Kwa Tanzania hakuna shirika lenye nidhamu ya juu kama NHIF.
EBD HUMBA amelitumikia shirika kwa uadilifu wa hali ya juu sana. Nadhani ni shirika pekee lisilotumia magari ya ofisi kuchukua na kupeleka wafanyakazi makwao akiwemo Mkurugenzi mkuu. Anasitahiri kuongezewa mda
Either hujui unachokisema au una ajenda ya kumtetea huyu mzee mbinafsi. Ni kweli wakurugenzi wengine hawachukuliwi na magari ila gari lake humchukua yeye, mkewe, linapeleka watoto shule na kadhalika. Nashangaa unasema hata yeye halimchukui.
Kwa wanaosema ni muadilifu ni kwa sababu tu ni shirika ambalo kamwe haliwezi kutetereka kimapato. Huyu mzee hana utu, super arrogant, mfitini na uliza wafanyakazi utaambiwa navyoendekeza majungu. Hupati cheo kirahisi bila kuwa na majungu au una uhusiano, undugu na viongozi wa serikali au yeye mwenyewe. Uliza watu wanavyohamishwa kibwege pale. Uliza vyeo vinavyoundwa bila mpangilio pale ili kuwatengenezea ulaji watu aliokuwa anawataka. NHIF kuna makundi yanayochukiana na kuwindana sana kwa sababu ya huyu mzee, fanya uchunguzi usioelemea upande wowote utaambiwa.
Kukatiziwa kwake mkataba kunaweza kuwa kielelezo cha kuwa hakuwa muadilifu sana kama baadhi ya watu huku wanavyomtetea. Vipi manunuzi yaliyohojiwa na CAG ya mabilioni ya fedha ambayo yeye ana taarifa nayo??
vipi kuhusu kutokuwa na efficient audit committee. Umeona wapi Auditors wanareport kwa CEO badala ya Audit committee.
Nina wasiwasi na wanaomtetea kuwa pengine ni vibaraka wake au hawamjui vizuri. Kazi anasaidiwa na watu ambao ni watendaji, mfuko haukuanzishwa na yeye mwenyewe. Narudia kusema kukatiziwa kwake mkataba GHAFLA kunaweza kueleza hali halisi. Na ana bahati sana kufika hapo alipofika salama.
Kwa ubaya aliowafanyia watu nadhani amelipwa hapa hapa na hajaondoka vizuri. Amelazimishwa kuongezewa mkataba imeshindikana.
Nadhani nisiendelee sana ili nisionekane nina biased opinion kuhusu huyu mzee, "what goes around comes around....it doesnt matter when"