Zekidon
JF-Expert Member
- May 29, 2013
- 1,903
- 569
- Thread starter
- #21
Wanajf, jaribuni kumwelewa mleta hoja. Huenda anamaanisha yafuatayo:-Wanajf, jaribuni kumwelewa mleta hoja. Huenda anamaanisha yafuatayo:-
- huenda serikali kwa njia moja au nyingine inahusika kutengeneza maskini.
- huenda serikali inahusika kutengeneza wezi wa raslimali za umma.
- huenda serikali imeajiri wezi badala ya watoa huduma ambao ni jamaa zao na inawalinda kuliko inavyolinda raslimali za umma.
- huenda anaiamsha serikali ili kuongeza viwango vya mishahara itakayotosheleza.
- huenda anaiambia serikali iajiri watu kulingana na fani zao na si kwa kujaza nafasi ili iweze kuwadhibiti.
- huenda anaiasa serikali itenge siasa na taaluma ili kuliepusha taifa kukosa maadili na nidhamu ya uwajibikaji.
Asante mleta uzi kwa kuthubutu kuiasa serikali kuepuka na mfumo mbovu wa kuajiri na kulipa mishahara kiduchu pamoja na kuwaumba na kuwalinda wezi wa raslimali zetu.
asante mkuu kwa kunielewa kwa asilimia zote. inasikitisha mno kuona watu wakiamka asubuhi wanawaza kwenda kupiga dili maofisini ili kujaribu kuingiza siku badala ya kwenda kufanya kazi kwa ufanisi. unategemea kwa maisha ya aina hiyo hii nchi itaendelea lini?? never ever. sahau. tutaendelea kukopa mpaka dunia iishe wakati rasilimali tunazo. sad.