2015: Tunahitaji Rais mwenye UWEZO!

Mzee MMM,

Naungana na wewe issue hapa si kuwa watZ wanahitaji kijana, Vijana wana nafasi yao na sisi tunahitaji rais ambaye atakuwa ni msafi kwa maana ya hana makundi wala harufu ya Rushwa na actualy waTZ au Chama chake kinaona anafaa.

Hatutaki Rais anataka urais kwa udi na uvumba, Rais anayetakka kuwa rais, bali Rais ambaye watu wanaona anafaa.

Mfano, Dk Slaa hata Ubunge hakuwahi kupigania, na wala hata kwenye kampeni hakuwa anatoa machozi wala kupiga magoti ili achaguliwe, bali alikuwa anawaambia atafanya nini endapo watamchagua kuwa Mbunge wao. Na kwa wanaokumbuka hata 2000 wakati wa uchaguzi aliwaambia wanchi wa jimbo lake kama hawatawachagua madiwani wa chama chake basi itakuwa haina maana yeye kuchaguliwa kuwa mbunge kwa sababu mambo mengi yanayohusu wananchi yako katika nganzi ya Halimashauri.

Tunakumbuka jinsi 2010 alivyishawishiwa kugombea lakini hakutaka kugombania urais ndani ya chama chake, shinikizo lilipozidi kutoka humu JF, Wasomi mbali mbali na wananchi wa Kawaida ndiyo Kamati kuu ya chadema ilipoona anafaa kugombea na kmwomba kugombea.

WaTZ ni mashahidi jinsi alivyopewa Kura nyingi na katiaka kuhujumu matokeo yale hata huyu Zito anayetaka Urais kila kikicha alikuwepo nadhani mnakumbuka gazeti la mwanahalisi liliripoti mawasiliano ya moja kwa moja kati ya wakuu wa TISS na Zito katika kuchakachua na kuhakikisha anagawa CDM katika msimamo wa kutotambua Urais wa JK

Ni bora mtu mwingine aonekane anafaa kutikoni Zito kwani amepwaya sehemu nyingi sana.
 
diector 1
thinking zako kwa zitto zinaonekana una chuki za kupindikua na zitto. Pendekeza hao waezee wako tuwaone kama hatutashuhudia ukimpendekeza el. Acha uchonganishi.

zitto hatakuwa raisi wa nchi hii hawezi na hafai .full stop
 
hivi ni rais gani mnayemzungumzia ? rais wa JF ama TFF . samahani mimi ni mgeni maeneo haya.
 
Mwl. Nyerere alishasema tumuogope sana mtu anataka kukimbilia IKULU, alisistiza Ikulu hakuna biashara, akasema
tena tumuogope mtu huyo kama UKOMA, ZITTO ni UKOMA namuogopa....
.. inategemea na mazingira husiki, mathalani mtu kupata utajiri wa ghafla (kununuliwa) na kunza kugombea uraisi. kuna watu wamestruggle kuleta maendeleo majimboni mwao, na hata michango yao bungeni ina "MASHISKO" mie sina pingamizi nao juu ya urais. isitoshe mtu kuweka nia mapema inatupa wasaa wa kukupembua ipasavyo mbali nakua unatimiza haki yako kidemakrasia. .... kwahiyo mitizamo yenu juu ya ZITO ni mizuri kwasababu ina jazia HEKIMA katika kumtathmini mtu ( kwa mazuri na mabaya yake). Mie binafsi, naona ZITO ni MCHAPAKAZI mzuri sana, ningekuwa Central Commitee ya Chadema, (CC) ninge mptisha nakumpigia debe
 
Zitto kanunuliwa vipi unampitisha kuwa mgombea wa URAHISSI katika nch ya Kigoma?
 
Hold on a second; kama ningetaka kumzungumzia Zitto ningemzungumzia Zitto. Mada yangu iko wazi kabisa; hatuhitaji Rais mzee au kijana, hatuhitaji Mkristu au Muislamu, hatuhitaji Mdigo au Mchagga, hatuhitaji tu yeyote isipokuwa mwenye uwezo. Hili si gumu sana kulielewa. Sitaki Rais atajwe kuwa ni "Rais Kijana" as if ujana wake unahusiana kwa namna yoyote na Urais wake! Kama kuna mtu ana hoja ya kutaka kuwa Rais wa Tanzania aitoe SIMPLY and ABSOLUTELY on merit ya uwezo wake tu. Si kwa sababu "ni kijana" au "ni mzee" au ni "Mkristu" au ni "Muislamu"...

