ukosefu wa maji

No Wikipedia entry exists for this tag
  1. M

    JamiiForums Tanzania KERO Wakazi wa Kimara na kata zake hawana maji zaidi ya wiki sasa, DAWASA hamuelezi maji yatatoka lini!

    Uongozi wa mamlaka ya maji safi jijini Dar-es-salaam hautoi taarifa ni lini huduma ya maji safi itarejea Kimara na kata zake zote kwa ujumla. Wanawake na watoto wanasumbuka kutembea umbali mrefu kusaka maji bila ya mafanikio. Tunaitaka mamlaka ya maji Dar-es-salaam (DAWASA) kutuelezea ni lini...
  2. B

    JamiiForums Tanzania Wananchi wa Chekereli Mkoa wa Kilimanjaro wakosa maji safi kwa zaidi ya miaka 30, magonjwa ya tumbo yasambaa

    Wananchi wa kijiji cha CHEKERELI Kata ya Mabilioni Wilayani Sam,Mkoani Kilimanjaro, wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa zaidi ya miaka 30 ambapo kutokana na ukosefu huu, wamekuwa wakilazimika kutumia maji ya Mto Ruvu kwa mahitaji yao ya kila siku, hali...
  3. M

    JamiiForums Tanzania Hata kama Dkt. Tulia unakubalika Mbeya lazima uambiwe ukweli. Kipindupindu Mbeya ni ukosefu mkubwa wa maji

    Mbeya shida ya maji ni kubwa kuliko wanasiasa wanavyojua. Labda Kipindupindu ndiyo kitawaumbua. Pamoja na miradi mikubwa Mbunge Tulia ameileta Mbeya ukweli mradi wa maji umechelewa. Watu watakuwa wamekufa na Kipindupindu. Suala la Kipindupindu Mbeya halihitaji utafiti. Jibu liko wazi Mbeya...
  4. Mkalukungone Mwamba

    JamiiForums Tanzania Waziri Aweso ajitosa sakata wanawake Kijiji cha Oltepes kutumia mkojo wa ngombe kujisafisha wakiwa hedhini kutokana na ukosefu wa maji

    Zikiwa zimepita saa chache tangu Mwananchi iripoti wanawake katika Kijiji cha Oltepes kilichopo Kata ya Orbomba, wilayani Longido kutumia mkojo wa ng’ombe kujisafisha wakiwa hedhini kutokana na ukosefu wa maji, Waziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema analifanyia kazi. Akijibu changamoto hiyo katika...
  5. Inside10

    JamiiForums Tanzania Ukosefu wa maji: Watumia mkojo wa ng'ombe kujisafisha wakiwa hedhini

    Changamoto ya upatikanaji wa maji katika Kijiji cha Oltepes kilichopo Kata ya Orbomba, wilayani Longido huwalazimu wasichana na wanawake wa eneo hilo kutumia siagi ya ng’ombe ili kudhibiti damu ya hedhi na mkojo wa ng’ombe kujisafisha. Wanawake hao hulazimika kutumia siagi hiyo (mafuta ya...
  6. S

    JamiiForums Tanzania KERO Morogoro: Wananchi wa Mindu hawana Huduma ya Maji, wanatumia ya kwenye makorongo

    Mimi Mkazi wa Mindu, Manispaa ya Morogoro jamani huku kwetu kuna kero ya maji mno licha ya kuwepo kwa bwawa lakini sisi hatuna huduma ya maji mpaka imekuwa kero inatulazimu kutumia maji ya kwenye Visima na Makorongo hali ambayo ni hatari kwa Afya zetu na ni hatari kupata magojwa ya milipuko...
  7. Stephano Mgendanyi

    JamiiForums Tanzania Mbunge Ole Lekaita: Kinamama walikuwa wakitoka kutafuta Maji saa 8 Usiku

    Mbunge Edward Ole Lekaita Kisau, Mbunge wa Jimbo la Kiteto amesema kabla ya kutekelezwa kwa miradi aliyoileta Dkt. Samia Suluhu Hassan Kiteto kina mama walikuwa wakitoka nje kuchota maji saa 8 usiku kwa ajili ya familia na mifugo. "Kijiografia Jimbo la Kiteto Mkoa wa Manyara ni Jimbo kubwa...
  8. A

    JamiiForums Tanzania KERO Mtaa wa Simba kata ya Kilungule, Bunju Beach hatuna maji zaidi ya wiki 3, DAWASA hawatupi majibu ya kueleweka

    DAWASA tunaomba majibu ni kwanini hatupati maji kwa kipindi chote hicho na bila taarifa, na pia wakipigiwa simu wanadai wanashughulikia lakini hakuna chochote kinachoendelea. Imekuwa ni changamoto ya kujirudia rudia isiyopata utatuzi. Maji yatatoka wiki moja halafu watatuma bili baada ya hapo...
  9. USSR

    JamiiForums Tanzania Ukosefu wa maji mkoa wa Dar es Salaam,je mtaani kwako kuna maji?

