ya kidirisha kidogo ambacho kilifunguka na hapohapo mwanga fulani mwekundu ukaanza kupitia sehem hiyo ya kisogoni. Kisogo cha yule bwana kikafunuliwa kidogo kwa kutumia ule mwanga ambao ulitumika kukata sehemu hiyo.
Kiasi kidogo cha ubongo kikatolewa, na baada ya hapo, Dokta Ice alifungua mkoba wake na kutoa Diskette na kuchomeka kwenye sehemu maalumu ya kwenye komyuta aliyokuwa anaitumia. Ikaanza kusoma harakahara na baadaye ikaandika ‘loading succefully, 100%’. Dokta akashusha pumzi na kisha akabofya kitufe cha Enter. Hapo kule kwenye kisogo cha yule bwana, ikapandikizwa chipu na kisha ile ngozi iliyotolewa kisogoni, ikapachikwa na kupitiwa na mwanga ule mwekundu. Pakarudi vilevile.
Yule muafrika akatoka kule alipobananishwa na kusogezwa katikati ya lile jokofu. Dokta akabonyeza tena vitufe kadhaa kwenye kompyuta yake, yule bwana akaanza kuzunguka taratibu kwenye lile jokofu kw a dakika zipazo kumi. Aliposimama, kompyuta ikaongea kwa sauti ya kike, ‘upgrade complete’. Kisha maji yakajazwa ndani ya jokofu na dokta akawa kamaliza kazi ambayo alipanga kuifanya jana yake.
Dakika ishirini mbele, akamtoa mtu yule kwenye jokofu na kumuingiza kwenye mashine nyingine iliyoanza kuupembua mwili wa muafrika yule hadi ikaridhika na kutamka maneno mengine ya kiingereza, ‘Scan Complete’.
Dokta Ice akatabasamu baada ya kufungua mashine ile na yule muafrika kusimama mwenyewe na kumtazama Dokta.
“Nipo tayari kukutumikia mkuu.” Aliongea bwana yule kwa Kiingereza na kumfanya Dokta kuzidi kutabasamu.
ITAENDELEA.