Dam55
JF-Expert Member
- Oct 8, 2015
- 5,592
- 11,831
"A good Lord has only ten" George Clemenceu alisikika akimkosoa Rais wa marekani Woodrow Wilson kwenye mkutano wa Versaille treaty mwaka 1919.
Hii imetokana na Rais wa marekani wa wakati huo Woodrow Wilson kuja na sheria 14 kwenye mkutano huo akiwa kama mwenyekiti.
George kutoka ufaransa alimpinga rais wa marekani baada ya kuweka sheria 14 kandamizi zilizoelekezwa kwa Germany as the war causative wa vita ya kwanza ya dunia.
Alimwambia hata Mungu mwenyewe ana sheria kumi tu sasa iweje wewe uwe na sheria 14 umezitoa wapi?.
Licha ya marekani kuonekana kuwa ni taifa lenye nguvu lakini yeye hakuogopa kumkosoa tena kwa maneno makali.
Ujumbe wangu kwa wanaharakati na watetezi wa wanyonge msiogope kukosoa pale ambapo mnaona kuwa haki haitendeki licha ya sheria kali zilizowekwa kuwazuia.
Mifano ni mingi ya changamoto mnazokumbana nazo lakini kamwe msikate tamaa.
Lakini pia naomba niwakumbushe kuwa msitumie kivuli cha uwanaharakati kujinufaisha kisiasa ama kutetea mambo ambayo si rafiki kwa maendelea ya taifa letu, kamwe msikubali kutumika.
Siku zote simamieni kwenye ukweli huku mkijua kuwa watanzania wanaona kinacho endelea na wameamka katika usingizi na upofu wa muda mrefu.
Sheria kandamizi za mitandao
Mashitaka ya uhujumu uchumi
Mashitaka ya uchochezi
Kuminywa kwa vyombo vya habari
N.k
Haya yote ni mfano wa sheria kama zile za Woodrow Wilson hivyo basi tunawahitaji wakina George wa kizazi hiki kuja kukosoa bila kuogopa kwa masilahi mapana ya taifa letu.
Poleni sana wanaharakati wetu Mungu awatie nguvu kwenye Mapambano yenu.
Note; uwanaharakati sio matusi na kupinga kila lililo jema bali ni kutetea na kusemama upande wa wale wanao onewa kwa sheria kandamizi, matumizi mabaya ya madaraka na kila namna ya unyonyaji.
Hii imetokana na Rais wa marekani wa wakati huo Woodrow Wilson kuja na sheria 14 kwenye mkutano huo akiwa kama mwenyekiti.
George kutoka ufaransa alimpinga rais wa marekani baada ya kuweka sheria 14 kandamizi zilizoelekezwa kwa Germany as the war causative wa vita ya kwanza ya dunia.
Alimwambia hata Mungu mwenyewe ana sheria kumi tu sasa iweje wewe uwe na sheria 14 umezitoa wapi?.
Licha ya marekani kuonekana kuwa ni taifa lenye nguvu lakini yeye hakuogopa kumkosoa tena kwa maneno makali.
Ujumbe wangu kwa wanaharakati na watetezi wa wanyonge msiogope kukosoa pale ambapo mnaona kuwa haki haitendeki licha ya sheria kali zilizowekwa kuwazuia.
Mifano ni mingi ya changamoto mnazokumbana nazo lakini kamwe msikate tamaa.
Lakini pia naomba niwakumbushe kuwa msitumie kivuli cha uwanaharakati kujinufaisha kisiasa ama kutetea mambo ambayo si rafiki kwa maendelea ya taifa letu, kamwe msikubali kutumika.
Siku zote simamieni kwenye ukweli huku mkijua kuwa watanzania wanaona kinacho endelea na wameamka katika usingizi na upofu wa muda mrefu.
Sheria kandamizi za mitandao
Mashitaka ya uhujumu uchumi
Mashitaka ya uchochezi
Kuminywa kwa vyombo vya habari
N.k
Haya yote ni mfano wa sheria kama zile za Woodrow Wilson hivyo basi tunawahitaji wakina George wa kizazi hiki kuja kukosoa bila kuogopa kwa masilahi mapana ya taifa letu.
Poleni sana wanaharakati wetu Mungu awatie nguvu kwenye Mapambano yenu.
Note; uwanaharakati sio matusi na kupinga kila lililo jema bali ni kutetea na kusemama upande wa wale wanao onewa kwa sheria kandamizi, matumizi mabaya ya madaraka na kila namna ya unyonyaji.