    Sisi wakazi wa mbezi Louis hatuna maji wiki ya pili sasa kwa taarifa za uhakika ni mkoa mzima unatatizo la ukosefu wa maji na huenda waziri Aweso akawa waziri wa tatu kutoka tanga kutimuliwa baada ya Ummy Mwalimu na Januari makamba! Je, mtaani kwako kuna maji? Unateseka na kadhia hii ukiwa...
  10. Insidious

    JamiiForums Tanzania Ukosefu wa maji Tabata, DAWASA hawana majibu

    Kwenu Wahusika, kwa mara ya pili! Naandika kutoa malalamiko yangu na kuhusu kukosekana kwa maji kutoka DAWASA katika maeneo mengi ya Tabata, kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa ambayo pia inatufanya kuingia gharama kubwa kupata maji hayo. Bill yetu ya hivi karibuni inaonyesha matumizi ya maji kuwa...
  11. Mkalukungone Mwamba

    JamiiForums Tanzania Maandamano Makubwa Kata ya Olijoro Namba 5, Mkoani Manyara Wananchi Wafunga Barabara Kudai Maji, Polisi waingilia kati

    Wananchi wa Kata ya Olijoro namba 5 Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara ambapo leo Agosti 26, 2024 yamefanyika maandamano makubwa ya Wananchi wakiishinikiza Serikali, Kuwapatia maji baada ya huduma hiyo kuikosa kwa muda mrefu sasa. Wananchi na Viongozi wa Vijiji wamesema changamoto hiyo ni ya...
  12. A

    JamiiForums Tanzania KERO Ukosefu wa Maji baadhi ya maeneo ya Tabata

    Ndugu DAWASA na Waziri wa maji, Ninaandika kueleza hasira yangu kuhusu tatizo linaloendelea la ukosefu wa maji katika baadhi ya maeneo ya Tabata Kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa hatujawa na maji, na licha ya kupiga simu mara kwa mara kwa laini ya huduma kwa wateja, tumeambiwa kwamba hawana taarifa...
  13. M

    JamiiForums Tanzania Mwekezaji aunganishiwa maji umbali wa Km 12 huku Vijiji bomba hilo lilipopita vikikosa maji

    Kitendo cha Mwekezaji kupelekewa maji na Wananchi kukosa, kimeibua maswali kwa Wananchi wa Kitongoji cha Mgodini, Nyakavangala, Kata ya Malenga Makali, Wilaya ya Iringa mkoani Iringa. Mwekezaji huyo amepelekewa maji, huku Wananchi wenye uwezo mdogo wakinunua maji kwa ndoo moja TZS 500/-, huku...
  14. Kisesetusese

    JamiiForums Tanzania KERO Responded Dar: Maeneo ya Segerea hadi Kinyerezi hakuna Maji

    Mkuu Naomba nilete kwako kero hii ambayo kwa hapa Dar es Salaam imeelekea kukomaa sasa. Kuanzia tabata, segerea kinyerezi huduma ya maji haipatikani. Bila shaka kuna kutoa rushwa maji yafunguliwe upande wenu. Maeneo ya Kanga Kinyerezi maji hayatoki wiki ya 3. Mheshimiwa unahujumiwa tunaomba...
  15. obedia musa

    JamiiForums Tanzania KERO Responded DAWASA wanauza maji kwa njia ya magari Kinyerezi wakati Mabomba hayatoi maji

    DAWASA KINYEREZI WAHUJUMU UCHUMI… Hii ni habari ni inayopaswa kuchukuliwa na kufanyiwa kazi na Mamlaka nyingine za nchi kwa haraka sana. Ni hivi, kutokana na uhitaji wa maji kuongezeka na watumiaji kuwa wengi, Serikali iliamua kuanzisha ofisi nyingine kwa upande wa Tabata kwa kufungua ofisi ya...
Back
Top Bottom