Dr Adam Francis
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 703
- 1,143
Katika Kumbukumbu la Torati 30:19, twasoma "Nazishuhudiza mbingu na nchi juu yenu hivi leo, kuwa nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, ili uwe hai, wewe na uzao wako"
Niwazi kuwa Mwenyezi Mungu ametupa uhuru wa kachagua hatima yetu kama mtu mmoja mmoja lakini pia kama Taifa kwa ujumla. Kwahiyo hali yetu ya sasa na ya baadaye inategemea sana tunachagua nini leo.
Sote ni mashahidi wa madhila yaliyotukuta October 29. Kama Taifa tulikata shauri kwa kauli moja kuwa "Never Again" Hata hivyo katika hali isiyokuwa ya kawaida wapo wenzetu wanaoona tuliyoyapitia hayatoshi wanatamani 7/7 tuirudie historia ile ya machungu.
Nina imani tunayo hoja na haja ya kuambiana ukweli. Katika mapambano ya ngangali na ngunguli huwa hakuna mshindi. Haswa haswa tutasababisha vifo, ulemavi, majeruhi, upotevu wa mali na uharibifu wa miundo mbinu.
Nchi yetu ni "work in progress" bado haijakamilika. Tofauti za mitizamo yetu juu ya hali yetu ya sasa na maoni ya nini tufanye kujikwamua sio sababu ya kutufanya tuingie barabarani, bali ni fursa yakutuleta kwenye meza ya mazungumzo.
Serikali imeshaonesha nia thabiti ya kufanya maridhiano. Hiyo ni fursa adhimu ya kujitokeza kusema kero, maoni na ushauri utakaotutoa sehemu moja kwenda nyingine katika njia salama. Rai yangu kwa wananchi wenzangu, 7/7 tuchague kujenga badala ya kubomoa
Niwazi kuwa Mwenyezi Mungu ametupa uhuru wa kachagua hatima yetu kama mtu mmoja mmoja lakini pia kama Taifa kwa ujumla. Kwahiyo hali yetu ya sasa na ya baadaye inategemea sana tunachagua nini leo.
Sote ni mashahidi wa madhila yaliyotukuta October 29. Kama Taifa tulikata shauri kwa kauli moja kuwa "Never Again" Hata hivyo katika hali isiyokuwa ya kawaida wapo wenzetu wanaoona tuliyoyapitia hayatoshi wanatamani 7/7 tuirudie historia ile ya machungu.
Nina imani tunayo hoja na haja ya kuambiana ukweli. Katika mapambano ya ngangali na ngunguli huwa hakuna mshindi. Haswa haswa tutasababisha vifo, ulemavi, majeruhi, upotevu wa mali na uharibifu wa miundo mbinu.
Nchi yetu ni "work in progress" bado haijakamilika. Tofauti za mitizamo yetu juu ya hali yetu ya sasa na maoni ya nini tufanye kujikwamua sio sababu ya kutufanya tuingie barabarani, bali ni fursa yakutuleta kwenye meza ya mazungumzo.
Serikali imeshaonesha nia thabiti ya kufanya maridhiano. Hiyo ni fursa adhimu ya kujitokeza kusema kero, maoni na ushauri utakaotutoa sehemu moja kwenda nyingine katika njia salama. Rai yangu kwa wananchi wenzangu, 7/7 tuchague kujenga badala ya kubomoa