2015: CCM kuwa na mgombea, si Rais mtarajiwa

2015: CCM kuwa na mgombea, si Rais mtarajiwa

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Huu mwaka ni wa tofauti. Ni mwaka wa kipekee wa kiuchaguzi. Tangu demokrasia ya vyama vingi ianze mwaka 1992 na uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi hapo 1995, CCM haikuwahi kuwa kwenye mgagaziko kama mwaka huu. 2015 ni kiboko. Hadi sasa, chama chetu pendwa hakina mgombea wa Urais. Ni jambo dogo lakini linalostaajabisha.Haijawahi kutokea. Ni jambo la kuingizwa kwenye kitabu cha Guiness.

Ndani ya CCM,kumetamalaki makundi. Ni kitu cha kawaida chamani. Ndani ya chama wasiotakiwa wanajitakisha kwa nguvu;wanaotakiwa hawataki. Wanaotaka hawana nguvu-ya kifedha na kiushawishi. Patashika nguo kuhanika chamani. Ni mara ya kwanza Tanzania itashuhudia chama tawala-CCM kikiwa na mgombea wa Urais badala ya Rais mtarajiwa. Haijawahi kutokea CCM kuogopa na kuchelewa kumwanika mgombea wake.

Kwa niliyoyashuhudia kanda ya kusini (Lindi, Mtwara na Ruvuma),kanda ya mashariki (Dar es Salaam,Pwani na Morogoro) na sasa kanda ya kaskazini (Tanga, Klmanjaro, Arusha na Manyara), sihofu wala kusita kusema kuwa CCM itakuwa kwenye uzani sawa na wapinzani kwenye mbio za Urais,Ubunge na Udiwani. CCM haitatisha na kuonekana imeshashinda mahali au nafasi fulani.Never!

Nitakapokwenda Dodoma kwenye vikao vya kichama,nitajipa muda wa kuidurusu kanda ya kati (Singida na Dodoma). baadaye kanda ya ziwa na kanda nyinginezo. Nasema tena,ni kwa mara ya kwanza katika historia ya siasa za Tanzania, CCM itakuwa na mgombea wa Urais badala ya Rais mtarajiwa. Mambo yamebadilika!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha)
 
Huu mwaka ni wa tofauti. Ni mwaka wa kipekee wa kiuchaguzi. Tangu demokrasia ya vyama vingi ianze mwaka 1992 na uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi hapo 1995, CCM haikuwahi kuwa kwenye mgagaziko kama mwaka huu. 2015 ni kiboko. Hadi sasa, chama chetu pendwa hakina mgombea wa Urais. Ni jambo dogo lakini linalostaajabisha.Haijawahi kutokea. Ni jambo la kuingizwa kwenye kitabu cha Guiness.

Ndani ya CCM,kumetamalaki makundi. Ni kitu cha kawaida chamani. Ndani ya chama wasiotakiwa wanajitakisha kwa nguvu;wanaotakiwa hawataki. Wanaotaka hawana nguvu-ya kifedha na kiushawishi. Patashika nguo kuhanika chamani. Ni mara ya kwanza Tanzania itashuhudia chama tawala-CCM kikiwa na mgombea wa Urais badala ya Rais mtarajiwa. Haijawahi kutokea CCM kuogopa na kuchelewa kumwanika mgombea wake.

Kwa niliyoyashuhudia kanda ya kusini (Lindi, Mtwara na Ruvuma),kanda ya mashariki (Dar es Salaam,Pwani na Morogoro) na sasa kanda ya kaskazini (Tanga, Klmanjaro, Arusha na Manyara), sihofu wala kusita kusema kuwa CCM itakuwa kwenye uzani sawa na wapinzani kwenye mbio za Urais,Ubunge na Udiwani. CCM haitatisha na kuonekana imeshashinda mahali au nafasi fulani.Never!

Nitakapokwenda Dodoma kwenye vikao vya kichama,nitajipa muda wa kuidurusu kanda ya kati (Singida na Dodoma). baadaye kanda ya ziwa na kanda nyinginezo. Nasema tena,ni kwa mara ya kwanza katika historia ya siasa za Tanzania, CCM itakuwa na mgombea wa Urais badala ya Rais mtarajiwa. Mambo yamebadilika!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha)

Hata Kama itaonekana ni ujumbe toka mtaa wa ufipa Kinondoni, lakini Una mantiki nzuri na yenye ukweli.
 
