2020 upinzani hautafikisha wabunge 10

2020 upinzani hautafikisha wabunge 10

utaifakwanza

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2013
Posts
14,193
Reaction score
2,815
Kasi ya Dr Magufuli kutatua kero za watanzania, kutumbua majipu yalikuwa yanafaidi keki ya taifa peke yao, kuendelea kuboresha miundombinu ya usafiri, kuziba mianya ya uvujaji wa rasilimali za nchi pamoja kurudisha nidhamu katika utumishi wa umma ni baadhi tu ya makubwa aliyokwisha ifanyia Nchi yake mzalendo huyu.

Ni mwaka mmoja na ushee hivi sasa tangu aikamate Ikulu lakini kazi yake ni sawa na wale waliozeekea mle. Tuendelee kumuunga mkono na sio siri tena kwamba kwa hali hii come 2020 wapinzani kwa ujumla wao wanaweza wapate wabunge wasiozidi 9.

Tutaona.
 
Kuota ni bure.. Haulipii kodi yoyote.. Endelea kuota.
 
Kwani nchi hii tumeisha piga kura za kumpata rais
 
Watanzania hatuwataki tena Hawa wapinzani. Japo CCM ina mapungufu Ila Hawa wapinzani ni matapeli tu wa kisiasa. Tangu rais magufuli ashike nchi tumejua aina ya upinzani tulionao.. Rais magufuli hakuna kuwapa tume huru. 2020 fanya juu chini hata Kwa kuiba kura hakuna Watetez wa wauza ngada kushinda uchaguzi
 
Dah.... Kwa style hii ya Mbowe? Labda aanze kuzikwa yeye kwanza... maana hamjui atakuja kwa gia gani 2020....ukichukulia biashara zake za kifisadi zimebainika... Sijui?
ukawa haibebw na mbowe
Bla mbowe ukawa bdo inazd kuchanja
Mbuga
 
Usamehewe kwa dhambi uitamaniyo!..
 
Uhuru wa demokrasia umebakwa, siasa wataifanyia wapi??? Mkuu Jpm kashapiga marufuku, aruhusu mikutano aone namna wabunge wa upinzani wanavyofanya kazi, watachambua kama karanga '' kale ka wimbo nakapendaga sana ''
 
Hivi mtoa mada siasa unaijua vizuri kwa kifupi siasa ni nchezo mchafu inaweza kukugeuka ndani ya dk 1 angalia ujizaniae umesimama usije kuanguka bado mapema mno.Watu mtaani maisha magumu hakuna mzunguko ukitumia elfu 2 leo kesho hujui unapata wapi .wafanya biashara tumepigwa kodi double price .Wewe hujui kitu unashinda kwenye mitandao kutwa jioni ugali wa shikamoo maisha yanaenda .Time will tell .
 
Watanzania hatuwataki tena Hawa wapinzani. Japo CCM ina mapungufu Ila Hawa wapinzani ni matapeli tu wa kisiasa. Tangu rais magufuli ashike nchi tumejua aina ya upinzani tulionao.. Rais magufuli hakuna kuwapa tume huru. 2020 fanya juu chini hata Kwa kuiba kura hakuna Watetez wa wauza ngada kushinda uchaguzi
We utakuwa ujielew wew walazimisha tutoe matus mm n mtanzania nan kakwambia siwataki wapinzan.jisemee wewe binafs sio kugeneralize .et watz..mfyuuuuuuuuu.
 
Back
Top Bottom