Jamani tatizo lenyewe ni appendix ambayo inabidi kufanyiwa small operation kabla haijapasukia tumboni.Kwa sasa kuna dawa ambazo nimepewa nizitumie kwa siku 5 baada ya hapo ndo swala la operation litafuata.Wanadai kufanya operation kwa mjamzito ni hatari!
Dada pole sana, huyo daktari wako naona ni kati ya wale walipata zero form four waka-fluke wakawa madaktari. Appendicitis kama ni acute ni kweli inahitaji operation ya haraka (ni surgical emergence) asingekupa siku tano, inaweza kupasuka na ukapata madhara makubwa. Kama ni sub-acute appendicitis unaweza kupewa dawa na ikaisha hii huwa haihitaji upasuaji wa haraka unless imeturn into acute au imeshindwa kurespond kwa dawa.
Na operation kwa mama mjamzito si indication ya kutoa mimba. Ni kweli kwamba unapofanyiwa operation kuna uwezekano wa mimba kuharibika especially kama dawa za usingizi zilizotumika zinamadhara ya moja kwa moja kwa mtoto. Lakini kuna chance kubwa ukafanyiwa upasuaji na mimba yako ikaendelea kukua.
Trust me (if you can) nimefanya operation zaidi ya moja kwa mama mjamzito aliyekuwa na tatizo jingine na mimba zao hazikutoka, hivi last week nimemwona mmoja aliyekuja kwa follow-up akiwa na mimba yake ya wiki 36 sasa ana-approach term. Kati ya nilowafanyia operation wawili walikuwa na heterotopic pregnancy (yaani mimba moja imo ndani ya kizazi nyingine nje) na wote wawili mimba zao ziliendelea kukua licha ya operation nilizowafanyia ambazo ni kubwa kwa sababu mimba za nje zilishapasuka. Hii operation yako ni ndogo (kama utafanyiwa) ambayo haihitaji dawa ya usingizi ya muda mrefu wala haina manupulations nyingi, so chance ya kwamba mimba yako haitaharibika ni kubwa.
Nakushauri nenda Muhimbili waone madaktari bingwa wa upasuaji, kwanza wakuangalie na waridhike kwamba kweli ni appendicitis na pili wakushauri aina ya matibabu unayohitaji. Nenda haraka, kama ni appendicitis kweli inahitaji huduma ya haraka, LAKINI HAIHITAJI UTOLEWE MIMBA KABLA HUJATIBIWA.
Ningeshauri wajawazito wote, kama una-access ya specialist (obstetrician/gynaecologist) tafadhali muone yeye kwa ushauri wa uhakika.