21st to remember. Tarehe 21 ya kukumbukwa.. A count down!

21st to remember. Tarehe 21 ya kukumbukwa.. A count down!

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
359,898
Reaction score
828,498
Bwana Humphrey Polepole keshatuandaa vema kumsikiliza leo tar 21. O8. 2025.. Ni tangazo lenye hamasa kwamba litatokea jambo kubwa.. Kwa maneno yake ya siku za nyuma aliwahi kusema wasipomsikiliza basi ataongea ambayo hawatapenda kuyasikia

Kwa tafsiri ya haraka ni kwamba leo tarehe 21. O8.2025 ndio inaweza kuwa siku ya kuizika rasmi CCM ama kuimalizia kabisa kutokana na yale atakayo yaongea
Je ataongea nini? Kuweka ramli chonganishi pembeni ataongea yaleyale ambayo siku zote yaliongelewa chini ya zulia ama kwa sauti ya China
Ataongea yaleyale ambayo hakuna chombo cha habari kilithubutu kuyaandika
Ataongea yale ambayo ccm iliyafanya kushinda chaguzi
Ataongea kuhusu mtandao ndani ya ccm, ambao ndio unaamua nani awe nani kwenye nini
Naamini pia ataongea kuhusu utekaji na watekaji, nani alitekwa alipelekwa wapi na kama yuko hai ama mfu.. Na alikoenda kutupwa ama kuzikwa

Kwa kifupi ataongea mambo mabaya waliyofanyiwa watanganyika chini ya utawala wa ccm! Na kwa vyovyote hayatakuwa na afya kwa chama tawala
Kuna hofu na kuna kejeli pia.. Hofu kwamba nini kitatokea baada ya mazungumzo yake! Kwamba atasababisha mtikisiko mkubwa utakaomaliza enzi za wana mtandao
Kejeli kwamba hana jipya na hakuna kitakachotokea.. Na kwamba akishindwa leo atakuwa amepiga mweleka mkubwa sana na kulipa nguvu zaidi kundi la wana mtandao
Baada ya mazungumzo yake inaweza kujulikana sasa nguvu yake ama walio pamoja naye na nguvu yao.. Ameamua kujivika mabomu ambayo kama hayatalipuka.. Taifa litaingia kwenye ukiwa mkubwa lakini kaka yakilipuka na kukosa upinzani wa uharibifu ndio itakuwa mwanzo wa ukombozi wa Tanganyika!

Yamebaki masaa machache Polepole kutengeneza historia mpya ya shujaa wa Tanganyika!
Tar 21 inaweza kuwa siku kuu Tanganyika.. A day to remember..
Tar 21 August inaweza kuwa siku maarufu zaidi Tanganyika na ikapewa kila aina ya slogan ikiwemo ya A DAY WHEN EVERYTHING WENT WRONG!

Mwezi August ulitabiriwa na watabiri wengi kama mwezi wa mtikisiko mkubwa ndani ya ccm! Tuna utazamia kuuona ukitimia...

Ni leo saa 2 kamili usiku, muda ambao ni wa taarifa za habari macho na masikio yatakuwa kwa Polepole.. Je kuna uhusiano wa kiroho kuhusu hii tarehe na muda aliouchagua!? Wanajimu kwenye hesabu za namba watatuambia.. 21.08.2025 02:00

Kumbukeni Akimaliza Polepole leo tutakuwa na mapumziko ya siku mbili kisha atakuja Gwajima. Ambaye naye ameahidi kuongea mazito na makubwa
Tuupe muda wakati...


View: https://www.facebook.com/share/v/19cuV4g9Qc/
 
Hizi ni biti za mtaka rushwa, apuuzwe Anataka mkate wake.
 
Wiki ijayo tarehe 29/08 vumbi la kampeni litaanza rasmi kutimka.
Hivyo watanzania wamekaa tayari kusikilza sera za vyama 14 ambavyo vitaanza kunadi ilani zao.
Na, Octoba 29 watanzania watatumia haki yao ya kidemokrasia ya kupiga kura.
Hatuna muda wa kumsikiliza kidudu mtu.
 
Wapi nimeandika hivyo ama umekurupuka tu usingizi kwenye ndoto nyevu na kuingia JF?
Nimeamka mda mrefu nisharudi masjid ndugu
Iyo kumzungumzia slow slow inamaanisha nini ? Kwanini msimuongelee mwengine isipokua huyo
 
Anamuuaje Rostam wakati JPM alikuwa anamkubali Hadi kumuarika Ikulu?

Polepole bhana anatakiwa kusikilizwa KWA Panorama ear.
Tuupe muda wakati maana alisema kuna ambayo atayasema ambayo ... "Hata yeye na 'wenzake' walishiriki" kuyafanya! Pengine pia atatengua kitendawili cha kifo cha Magu na wizi wa uchaguzi wa 2020
 
Nimeamka mda mrefu nisharudi masjid ndugu
Iyo kumzungumzia slow slow inamaanisha nini ? Kwanini msimuongelee mwengine isipokua huyo
Hatumuongelei bali nimeweka mada ya kile alichotangaza kukifanya leo na kama umesoma kwa weledi nimeandika kwa mizania kwamba anaweza "kushinda ama kushindwa" soma tena kwa utulivu
 
Wiki ijayo tarehe 29/08 vumbi la kampeni litaanza rasmi kutimka.
Hivyo watanzania wamekaa tayari kusikilza sera za vyama 14 ambavyo vitaanza kunadi ilani zao.
Na, Octoba 29 watanzania watatumia haki yao ya kidemokrasia ya kupiga kura.
Hatuna muda wa kumsikiliza kidudu mtu.
Washindani wakuu wakiwa ni ACT na CHAUMWA!?😂
 
Tuupe muda wakati maana alisema kuna ambayo atayasema ambayo ... "Hata yeye na 'wenzake' walishiriki" kuyafanya! Pengine pia atatengua kitendawili cha kifo cha Magu na wizi wa uchaguzi wa 2020
Kwa namna alivyoongea ni kama ukosoma maneno yake, ni kama anataka kuzungumzia wizi wa uchaguzi CCM.
 
Mshana Jr

Polepole hata aseme Samia na CCM ni mashetani, hakuna Mtanzania atayezingatia....

Watanzania wapo kama nyumbu, wanaifuata hatari na kuangamizwa....

Wakishakuwa kifoni ndio wanatambua kwamba walikabiliwa na hatari, na sasa ni wafu wasioweza kuamka tena...

Mavuguvugu ya kuamsha uhai wa Watanzania yameshafanywa na wanasiasa wengi hapo nyuma tangu Mrema hadi Lissu, lakini wafu hawa wameendelea kulala katika mauti...

Kitu pekee kinachoweza kuleta mabafiliko ni CCM wenyewe huko ndani waamue kubadilika ama kama chama au kikundi fulani chenye nia dhahiri na njema kumeguka...
 
Chadema kwa sasa ni genge la wahalifu wanao ratibu mipango ya kihalifu. tujitenge na hao wahuni tusipata matatizo bureee.
 
Back
Top Bottom