utakuja
JF-Expert Member
- Sep 20, 2010
- 1,062
- 996
Kusema ukweli, kwenye haya maswala ya intaneti— naweza kuwa kati ya wahenga nchini hapa; maana nakumbuka matumizi yangu yalianza mwanzo wa mwaka 2000, nikiwa bado mdogo sana. Enzi hizo nakumbuka tulikuwa tunapata intaneti nyumbani kutoka kwenye simu ya mezani ya TTCL: inayojulikana kama Dial-up internet (ilikuwa inapatikana kwa kuchomeka waya toka kwenye simu kwenda kwenye kompyuta).
Tokea miaka hiyo, nimeshapitia teknologia tofauti tofauti kwa kadri teknologia ya mawasiliano ilivyoboreshwa hapa nchini. Kuna intaneti ya satellite (ambayo ilikuwa kwenye internet café nyingi kubwa nchini), baadae kwenye miaka ya 2005 tulipo anza matumiza ya GPRS kwenye simu zetu za viganjani (tukawa tunapakua magame na nyimbo za kb300 waptrick
), kufatiwa na CDMA ya zantel, EVDO ya Sasatel (Rest in Peace), bila kusahau ukuaji wa Edge na 3g.
Kwa nini nimewarudisha nyuma kidogo? Nimefanya hivi kuwakumbusha tulipo toka na teknologia zote hizo zilivyokuwa; japo chache zilikuwa bora hususani EVDO ya Sasatel ni mfano mzuri wa teknologia ya intaneti iliyokuwa ya kimataifa— lakini hizi nyingine kwa matumizi yangu, kiukweli zilikuwa ni pasua kichwa. Sana sana kwenye haya maswala ya kuangalia video youtube ya dakika 3 tu; inaweza kuload hata dakika 15, au kupakua vitu mtandaoni lazima ukeshe usiku wa saa 8 ndio upate spidi inayoeleweka.
Kwanini nasema 4G ya Vodacom ndio mfano wa kuigwa? Hapa Tanzania teknologia ya 4G japo ilitambulishwa kwanza na Smile, na kufuatiwa na Tigo Tanzania; ndio kina Vodacom na TTCL wakafuatia. Lakini hii mitandao ukitoa Smile, ukiangalia kusema kweli hawakupi 4G ya "kweli". Kwa nini nasema hivi? Turudi nyuma kidogo kwanza tuangalie, mtandao mpaka huwe 3G; unabidi huwe na spidi ya juu (peak speed) ya 7.2Mbps kwa HSPA, 22Mbps kwa HSPA+ au baada ya marekebisho 3.75G hadi 42.2Mbps spidi ya juu. Japo hichi sio kitu cha lazima sana, maana wenye mitandao wanaweza kuita teknologia flani chochote wanachokitaka kwakuwa benchmark za spidi hazijawekwa rasmi kivile.
Lakini spidi za Tigo 4g na TTCL (kwenye hizo screenshot picha ambazo kwenye eneo la mtandao ni blank ni TTCL tena nimefanya hizo speedtest nje ya ofisi zao Samora) ni spidi sawa na 3.75G ya Airtel ya mwaka 2012, iliyokuwa inafika 16Mbps wakati mwingine zaidi— kwa mimi Vodacom ndio wenye 4G ya “kweli” :
Huu mtandao, bila unafiki kwangu mimi ni hatari, iwe usiku wa manane au asubuhi, spidi yake ni ya kasi sana; ukiwa youtube hata ukiweka video ya 4K au 2K haina buffering, Skype au Whatsapp calling hazina tatizo, kupakua movie online usually kwa experience yangu ni chini ya dakika 3.
