vifo maandamano tanzania

No Wikipedia entry exists for this tag
  1. Waufukweni

    Mzee Butiku: Tukubali tunaye Rais

    Mkurugenzi Mtendaji na Rais wa Taasisi ya Mwalimu Julius Nyerere, Joseph Butiku, amewataka Watanzania kukubaliana na uhalisia kwamba nchi tayari ina Rais aliye tayari kwa maridhiano. Butiku ametoa kauli hiyo leo Machi 4, 2026, wakati wa maadhimisho ya Siku ya Maridhiano (Maridhiano Day)...
  2. P

    Rais Samia kwa Rais wa Ghana: Kila kitu kipo salama Tanzania baada ya uchaguzi

    Ya kweli haya ndugu zangu? Kila kitu pipo shwari baada ya uchaguzi? Mambo yamerejea kama kawaida na uchumi umekua? ===== "Tanzania tuko watulivu na tuko sawa. Kisiasa, kila kitu kiko chini ya udhibiti baada ya uchaguzi wetu wa Oktoba. Sasa nchi imerejea katika hali ya kawaida na tunaendelea...
  3. Q

    Tundu Lissu: Mahakama ikikubali kupokea Notisi inayoongelea mauaji ya 29/10, itabidi watuambie nani aliruhusu Watanzania kuuawa

    Waheshimiwa Majaji, Wanataka tuzungumze mambo ya October 29 mtakuwa mmefungulia balaa jingine na isije ikawa shida. Mkifungua huo mlango tutaenda huko. Tutazungumzia mauaji ya kimbali na tutaulizana nani aliyeua watanzania. Hii kitu haina mashiko. Are they ready? Mimi niko tayari. Isiruhusiwe...
  4. Waufukweni

    PostGE2025 Lissu: Wanataka tuzungumze mambo ya Oktoba 29 mtakuwa mmefungulia balaa na isije ikawa shida

    Mahakama imesikiliza hoja za upande wa mashitaka na mshitakiwa kuhusu notice inayohusiana na ushahidi wa ziada, ambapo mshitakiwa Tundu Lissu amesisitiza kwamba jambo hilo halina msingi kisheria. Katika kesi inayohusiana na matukio ya uchaguzi mkuu wa 2025, Jaji Ndunguru alieleza kuwa hoja...
  5. Waufukweni

    PostGE2025 Askofu Gwajima atoa ushuhuda wa binti aliyepigwa risasi Oktoba 29 na kupona baada ya oparesheni nne

    Askofu Josephat Gwajima wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, leo katika Ibada kanisani kwake ametoa ushuhuda wa binti aliyepigwa risasi Oktoba 29, 2025 na kupona baada ya oparesheni nne. Askofu Gwajima pamoja na muumini huyo pia wanaeleza alipigwa risasi lakini hakuwa kwenye maandamano bali alikuwa...
  6. Waufukweni

    Ni uoga wa Oktoba 29, 2025 au nini kimebadilisha ukatili wa polisi kwa wafuasi wa CHADEMA Mahakamani?

    Tofauti na mwaka 2025 wakati kesi ya Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu imeanza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam na baadaye Mahakama Kuu jijini humo, mwaka 2026 kesi hiyo imeanza bila vitendo vya ukatili wa polisi kwa wafuasi wa chama hicho wanaohudhuria. Lissu alikamatwa...
  7. Waufukweni

    Prof. Tibaijuka: Nilipendekeza iundwe Tume ya Kijaji, ingepunguza kelele za ICC kuliko tume ya Rais matukio ya Oktoba 29, 2025

    "Rais alisema ataunda tume jambo jema kabisa na mimi nikaona kwa uzoefu wangu tuunde tume ya kijaji, ukienda Kwenye account ya X utaona kwamba nilipendekeza i iundwe tume ya kijaji. Sasa kama ilivyo mambo mengi labda haikueleweka tangu Tanzania iundwe haijawai kuunda na tume ya kijaji...
  8. Waufukweni

    PostGE2025 Tume ya Uchunguzi wa Matukio ya Oktoba 29, 2025 yakutana na Ridhiwani Kikwete

    Tume ya Kuchunguza Matukio ya Uvunjifu wa Amani yaliyojitokeza wakati na baada ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025, leo Januari 22, 2026, imekutana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete. Mkutano kati ya tume na Waziri Ridhiwani...
  9. DuaZaMama

    PostGE2025 Butiku: Tishio la kupigwa risasi liliwafanya watu kukaa ndani. watu milioni 5 mliambiwa mkae ndani na mlikaa

    Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku, amesema kuwa tishio la watu kupigwa risasi liliwafanya mamilioni ya wananchi kubaki majumbani. Alisema kuwa takribani watu milioni tano waliambiwa wabaki ndani na walitii agizo hilo. Ameongeza kuwa vijana...
  10. Waufukweni

    PostGE2025 Video: DW waachia Ushahidi mpya juu ya mauaji ya Oktoba 29, 2025

    Machafuko ya uchaguzi wa Oktoba 2025 nchini Tanzania yalifunikwa na giza zito la kuzimwa kwa intaneti, baada ya mrindimo wa bunduki kunyamaza ghafla. Sasa, ushahidi mpya unafichua kile ambacho hakikusimuliwa - vifo vya watu ambao idadi yao bado haijulikani, miili iliyotoweka, na tuhuma za...
  11. Waufukweni

