platozoom
JF-Expert Member
- Jan 24, 2012
- 9,548
- 11,517
Hata Dems kulikuwa na makandokando yake. Naamini hujasahau emails za Wakubwa wa Dem zikimpendelea Hillary.platozoom, kumbuka kwenye primary mtu yeyote anaweza kupiga kura hata wasio wanachama. Yawezekana waliokuwa wanampigia kura hawakuwa hata GOP ila walitaka apite wapate mteremko.
Hata huko kwa DEMS mambo yalikuwa hayo hayo. Wengi waliompigia Sanders hawakuwa wanachama. Bahati nzuri au mbaya viongozi wa DEMS walikuwa wajanja.
Kama Trump angekuwa hovyo kabisa tusingeona Polls za tofauti ya asilimia mbili au tatu au wakati mwingine neck to neck.
Hata kama Trump atashindwa lakini kuna ujumbe mahsusi umeonekana. Kwa nyakati za nyuma Mtu mropokaji kama Trump asingepata hata upenyo kidogo, kumbuka ile kauli ya Mit Romney ilivyomgharimu kwenye uchaguzi.
Lakini pamoja na kauli tata za Trump kuanzia primaries lakini bado anadunda. Maana yake rahisi, wengi sana wamechoka na the establisment.