Hakika ni mwaka wa mabadiliko....mungu atupe pumzi tushuhudie
 
Hadi sasa, chama chetu pendwa hakina mgombea wa Urais. Ni jambo dogo lakini linalostaajabisha.Haijawahi kutokea. Ni jambo la kuingizwa kwenye kitabu cha Guiness.

Mkuu analysis yako ni nzuri. Hata hivyo kutokuhangaika kumteua mgombea si kwa sababu chama kinashinikiza kura ya maoni kwanza ili rais aliyepo aongoze nchi kipingi cha mpito? Si ulimsikia Pinda akisema kura ya maoni ni mara baada ya kumaliza kuandikisha daftari la wapiga kura!
 
Kwa sasa Arusha Mzee wangu unapiga kampeni huko?Mbona hata huko mtaweka mgombea lakini hatakuwa Mbunge,unasemaje?

Tatizo la hiki chama kiteule ni Wote KAMBARE maana hata ukiwasafisha bado watarudi kwenye TOPE maana ASILI ya KAMBARE NI TOPE.............

Binti yangu Tetty, kila kata, jimbo na hadi Taifa,CCM itasimamisha mgombea.Kwa hapa Arusha Mjini,tungekuwa wajanja na kuponya pesa na hisa,tusingeimamisha mgombea. Lema hakabiki. Hoja yangu ni kuwa uchaguzi huu ni 50/50

Mzee Tupatupa
 
Last edited by a moderator:
UKAWA hao Mkuu. Kwanini UKAWA wakae kimya kumtaja mgombea wao? Wanakera sana

Mzee Tupatupa

Tunasubiri muanze nyie CHAMA KIKONGWE..Maana hata kwenye familia mkubwa anatangulia kuoa au kuolewa..Na ikitokea mdogo kaoa au kuolewa basi lazima itangulizwe ADHABU kwa muoaji ili apewe mkubwa kwa kuvunjiwa HESHIMA ya ukubwa yaweza kuwa KONDOO au MBUZI........Sasa sisi tunafuata miiko na tamaduni za KIAFRIKA MKUBWA ANZA KWANZA KUTAJA MWALI WAKO..........
 
CCM ipo ktk wakati mgumu pengine kuliko nyakati zote ktk historia ya siasa za nchi hii....

CCM haina wasi wasi kwani wanajua priorities za UKAWA sio strategic; as long as Lubuva na tume yake wataendelea kusimamia uchaguzi there is no waya UKAWA watawashinda ccm!!! UKAWA should wake up from their slumber and demand TUME HURU YA UCHAGUZI.
 
Binti yangu Tetty, kila kata, jimbo na hadi Taifa,CCM itasimamisha mgombea.Kwa hapa Arusha Mjini,tungekuwa wajanja na kuponya pesa na hisa,tusingeimamisha mgombea. Lema hakabiki. Hoja yangu ni kuwa uchaguzi huu ni 50/50

Mzee Tupatupa

Na Mzee Tupatupa,refer akiwa fair na mchezo ukawa fair play basi Simba lazima amfunge yanga mabao kadhaa.Sawa nimekuelewa,ila mweleze refer kuwa tunahitaji mcheza mzuri wa haki........Mpira dakika 90
 
Mwaka huu zamu yenu kuanza. Tajeni!

Mzee Tupatupa

Mzee Tupatupa,ungekuwa kwetu MACHAME ungepigwa FAINI,wewe ni mkubwa taja tu MWALI WAKO tumjue ili tuinywe mbege yake kwanza...........
 
Na Mzee Tupatupa,refer akiwa fair na mchezo ukawa fair play basi Simba lazima amfunge yanga mabao kadhaa.Sawa nimekuelewa,ila mweleze refer kuwa tunahitaji mcheza mzuri wa haki........Mpira dakika 90
Tetty,hilo limuhusulo refa haliwezekani.Jiandaeni kulinda haki yenu tu.Maroroso hayatakosekana.

Mzee Tupatupa
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom