9 December 1961 ulikuwa wapi?

Sijazaliwa. Yanini wengine kusema uongo humu au kufanya jokes. Tuwaache wazee waje watupe uhondo hapa.
 
jamani fungukeni zaidi ,mlikuwa wapi?
 
sijazaliwa. Mamangu aliolewa 1977 na 1978 akazaliwa 1st born ( my dada ).. Ngoja nimuulize mamangu alikuwa wapi siku hiyo...
 
Nilikuwa kwenye mifuko miwili inayohang btn two legs na kwenye ovari nikisubiri kurutubishwa ili nitoke na baada ya kutoka ndipo nikawa nafahamika kama handsome wa mama.
 
Mshua alikuwa na miezi tu, maza ndo kabisa hata kufikiriwa tu kuzaliwa hakuna. Sisi wana wa mzee ruksa bwana, haya ngoja tuwapishe wale wa mzee wa kifimbo walonge. Hoping mzee wetu mwandosya atachangia kidogo maana kumbe naye ni memba mwenzetu.
 
Nilikuwepo, kitu nnachokumbuka ni mafashfash na nnakumbuka bendera zilizopambwa barabarani hususan nje ya nyumba yetu, kumbuka nyumbani kwetu ni jirani kabisa na ilipozaliwa TANU na nnakumbuka ngoma iliyopigwa nje ya nyumba yetu usiku kucha nadhani lilikuwa ni gombe sugu, nilikuwa ni mdogo sana kiasi cha kuwa na "vague" memories. Nakumbuka bibi yangu alitupa wote (wajukuu) senti tano tano kama sadaka kwa furaha yake (senti tano siku hizo ilikuwa na tundu kati).

Nikikumbuka mengine ntarudi.
Kama nlikuona vile ukifurahi kupewa pesa yenye tundu katikati ilikuwa inaitwa hela tano, nyingine hela saba n.k.na zilikuwa zimepamba kwa picha ya meno ya tembo hivi. Siku zile neno Uhuru lilikuwa linawashinda kutamka baadhi ya majirani zako na kutamka buluu badala ya uhuru.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom