1969 mwanadamu hakuweza kutua mwezini!

1969 mwanadamu hakuweza kutua mwezini!

realsam

JF-Expert Member
Joined
Jan 4, 2013
Posts
289
Reaction score
135
1969 MWANADAMU HAkUWEZA KUTUA MWEZINI !!

Wamarekani walijitahidi sana kuudanganya Ulimwengu Mwaka 1969 kwa malengo yao binafsi kisiasa na kiuchumi, lakini Ukweli utabaki kuitwa Ukweli. Picha yote ya kwenda Mwezini Mwaka huo ilibuniwa ili kuulaghai Ulimwengu kwa sababu zifuatazo :

1- Mwezini hakuna Upepo unaovuma kama hapa kwetu,cha ajabu ilionekana Bendera ya Marekani ikipepea juu ya Mwezi tena kwa nguvu kubwa kabisa.

2- Picha zote walizo piga Angani zilikuwa za rangi,wakati ambao Teknolojia haikuwa na Uwezo wa kutoa Picha za rangi huko juu, bali ilitakiwa ziwe za rangi mbili tu, nyeupe na nyeusi.

3- Alama za Viatu vyao zilionekana kuzama sana chini,wakati Mwezini Vitu mfano wa Binadamu lazima vitakuwa vinaelea kwa sababu kitu kinachopima Kilo 60 Ardhini kitakuwa na kilo 10 Mwezi ni, na hii hutokana na Ukweli kuwa Mwezi hauna nguvu kubwa ya Uvutano (Gravitational Force) kama ilivyo Sayari ya Dunia.

4- Hakuna hata Nyota moja ilioonekana kwenye Picha za Wanaanga wakati wapo Mwezini. Ilitakiwa Nyota zionekane kwa sababu Matabaka hewa ya Mwezi (Atmosphere) ni sawa na hakuna. Hivyo, ni rahisi kuziona Nyota juu ya Mwezi.

5- Warusi waliwaomba Wamarekani kuwaelekeza wapi walipotua na kuweka Vyombo vyao vya Anga ili wavipige picha na kupata Ushahidi wa kuwepo na Ziara hiyo Mwezini.Kitu ambacho kilishindikana mpaka hii leo.

6- Waandaaji wa tukio lile hususan Upande wa Kamera,walijisahau na Vivuli vyao vilionekana kwa chini, wakati wakitoa maelekezo ya nini kifanyike.

Ndugu Msomaji,safari hii pamoja na kuwa ya mashaka, ilitangazwa mno na Ulimwengu mzima kuaminishwa kwamba,Wamerekani walitua Mwezini mnamo mwaka wa 1969.Mpaka leo hii Shule zote Ulimwenguni huwafundisha Wanafunzi wao juu ya Ukweli wa tukio hilo lililobuniwa.
 
Haya uwe nayo wewe tu, ikitokea umepata watoto usiwalazimishe waamini kama unavyoamini wewe, utawakatisha tamaa na kuonesha kwamba hawawezi kufika mwezini. We endelea kua na msimamo huu lakini usimlazimishe mtu mwingine afuate hivi hata kama ni mwanao
 
16-24/julai/1969 Neil Armstrong,Buzz Adrin, na Mike Collins walisafiri hadi mwezini, hayo mengine kawafundishe washamba wa uko kwenu.
Tukio lilikuwa live mwanzo hadi mwisho(youtube video ipo)

Hoja ya tatu ni dhaifu sana kuliko zote ingawa zote ni dhaifu.

Wenzako mwezini wameenda zaidi ya mara tatu hata hao warusi unaowasema wameenda sana tu.

Wenzako wamejenga space station,na wanatuma vyombo sayari za mbali kuliko hapo mwezini.

Kuhusu bendera kupepea wakati hakuna upepo maelezo yake yapo wazi, NASA walijua kabisa mwezini hakuna upepo hivyo bendera isingepepea hivyo kipindi Adrin anapiga saluti mbele ya bendera alivuta uzi (picha inaonyesha) uliofungwa kwa lengo la kuifanya ipepea ila ukiangalia picha ya mwisho kipindi wanaondoka bendera imesinyaa kabisa.

Kwa watu wanaojua teknolojia ya space shuttling hawawezi kuamini upuuzi wako.

Tembelea NASA na website ya SPACE upate maarifa kijana sio umekaa tu unamshangaa Amber ruty.

Nisamehe kwa reaction yangu huo ndio udhaifu wangu nikikutana na hoja za kipuuzi.
 
Hoja zote zimetolewa ufafanuzi wa kutosha mtandaoni kasome usipende kushikiwa akili.
 
Kwani aliyeenda mwezini ni mrusi au Mmarekani?
 
mi naomba picha za warusi wakiwa mwezini nifananishe na za wamerakani
 
Mtoa mada unaweza kuwa na hoja za msingi maana nimeangalia Kile Chombo cha anga wanachotengeneza Boeing kwa kushirikiana na Lockheed Martin kinaitwa orion wamekitengeneza wakakirusha juu sana ya Tabaka la Dunia kupita ISS na satellite zote kikapita van allen radiation belt huku wakiweka sensors za aina mbalimbali kukusanya data.

Hii van Allen radiation belt ina chembechembe zenye chaji za nguvu kubwa zinazotokana na miale ya jua , milipuko ya nyota, Black holes, asteroids nk. Hili eneo ni hatari sana kiumbe hai chochote kikipita Lazima kipikwe kwa hio miale. Kwahiyo wataalamu wa Boeing na Lockheed Martin wanaumiza kichwa teknolojia ya kutengeneza shield ambayo itamlinda binadamu na hii miale.Nasa wamekubali mpaka sasahivi binadamu haijawezekana kumpitisha kwenye hii van Allen’s belt radiation. Safari yoyote ya mwezini,mars nk lazima ipitie van Allen’s belt radiation.
 
Mkuu usidanganyike na maelezo ya astronauts wa kirusi huko google.
.
Tizama channel ya NASA uone maajabu.
Mwaka 1958 mwana fizikia James Van Allen aligundua energetic particles ambazo zipo kama rings hivi katika sayari yetu hii ya Dunia. Ni mionzi(radiation) yenye ukanda(belt) ya aina mbili zimeizunguka Dunia. Hiyo mionzi(radiation) kwa tabaka lake la nje imeundwa kwa billions of high energy ambazo zimejizalisha kutoka kwenye Jua ambazo zinanasia au zinagandia katika earth's magnetic field, katika pahala panapojulikana kama magnetosphere.

Eneo la ndani la hii mionzi kwenye huo ukanda ni matokeo ya mwingiliano wa cosmic rays katika earth's atmosphere, na cosmic rays ni atom fragments ambazo zinanyeshelezea katika sayari ya Dunia from outside ya solar system yetu.

Kwa uvumbuzi huo hiyo mionzi ikapewa jina la mwanafizikia aliyeigundua. Ikaitwa Van Allen belt Radiation.

Habari kutoka NASA ni kwamba, satellite itakayoingia imma kwa kukusudia au kwa bahati mbaya ikakosea njia katika Van Belt Radiation uwezokano wa kuharibika ni kwamba hiyo satellite itaharibika kwa mionzi hiyo, na italeta athari hasi kwa astronauts vilevile. Mwaka 2012, NASA walituma twin Van Allen Probes Instruments ili kufanya uchunguzi zaidi kuhusu Van belt radiation. Walichogundua ni kwamba ni impenetrable barrier in space, na ipo umbali wa Km 600 kutoka earth's surface. David Sibeck kutoka NASA Goddard Space Center anasema kwamba: Teknolojia yetu tuliyonayo sasa hivi bado si rafiki wa kuweza kupita kwenye hiyo mionzi , kwa sababu kuguswa kidogo tu kwa chombo kitakachopita kwenye hiyo mionzi hata kwa mara moja, ina uwezo wa kuleta athari ya moja kwa moja kwa chombo na astronauts.

Ila tufahamu ya kwamba astronauts waliyopo ISIS hawa hawagusi hiyo belt, huwa wanaelea nyuma ya belt. Kwa maana hata kuinusa hawainusi, wapo nayo mbali kwa sababu hiyo mionzi haicheki na mtu.

Mwishoni David Sibeck anasema, kwa kufanya uchunguzi na kuendelea kujifunza kuhusu Van belt radiation, anasema: At earth, we can study these details and apply that knowledge both to our journey to Mars and...kwenye mwezi....na hii ni kauli ya 2018. Kwa sababu 2020 van Allen probes instruments inatarajiwa kumaliza mission yake kwa sababu ina running low in fuel.

Kwa hiyo, hapa ni masuala ya kumkichwa tu, kama una amini teknolojia inaenda mbele na kurudi nyuma kwamba WALIENDA MWEZINI HAYA.
 
Mwaka 1958 mwana fizikia James Van Allen aligundua energetic particles ambazo zipo kama rings hivi katika sayari yetu hii ya Dunia. Ni mionzi(radiation) yenye ukanda(belt) ya aina mbili zimeizunguka Dunia. Hiyo mionzi(radiation) kwa tabaka lake la nje imeundwa kwa billions of high energy ambazo zimejizalisha kutoka kwenye Jua ambazo zinanasia au zinagandia katika earth's magnetic field, katika pahala panapojulikana kama magnetosphere.

Eneo la ndani la hii mionzi kwenye huo ukanda ni matokeo ya mwingiliano wa cosmic rays katika earth's atmosphere, na cosmic rays ni atom fragments ambazo zinanyeshelezea katika sayari ya Dunia from outside ya solar system yetu.

Kwa uvumbuzi huo hiyo mionzi ikapewa jina la mwanafizikia aliyeigundua. Ikaitwa Van Allen belt Radiation.

Habari kutoka NASA ni kwamba, satellite itakayoingia imma kwa kukusudia au kwa bahati mbaya ikakosea njia katika Van Belt Radiation uwezokano wa kuharibika ni kwamba hiyo satellite itaharibika kwa mionzi hiyo, na italeta athari hasi kwa astronauts vilevile. Mwaka 2012, NASA walituma twin Van Allen Probes Instruments ili kufanya uchunguzi zaidi kuhusu Van belt radiation. Walichogundua ni kwamba ni impenetrable barrier in space, na ipo umbali wa Km 600 kutoka earth's surface. David Sibeck kutoka NASA Goddard Space Center anasema kwamba: Teknolojia yetu tuliyonayo sasa hivi bado si rafiki wa kuweza kupita kwenye hiyo mionzi , kwa sababu kuguswa kidogo tu kwa chombo kitakachopita kwenye hiyo mionzi hata kwa mara moja, ina uwezo wa kuleta athari ya moja kwa moja kwa chombo na astronauts.

Ila tufahamu ya kwamba astronauts waliyopo ISIS hawa hawagusi hiyo belt, huwa wanaelea nje ya belt. Kwa maana hata kuinusa hawainusi, wapo nayo mbali kwa sababu hiyo mionzi haicheki na mtu.

Mwishoni David Sibeck anasema, kwa kufanya uchunguzi na kuendelea kujifunza kuhusu Van belt radiation, anasema: At earth, we can study these details and apply that knowledge both to our journey to Mars and...kwenye mwezi....na hii ni kauli ya 2018. Kwa sababu 2020 van Allen probes instruments inatarajiwa kumaliza mission yake kwa sababu ina running low in fuel.

Kwa hiyo, hapa ni masuala ya kumkichwa tu, kama una amini teknolojia inaenda mbele na kurudi nyuma kwamba WALIENDA MWEZINI HAYA.
Safi sana umeelezea in details 👌🏿 Maana hii van Allen’s Kama ulivyoelezea ipo kms 600 kutoka duniani wakati astronauts na cosmonauts wa ISS wapo Kwenye Safe zone kms 300 kutoka duniani.In the space it is a very trouble place full of hazards and dangers. Juzi juzi alikuja visitor from outside solar system for the first time anaitwa oumuamua hii ni natural object ilikuja kwa kasi ya Ajabu ikazunguka Jua ikarudi ilipotoka sasahivi ipo maeneo ya Saturn Ikizidi kutokomea
 
Safi sana umeelezea in details 👌🏿 Maana hii van Allen’s Kama ulivyoelezea ipo kms 600 kutoka duniani wakati astronauts na cosmonauts wa ISS wapo Kwenye Safe zone kms 300 kutoka duniani.In the space it is a very trouble place full of hazards and dangers. Juzi juzi alikuja visitor from outside solar system for the first time anaitwa oumuamua hii ni natural object ilikuja kwa kasi ya Ajabu ikazunguka Dunia ikarudi ilipotoka sasahivi ipo maeneo ya Saturn Ikizidi kutokomea
Kiongozi, unaweza kunisaidia kunipa hata link ya hii issue uliyonidikeza kama hautajali? Imenivutia kiukweli.
 
Back
Top Bottom