    PostGE2025 Hellen Kijo Bisimba: Serikali inaogopa maandamano na maandamano ndiyo njia pekee iliyobaki kuishinikiza serikali

    Aliyewahi kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu, Dkt. Hellen Kijo Bisimba amesema "Kwa uzoefu wa Tanzania, serikali huwa na hofu kubwa dhidi ya maandamano na maandamano ndiyo njia pekee iliyobaki kuishinikiza serikali"
  12. Waufukweni

    PostGE2025 Clemence Mwandambo: Nimempigia Kura Samia, Familia yangu haikushiriki maandamano Oktoba 29, 2025

    Mwanamitandao Clemence Mwandambo amesema amekuwa akitumia video anazochapisha mtandaoni katika kuwashauri wanasiasa na kuwasilisha mawazo yake, lakini mara nyingine wanasiasa wamekuwa hawataki kuambiwa mawazao tofauti na wakiambiwa hivyo wanaona kama wanaowaambia wana kiburi. "Kwa bahati mbaya...
  13. Waufukweni

    PostGE2025 Azim Dewji: Wanataka kuleta vurugu halafu wasingizie hakuna HAKI Tanzania

    Mfanyabiashara na mdau maarufu wa maendeleo nchini, Azim Dewji, amewatahadharisha Watanzania kuwa makini na viashiria vya vurugu ambavyo vinaweza kutoa mwanya kwa mataifa ya nje kuvamia na kupora rasilimali za nchi, akitolea mfano wa matukio ya hivi karibuni nchini Venezuela. Akizungumza kuhusu...
  14. Waufukweni

    PostGE2025 Waziri Mkuu Mstaafu, Pinda: Maandamano gani ya kuchoma Nyumba za Watu?

    Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Awamu ya Nne, Mizengo Pinda, amesema maandamano yaliyotokea Oktoba 29 hayakuwa ya amani, akieleza kuwa baadhi ya Vijana walishiriki bila kupata maelekezo sahihi, hali iliyosababisha mipango ya kuharibu mali na miundombinu ya umma pamoja na...
  15. Waufukweni

    PostGE2025 Samia: Hatua za kuunda Tume ya Maridhiano zimeanza

    Rais Samia Suluhu Hassan amesema kuwa mwanzoni mwa mwaka 2026 Serikali imejipanga kujenga umoja wa kitaifa ambapo mchakato wa kuunda Tume ya Maridhiano tayari umeanza na Serikali itashirikiana na wadau wote ili kukubaliana muundo wa Tume hiyo. Katika hotuba yake ya kuaga mwaka 2025 na...
  16. Waufukweni

    PostGE2025 Samia: Tumeondokewa na wapendwa wetu, tuendelee kuwaombea

    Samia Suluhu Hassan, katika salamu za mwaka mpya 2026 amesema "Tumeondokewa na wapendwa wetu, tuendelee kuwaombea"
  17. Waufukweni

    PostGE2025 Tume ya Uchunguzi: Puuzieni wanaoshawishi msitoe maoni, shirikianeni na tume

    Tume ya Uchunguzi imetoa wito kwa wananchi kupuuza ushawishi wowote unaolenga kuwazuia kushirikiana na tume hiyo na badala yake watoe maoni na ushauri kwa tume. Wito huo umetolewa Desemba 26 kupitia taarifa ya tume kwa umma iliyobainisha kuwepo kwa watu au makundi ya watu yanayotekeleza...
  18. Waufukweni

    PostGE2025 Wamachinga Dar: Ni bora tupoteze uhai lakini tulitibu taifa. Vipi na hawa wajumuishwe kwenye kundi la Wasanii?

    Leo nimewasikiliza hawa Wamachinga wa Dar na mmoja wao anasema ni bora tupoteze uhai lakini tulitibu taifa. Naona hata hawa tujumuishwe kwenye kundi la Wasanii, kususia biashara zao, twende kuwaunga mkono wale ambao wana Utu na hawajitokezi kuzungumza ujinga bila kujali watu waliopoteza maisha...
  19. Waufukweni

    PostGE2025 Jaji Warioba: Waliouawa Oktoba 29, 2025 ni wengi kuliko waliouawa kwenye Vita ya Kagera

    Kwenye mahojiano na Jamhuri TV, Jaji Mstaafu Joseph Warioba amesema kwenye Vita ya Kagera, vijana wengi waliuawa na adui. Aidha, ukilinganisha na takwimu zinazozungumziwa sasa, idadi ya waliokufa ni kubwa zaidi kuliko ile ya vita. Tofauti ni kwamba, wakati ule tuliuawa na adui, lakini sasa...
  20. J

    Kulikoni CCM na Serikali kutokutoa mkono wa pole kwa Polisi na wananchi waliofariki katika vurugu za Oktoba 29?

    Wanadai kuna Polisi waliouwawa katika vurugu za Oct 29. Kitu cha ajabu hatujaona wala kusikia serikali na CCM wakitoa mkono wa pole kwa marehemu hao. Pia kuna wananchi kibao wamefariki katika vurugu za Oct 29. Baadhi yao walikuwa mashabiki wakubwa wa Rais Samia na CCM. Mfano mzuri ni Sharifu...
Back
Top Bottom