200billion kukodi madaktri ni sahihi

Kweli majebere unatumia pudendal nerve kufikiria!
 
Last edited by a moderator:
Kwa kawaida mtu akifikia mwisho wa kufikiri huishia kusema: sasa basi liwalo na liwe (the point of no return) hufuatia na maamuzi ya ajabu sana. unauza usafiri wako ukitegemea lift ya jirani!
 
Tanzania Daima ni gazeti la Udaku sio la kulifuata kabisa.
 
Bilioni 200 haitoshi kuwalipa madaktari ule mshahara wa milioni tatu na nusu wanazodai.inatakiwa matrioni ya pesa na hayapo.
 

Wewe ndipo upo nyuma ya muda, hiyo MNH unayoisema hafai, huduma duni yaani heri hata ukaenda kwa mganga wa kienyeji kama nyuzi za kushonea mama mja mzito anayetaka kufanyiwa operation hakuna!!!!

Endea kulala tu.
 
Kama nchi nzima hamna ct scan ambayo cost yake ni chini zaidi ya shangingi! Maj u r out of ur mind!
 
watanzania bwana kwa kulalamika tu hawajambo! chukueni hatua sio kila siku kwenye mitandao mnajadili then mnaishia kunyamaza .....mbona wenzenu wa misri tunisia na kwingineko wameweza.......acheni maneno kama wanasiasa wenu wake up and take action......
 
Na serikali haiwezi kuacha kutafuta njia mbadala ya kuhakikisha wagonjwa wanapata huduma kwa sasa wakati madaktari hawajachoka kugoma.tena ikibidi waingie mkataba na makampuni yenye mahosptali huko india ili waendeshe hospital zetu za rufaa.
 


Kwanza hii ni porojo tu ya mkuu ambaye amekubuhu na kutukuka kwa uongo. Wote mnakumbuka muda kiasi gani ulipita kabla madakatari kutoka jeshini kufika Muhimbili awamu ya kwanza ya mgomo. Hivyo unaposema kuwa wagonjwa watibiwe, swali ni lini? Vilevile, tusidanganyane duniani hakuna nchi yenye ziada ya madaktari.

Tatu hii inaonyesha kuwa serikali haitaki tu kuwapa madaktari wetu malipo ya kukidhi mahitaji lakini uwezo inao kama inavyoainishwa hapa chini:

Kama serikali ingetumia busara kidogo tu na kuwaajiri hawa sawa na wanataaluma kutokana na unyeti wa kazi zao kwa uhai wa Watanzania wangeweza kabisa kuwapa mshahara wa TZS 3,500,000/=. Hata kama ingekuwa pungufu ya hapo lakini sio laki tisa.

Ina maana kuwa class mate wako aliyebaki MUHAS akaajiriwa kama mhadhiri msaidizi na wewe unayeajiriwa kuwa Daktari kule Ikwiriri tayari mnapishana kwa zaidi ya laki tano. Ikiwa tuna madaktari (MD) wasiozidi 2,500 malipo yao yanawezekana kabisa. Kwani unadhani zinahitajika fedha kiasi gani?

Mbona serikali haisemi? Kwa taarifa yako kama kwa wastani kila daktari angelipwa 7,000,000/= (mara mbili ya madai yao maana kuna masinia) basi kwa mwezi serikali ingetumia TZS bilioni 17.5 sawa bilioni 210 (inalingana na pesa ambayo serikali imeamua kukodi madaktari toka nje) kwa mwaka ambayo ni sehemu ndogo sana ya posho za vikao (sitting allowance) serikalini, kwenye mashirika ya umma na serikali za mitaa.

Nina uhakika kuwa malipo halisi yatakuwa pungufu ya haya na yanawezekana. Hii ingeonyesha jinsi serikali ilivyo makini na inavyojali uhai wa Watanzania lakini sasa imeonyesha kinyume chake ndio maana haijali kuona mtu ameuwawa, uhai kwa serikali hii si kitu cha thamani hata kidogo.

Je, ni mambo mangapi ya kipuuzi yanayofanywa kwa kutumia fedha nyingi za taifa zaidi ya hizi? Yana umuhimu gani kwetu kama Watanzania?

Ukweli ni kuwa tu serikali haitaki na kunapokuwa na watu kama wewe ambaye unaiunga mkono wanafarijika sana maana wajinga ndio waliwao. Hivi kweli ukiwa mgonjwa ukatibiwa na daktari ambaye hajaridhika unadhani utapata huduma inayotakiwa? Walazimisheni, wafukuzeni na muwajengee chuki madaktari; matunda yake sote tutafaidi.

"Mungu hadhihakiwi, kwa maana apandacho mtu ndicho atakachovuna"; na kwa nchi au utawala ni hivyo hivyo.
 
Priority ndio udhaifu wa serikali hii, you buy 30 shangingi instead of 30 ct scanners!
 

Ni kweli mkuu, ndiyo maana hata kile cha MNH ni Phillips kumbe ni bei chee, na ni kibovu kwa muda wa miezi saba hakifanyi kazi lakini Regency hospital kinafanya kazi bila shida.
 
Chama changu lazima kinapepo mbaya sana, hakika tumelogwa na tumewapa uongozi mataahila!

Bora tu niwahi kanisani maana kwa upuuzi kama huu naweza nikaharibu sabato kwa udhaifu wa serikali.
WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI.
 
Hii habari inaweza kukanushwa na Serikali leo au kesho au wanaweza kusema wamenukuliwa vibaya.
 
Huyo ndiye JK na vipaumbele vyake! Mtu yeyote mwenye akili hawezi kuelewa hilo, unless unawaza kimagambamagamba!
Kweli ushindwe kutatua matatizo ya wananchi lakini uwe na resources za kuwakomoa madaktari? Sasa naamini Ulimboka ameteswa na serikali
 
200bil nje ya bajet? serikali inahela nyingi sana na huu ni ushahidi
 
dah yaani sisi tumerogwa na aliyeturoga amekufa hakuna wa kutegua tego , tuna kwenda tu kama mang'ombe yanayoswagwa na maraisi wa nchi za magharibi ooooooh mbalu
paty unadhani nini kifanyike ili kuepukana na laana hii isikamate vizazi vyetu?
 
Last edited by a moderator:

Tanzania Daima nalo gazeti au udaku tu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…