100$ Loan to Oldman

Inkoskaz

JF-Expert Member
Nov 6, 2010
6,372
2,374
Mzee mmoja alienda bank kuomba mkopo wa dola 100,bank manager akwamwambia sharti awe na kitu cha dhamana ambapo kwa mshangao mzee alionyesha gari yake Ferrari yenye thamani kama dola laki tatu hivi..meneja hakuwa na kipingamizi akapokea pia file lenye document halali za gari na kumuelekeza kwa meneja mikopo amshughulikie mara moja na kumueleza kuwa riba ni 10% per month yaani dola kumi.mzee akakamata mkopo na kuondoka akiacha bank manager anaagiza gari lihifadhiwe na kulindwa vizuri kulingana na thamani yake.
Baada ya mwezi kamili mzee alirejea na kurudisha mkopo na riba ya 10$ lakini bank manager akamuita ofisini kwake kwa mazungumzo zaidi ambapo alimuuliza mzee kuwa amechunguza na kubaini mzee ni mfanyabiashara anayejiweza sasa iweje aende kukopa benki yao kiasi kidogo tu cha fedha?Mzee kwa upole akamuuliza bank manager "Hivi ni wapi hapa mjini unaweza kupaki gari ya thamani kama hiyo yangu kwa usalama bila pressure mwezi mzima kwa ujira wa dola10 tu?"
 
Back
Top Bottom