2015: Tunahitaji Rais mwenye UWEZO!

Rais awe kijana.Wazee wengi wa Tanzania wana mawazo mgando.
Kwa mfano, umoja/baraza la vijana, wanawake, wazazi ... haya yote ni mawazo ya nani? Nani aliamua miundo hii ya vyama?
So, obsolete!!! kila chama kinafuata miundo ya kizamani sana.
UKITAKA KUFANYA KITU UNAAMBIWA WAZEE WA CHAMA WAMEKATAA.
Ni wakati muafaka wazee wakae pembeni, hakuna mzee mwanasiasa mwenye jambo jipya, wote walikuwa kwenye system na wameshaharibu. Wakae pembeni.
 
Siyo vijana tu wanaonyanyua vyuma. Tembeleeni gym halafu muingie weight room muone jinsi kulivyo na mchanganyiko wa ma rika tofauti.

Hata vibibi vinabeba vyuma. Vibabu ndo usipime kabisa.
 

Nani huyo kijana unayetaka awe rais?
 
Mimi naamini hata umri wa kikomo ni muhimu, kuna mahali nilisikia mwalimu wakati anang'atuka watu walishaanza kumuita hambiliki (hashauriki) na alikuwa mkali kwa kuitwa jina hili.

Unafikiri alikuwa anaitwa "haambiliki" kwa sababu ya uzee? Unajua Nyerere aliacha Urais akiwa na miaka mingapi? Kukupa taarifa tu alikuwa na miaka 63. Michael Sata wa Zambia ana miaka 74, Mwai Kibaki 80, Truman alipoapishwa alikuwa 60 na Regan 69!!! think about it.. Rais kijana Marekani kuapishwa alikuwa ni T. Roosevelt akiwa na miaka 42 na mzee zaidi akiwa ni Regan! Marekani kwa miaka yote na marais 44 imewahi kuwa na marais 2 waliokuwa chini ya miaka 45!! And its doing just fine.
 

Unafikiri hawa wazee waliibuka tu wakiwa na mvi? unawaona wazee waliingia na kupewa nafasi mbalimbali wakiwa vijana!! Wote unaowaita wazee leo ukirudi kati ya 1964-1972 walipoingizwa kwenye utumishi wa umma wengi walikuwa ndio "vijana" wa wakati huo!!! Kwanini unafikiri vijana wa "sasa" watakuwa na tofauti?
 
Mwanakijiji,

Je ni kwa vile tu kijana wa Kigoma inaonekana ameamua na katangaza nia "mapema"?
 

Mimi nakubaliana kabisa na unachosema ila mwanakijiji hamaniishi hivyo, yupo kwenye kampeni! soma maneno ya mwanakijiji hapa nanukuu "Unafikiri alikuwa anaitwa "haambiliki" kwa sababu ya uzee? Unajua Nyerere aliacha Urais akiwa na miaka mingapi? Kukupa taarifa tu alikuwa na miaka 63. Michael Sata wa Zambia ana miaka 74, Mwai Kibaki 80, Truman alipoapishwa alikuwa 60 na Regan 69!!! think about it.. Rais kijana Marekani kuapishwa alikuwa ni T. Roosevelt akiwa na miaka 42 na mzee zaidi akiwa ni Regan! Marekani kwa miaka yote na marais 44 imewahi kuwa na marais 2 waliokuwa chini ya miaka 45!! And its doing just fine."

Chama

Gongo la mboto DSM
 

Mkuu Chama, nadhani umeona alivyoelezea alichomaanisha hapa. Na ndio maana jana nikaomba umuulize akueleweshe.


Nukuu ya Mwanakijiji hapo juu inapingana na hicho ulichosema kwenye wekundu.
Binafsi sioni kama kuna kampeni yeyote hapo.

Labda unieleweshe vizuri.
 
Bob Lee Swagger;
Jifunze kusoma riwaya ndipo utaelewa maandiko ya mwanakijiji; mbona haji yeye mwenyewe kukanusha?