Sasa ombi langu kwa mitandao mingine, hususani Tigo nyieee... naombeni, sana tena sana mjitafakri upya— sijui nyie kwenu pakoje lakini mitaa ya kwetu Tigo na TTCL ni majanga. Ningependa sana mitandao ya bongo isiwe inapenda kuigana tu kwenye kupandisha bei ya vifurushi, lakini pia kwenye vitu kama hivi vya kuboresha minara yao kufikia kiwango cha Vodacom. Na kwa Vodacom, bei zenu hizo, japo tufikirieni kidogo. Mwisho
Tokea miaka hiyo, nimeshapitia teknologia tofauti tofauti kwa kadri teknologia ya mawasiliano ilivyoboreshwa hapa nchini. Kuna intaneti ya satellite (ambayo ilikuwa kwenye internet café nyingi kubwa nchini), baadae kwenye miaka ya 2005 tulipo anza matumiza ya GPRS kwenye simu zetu za viganjani (tukawa tunapakua magame na nyimbo za kb300 waptrick
), kufatiwa na CDMA ya zantel, EVDO ya Sasatel (Rest in Peace), bila kusahau ukuaji wa Edge na 3g.Kwa nini nimewarudisha nyuma kidogo? Nimefanya hivi kuwakumbusha tulipo toka na teknologia zote hizo zilivyokuwa; japo chache zilikuwa bora hususani EVDO ya Sasatel ni mfano mzuri wa teknologia ya intaneti iliyokuwa ya kimataifa— lakini hizi nyingine kwa matumizi yangu, kiukweli zilikuwa ni pasua kichwa. Sana sana kwenye haya maswala ya kuangalia video youtube ya dakika 3 tu; inaweza kuload hata dakika 15, au kupakua vitu mtandaoni lazima ukeshe usiku wa saa 8 ndio upate spidi inayoeleweka.
Kwanini nasema 4G ya Vodacom ndio mfano wa kuigwa? Hapa Tanzania teknologia ya 4G japo ilitambulishwa kwanza na Smile, na kufuatiwa na Tigo Tanzania; ndio kina Vodacom na TTCL wakafuatia. Lakini hii mitandao ukitoa Smile, ukiangalia kusema kweli hawakupi 4G ya "kweli". Kwa nini nasema hivi? Turudi nyuma kidogo kwanza tuangalie, mtandao mpaka huwe 3G; unabidi huwe na spidi ya juu (peak speed) ya 7.2Mbps kwa HSPA, 22Mbps kwa HSPA+ au baada ya marekebisho 3.75G hadi 42.2Mbps spidi ya juu. Japo hichi sio kitu cha lazima sana, maana wenye mitandao wanaweza kuita teknologia flani chochote wanachokitaka kwakuwa benchmark za spidi hazijawekwa rasmi kivile.
Lakini spidi za Tigo 4g na TTCL (kwenye hizo screenshot picha ambazo kwenye eneo la mtandao ni blank ni TTCL tena nimefanya hizo speedtest nje ya ofisi zao Samora) ni spidi sawa na 3.75G ya Airtel ya mwaka 2012, iliyokuwa inafika 16Mbps wakati mwingine zaidi— kwa mimi Vodacom ndio wenye 4G ya “kweli” :
Huu mtandao, bila unafiki kwangu mimi ni hatari, iwe usiku wa manane au asubuhi, spidi yake ni ya kasi sana; ukiwa youtube hata ukiweka video ya 4K au 2K haina buffering, Skype au Whatsapp calling hazina tatizo, kupakua movie online usually kwa experience yangu ni chini ya dakika 3.
Sasa ombi langu kwa mitandao mingine, hususani Tigo nyieee... naombeni, sana tena sana mjitafakri upya— sijui nyie kwenu pakoje lakini mitaa ya kwetu Tigo na TTCL ni majanga. Ningependa sana mitandao ya bongo isiwe inapenda kuigana tu kwenye kupandisha bei ya vifurushi, lakini pia kwenye vitu kama hivi vya kuboresha minara yao kufikia kiwango cha Vodacom. Na kwa Vodacom, bei zenu hizo, japo tufikirieni kidogo. Mwisho