Labda inabidi niwe natafuna kabisa kabla wengine hawajaanza kusoma nisichoandika.
 
kWA HAYA MAANDIKO YOTE KAMA INGEKUWA NI MTU WA KUJIFUNZA ANGEJIFUNZA SIKU NYINGI
 
Weledi hauturuhusu tena kujaribu (trial) kwenye sanduku la kura. Hatuna fursa na wala hatuhitaji kujaribisha hasa kwa vigezo vyepesi vyenye mvuto wa pipi. Kwa nafasi zote kuanzia udiwani, ubunge mpaka urais ni lazima Watanzania tuwe makini sana na werevu 2015.

Tunataka mtu ambaye hatatumia miaka 4-5 "kujifunza" ili eti tuje tumpe miaka mingine mitano ya kurekebisha na kufanyia kazi aliyojifunza. Urais sio shule wala theatre, urais ni kazi na matokeo.

Of coz JK kaashusha sana hadhi ya taasisi ya Urais ndio maana kila mtu anaona anaweza kuwa rais.

MM naunga mkono hoja 100%
 
Mnapenda ligi kweli. Kwamba kuna vijana wenye uwezo wa kuwa Rais Tanzania hilo sipingi....However,We dont give a damn about if the president is young or old.
All Tanzania need is a good man who is not afraid to step on toes and of course with a clear focus.

Tusitumie nguvu nyingi,let Tanzanians decide!
 
ikulu kuna biashara gani? ikulu ni mzigo cyo mahala pa kukimblia.......Nyerere( 1995)
 

...Mie mgeni mitaa hii, kwani King Cobra ana mafanikio gani zaidi ya kuwa Rais wa Zambia?au kwa sababu sasa amekuwa Rais na yeye, ndugu na rafiki zake sasa wanakula maisha kwa gharama za Wazambia?..http://www.zambianwatchdog.com/2012/06/20/more-question-satas-delegation-of-relatives/


...King Cobra so far ni walewale...http://www.newsdzezimbabwe.co.uk/2012/06/sata-attacked-as-he-leaves-for-london.html
 
Ikulu kuna biashara gani? Ikulu cyo mahala pa kukimbilia...............nyerere(1995)
 
Haya mambo sijui sasa yanaelekea wapi sasa!
Kuna kundi tuliambiwa tukiliwezesha linaweza...ina maana haliwezi lenyewe hadi liwezeshwe? matokeo yake kweli tukaamua "kuliwezesha" kila kona na kila nyanja...

Wakati wa kuchagua spika pia kigezo hicho kikatumika...matokeo yake ndo haya tunayoyaona leo.
 
Mtu smart hawezi kuhusisha uongozi na umri,wala uongozi na dini,wala uongozi na anakotokea,wala uongozi na anachomiliki,bali namna anavyoweza kukabiliana na changamoto,urais na pahala panapohitaji uelewa wa juu,hekima ya kipekee,busara ya kipekee,a real comitted one,uadilifu usiotiwa shaka,upendo kwa waliokutuma i.e voters,uzalendo wa kweli,mtu mwenye uwezo wa kubuni namna na njia za kutukomboa kiuchumi n.k na akasimamia,uwezo huu definitely hautokani na anapoishi sasa,hautokani na dini yake,haupatikani ktk kabila lake bali kwa mtu mwenye sifa ya kuwa rais,na obviously mtu huyu huwa hajioni kuwa yeye ndiye bali wanakuwa naye ktk harakati mbalimbali,hajitangazi bali mwenendo na sifa zake humtangaza,hivyo tutambue kuwa muda pia ni kigezo kitachotupa mtu mwenye sifa na weledi watz tuutakao.
 

yeah, king cobra namkubali. 2005 jk alivyoingia kwa madaraka si walisema ni kijana! nini kafanya hadi sasa?
 


tukiwa na katiba safi hata mwehu anaweza kuwa Rais na tusi athirike sana...

tazama Philipines...kuna muigizaji maarufu alikuwa anaitwa Estrada akafanikiwa kuwa Rais..
sheria na katiba zikamtimua hadi jela.....

na aliemrithi nae alipoleta uhuni..
leo yupo kizimbani.....

ishu hapa ni katiba sahihi na sheria nzuri tu baasi
 

Mbona maneno makali? "vijana wenye uwezo" na "wazee wenye uwezo" wote wapo Tanzania. Kama vile wapo Kina "mama wenye uwezo" na kina Baba wenye uwezo" au "Wasukuma wenye uwezo" au "Wandengereko wenye uwezo". Kwanini tusijikite tu kwa wenye "uwezo". Yeyote mwenye kuamini kuwa ana uwezo apewe nafasi yake na ajitokeze pasi ya shaka bila kutuchombezea vitu vingine irrelevant. Ujana, uzee, kabila au jinsia havina sababu kabisa ya kuingizwa katika mjadala wa Rais au viongozi wetu. Sivyo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…