Chama
Gongo la mboto DSM
 
Bob Lee Swagger;
Jifunze kusoma riwaya ndipo utaelewa maandiko ya mwanakijiji; mbona haji yeye mwenyewe kukanusha?

Chama
Gongo la mboto DSM

hahahaha hahahahah umenifurahisha mkuu.
Asante sana, ninachukua ushauri wako.
 

Huo uwezo tutaupimaje, kwa maneno jukwaani au kwa rekodi ya mtu kiutendaji? Kumbuka hata JK tulimjaribu bila rekodi yoyote na matokeo yake tumeyaona.

Mzee mwenzangu, nina wasiwasi unampigia ndogo ndogo EL kiaina?
 
hahahaha hahahahah umenifurahisha mkuu.
Asante sana, ninachukua ushauri wako.

Bob Lee Swagger
Mimi nakubaliana na wewe 100%; uliachoandika kipo wazi na hakina mjadala ila mwanakijiji ameandika riwaya na ndio sababu hawezi kukanusha

Chama
Gongo la mboto DSM
 

Umri wa watu wa kizazi cha Nyerere ni vigumu sana kuutaja kwa uhakika, wengi wao walikuwa wanakadiria tu, kama baba/ mama yangu aliniambia nilizaliwa wakati mjerumani anajenga reli ya kati imefika hapa zuzu. Au wakati wa mafuriko fulani au njaa fulani iliyoweka record zama hizo. Anyway tukiachana na hilo mbona awali watu walimpa Mwl majina kama musa, mchonga n.k lakini mwisho wa siku akaishia kuitwa haambiliki na kwa maneno yake mwenyewe haya majina mengine aliyakubali tena kwa kutoa sababu za kuyakubali. Lakini hili la haambiliki hili akasema nitamfunga mtu. So ubishi na kutokushaurika vilikuwa ni sifa za Nyerere alipo fikia umri wa uzeeni. Narudi palepale, kama kilivyo kigezo cha umri wa ruksa ya mwanzo wa kugombea lazima na umri wa ukomo wa kugombea urais wa tz uweke kikatiba.Kama sisi ni taifa la watu makini.

Naona umetoa mifano ya umri wa marais wa usa, zambia, kenya, mimi sioni tatizo kama tutaweka kigezo cha ukomo wa umri wa kugombea halfu hawa nao wakaja kujifunza kwetu, tunatakiwa kujiami tu imekuwa ni kasumba sasa kuwa kila jambo lazima kwanza tuangalie wazungu wamefanya nini tunaiga hata yanayohitaji kutumia busra zetu, tena busara kidogo tu.
 

Afande hapo bolded and red, mbona hizo ukitaka kama vigezo utapewa sana tu, tena wasanii na matapele wa kisiasa ndio watakumaliza nazo kabisa tatizo la watz ni kuwa wasahaulifu sana si juzi tu hapa tulizisikia vision na mission tena kwa mbwembwe zote kiko wapi sasa?
 
Easy,
Mazingira waliyokulia wazee wetu si sawa na mazingira waliyokulia vijana wa sasa hivi.
 
Ndugu zangu watanzania, hii tabia ya kuchagua watu ili mradi tu kujaza nafasi tuhakikishe haijirudii tena 2015. Hivi kweli watanzania tutaendelea kuishi kwa ahadi hewa za "maisha bora kwa kila mtanzania" huku rasrimali zetu zikiporwa na wageni hadi lini? huu wimbo wa nchi yetu ni changa na masikini unachusha! Miaka 50 ya uhuru tuliyosherehekea kwa kuonyeshana zana hafifu za kivita ambazo hatujatengeneza wenyewe huku viongozi wakizuga kwamba wanajipanga, wanajifunza na bado wako kwenye mchakato isiyoisha! Tusifanye tena mzaha 2015.
 
kwaushauri wangu naomba tukuchague wewe vipi waweza kutukomboa???
 
Hii ni kazi yetu wote. Anzia pale ulipo kumwaga elimu ya uraia, umuhimu wa kujiandikisha na kupiga kura. LAKINI UJUE CHAMA CHA MABWE NI JANGA LA TAIFA. Kwa pamoja tutafika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…