2026 FIFA World Cup - Special Thread

Dah mkuu usinikumbushe tena nilikua najiandaa kwenda kufanya cesarean section ikabidi nisitishe akafanya rafiki yangu. Aisee niliumia sana.
Mechi ya kwanza ya mpira kuumia maumivu makali ni Man U Vs Barca 2010 kama 11 kama sikosei enzi hizo nipo shule ya msingi , napenda Man U kuliko kitu chochote Duniani siku hiyo nilipata tabu sana na ukawa mwanzo wa kumchukia Messi.

Yanga na Mamelodi sikuamini eti mtu mzima nishindwe kulala kisa maumivu ya mpira dah! maumivu yalidumu kama wiki mbili mpaka nikasahau , tokea siku hiyo mpaka leo kama nimeacha hata kuangalia mechi za Yanga . Mpaka Leo haijalishi Yanga anacheza mechi gani hauwezi kunikuta natoa hela yangu kwenda Banda umiza kucheki na kuifuatilia kama zamani .

Sasa maumivu ya mpira sina kabisa baada ya depression nilipunguza kama sio kuacha kabisa ushabiki , sasa nacheki mechi moja Moja tu au michuano muhimu kama burudani tu na sio kama shabiki kindakindaki wa kuumia kama zamani
 
Kumbe wewe ni mkubwa yaani uliumia mwaka 2010?
 
Ndio naangalia hp naaona kweli jamaa alikanyaga vby mguu
nimebishan n wa2 tukio hil
Nmeonekana mjng sn
 
Build up ya goli la tatu kulikuwa kuna faulu ilichezwa ila refa alipeta ni kama walivyolikataa lile la misri baada ya kutokea rabsha kwenye build up ile refa aliiona ila kwa hii ya Argentina refa alijidai hakuona
Na nilivoona kama kipa wa Egypt alikuwa anaiskilizia. Na ndio maana aliloose concentration. Lile goal ange concentrate lisingepita
 
Daah mimi mechi ya Barca na Inter mwaka jana nilishikwa na homa kali sana sikulala usiku. Nikaona ipo siku nitakufa bure
 
Mkuu pole.
Out of Point 2010 ulikuwa bado shule ya msingi?
Inamaana unapishana kidogo umri na first born wangu πŸ˜ƒπŸ˜ƒ
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…