Naibu Mkurugenzi Habari Uenezi na Mawasiliano kwa Umma wa Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA) na Mwandishi wa Habari wa Mawio Online TV, Ipyana Samson Umetuliwa na Chama hicho kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Uyole Jijini Mbeya Katika Uchaguzi Mkuu wa Rais Ubunge wa Diwani Utakaofanyika Oktoba...
Baba Levo ameshinda kuwania Ubunge kwa kura za maoni Katika mchakato wa kura za maoni wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa ajili ya kumpata mgombea ubunge wa Jimbo la Kigoma Mjini.
1. Clayton Chipando (Baba Levo): 77
2. Kilumbe Shaban Ng'enda: 38
3. Dkt. Ahmad Sovu: 32
4. Baruan Muhuza: 20
5...
Wakati wewe unachangaa na Mwijaku kukosa ubunge, pembeni kuna familia za viongozi wameamua familia nzima ziingie bungeni. Miongoni hapo chini ni wanafamilia wa familia za viongozi wanaowania ubunge 2025 na wamefanikiwa kupita kamati kuu
Familia ya Rais SAMIA SULUHU HASSAN
1. Mtoto - Wanu...
Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimempitisha mfanyabiasha maarufu Salum Kinyoro 'Kibakuli' kuwania ubunge wa Jimbo la Handeni mjini.
Salum atachuana na wagombea wengine watano.
Katibu wa Itikadi na Uenezi, Amos Makala ametangaza majina hayo leo Julai 29, 2025.
Wakuu
Kumekuwepo maswali mengi kuhusu wingi wa waliojitikeza kuchukua fomu za kutia nia na ubunge na udiwani, kupitia Kipindi cha Mada Kuu - TBC kilichofanyika Julai 10, 2025 Mchambuzi wa Masuala ya Siasa, Deus Kibamba alieleza badhi ya sababu zinazowavutia wengi kuwania nafasi ya Ubunge nchini...
Jumla ya watia nia 44 wanawake wamechukua fomu za kuwania nafasi mbalimbali za uongozi Mkoani Mtwara ikiwemo Ubunge,Ubunge Viti Maalum pamoja na Ubunge Viti Maalum Vijana Tanzania Bara.
Akitoa taarifa za watia nia wa nafasi hizo katika majimbo 10 yaliyopo mkoani Mtwara Katibu wa Siasa,Uenezi na...
Kada wa Chama cha Ukombozi wa Umma (Chaumma), Davidi Tajiri Mhanga (kulia), amechukua fomu ya kutia nia kuwania Ubunge Jimbo la Mkuranga na kukabidhiwa na ofisa usimamizi wa shughuli hiyo makao makuu ya chama hicho, Shadya Abubakar
Fomu hiyo amechukua leo, Julai 3, 2025 ofisi za makao makuu ya...
Mwenyekiti wa umoja wa wafanyabiashara na watoa huduma Tanzania, Martin Massawe, amechukua fomu kuomba kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi, kugombea ubunge Jimbo la Moshi vijijini
Massawe ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri kuu ya CCM Mkoa wa Kilimanjaro, amechukua fomu hiyo Julai 2, 2025 ambapo...
Mtaalamu wa mambo ya Uchumi, Enock Koola amejaza na kurudisha fomu ya kuwania Ubunge, Jimbo la Vunjo linalopatikana katika Wilaya ya Moshi Vijijini.
Zoezi la kuchukua, kujaza na kurudisha fomu limesitishwa rasmi siku ya Jana Julai 2.
Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Shamira Mshangama amechukua fomu ya kuwania ubunge wa viti maalumu Mkoa wa Tanga.
Shamira amechukua na kujeresha fomu hiyo Julai 2, 2025 kwa Katibu wa UVCCM Mkoa wa Tanga, Ibrahim Kandumila katika Ofisi ya CCM Mkoa wa Tanga...
Wakili wa kujitegemea Tumsifu Kweka, ambaye pia ni Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM mkoa wa Kilimanjaro pamoja na Mkutano Mkuu wa CCM Taifa, leo amejitokeza rasmi kuchukua fomu za kuwania ubunge katika Jimbo la Siha kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Kweka alifika katika Ofisi za CCM wilaya ya...
Mkuu wa zamani wa mkoa wa Lindi na mbunge mstaafu wa jimbo la Mbozi, Godfrey Zambi amechukua fomu za kuomba ridhaa ya Chama Cha Mapinduzi kwa ajili ya kuwania kiti cha ubunge cha jimbo la Mbozi.
Mbali ya kuwa mkuu wa mkoa pia Zambi aliwahi kuwa Naibu Waziri wa Kilimo.
Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nebart George Mwapwele, amechukua rasmi fomu ya kuwania ubunge kupitia tiketi ya CCM katika Jimbo jipya la Kivule, mkoani Dar es Salaam
Nebart Mwapwele ambaye pia amewahi kuwa Mkurugenzi wa TCCIA, ameeleza kuwa uamuzi wake wa kuchukua fomu umetokana na nia...
Wakati Waziri wa Uchukuzi Abdallah Ulega na Mkewe Mariam Abdallah Ibrahim wamechukua fomu ya kuomba kuwania Ubunge wa jimbo na viti maalum katika Mkoa wa Pwani. wadau mbalimbali wamehoji hatua hiyo imelenga kutatua kero za wananchi au ni ubinafsi wa madaraka.
Mpaka leo hii kati ya wale waliochukua Fomu kuwania Ubunge kupitia CCM ambao ni wapya kabisa sijaona ambaye anafaa
Hivi kwanini CCM safari hii imeamua Kujidhalilisha hivi na kukubali hata kila mtu achukue fomu wachukue Fomu?
Aliyekuwa Mshindi wa Pili MNEC mwaka 2022 Walter Rishaeli Nnko, Leo June 29 amechukua fomu ya kugombea Ubunge katika jimbo la Kibamba lililopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo jijini Dar es salaam.
Nnko amesema anamshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa...
Katibu wa Watanzania waishio nje ya nchi 'Daispora' Tanzania, Hassan Maftaha akionyesha fomu ya kuwania ubunge wa Kinondoni baada ya kuichukua leo Jumapili Juni 29,2025.
Fomu hiyo amekabidhiwa na Katibu Msaidizi wa Uchaguzi Wilaya ya Kinondoni, Amosi Richard kwa ajili ya kuwania nafasi hiyo
Aliyekuwa Meya wa Manispaa ya Temeke jijini Dar es Salaam, Abdallah Mtinika amechukua fomu ya kuomba kuteuliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwania Ubunge wa Temeke.
Mtinika amekabidhiwa fomu hiyo leo Jumapili, Juni 29, 2025 na Katibu wa UVCCM Wilaya ya Temeke, Sayi Samba.
Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa, Ezekiel Mollel naye amechukua fomu ya kuwania ubunge Jimbo la Arumeru Magharibi.
Mollel ambaye pia ni mwalimu amekabidhiwa fomu hiyo leo Jumapili Juni 29, 2025, na Katibu wa CCM Wilaya ya Arumeru, Kamila Kigosi.
Khadija Mfaume Liganga, maarufu kama Dida, ambaye ni Mjumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa anayewakilisha Mkoa wa Mwanza, amechukua fomu kuomba ridhaa ya kuwania nafasi ya Ubunge wa Viti Maalum vya Wanawake kupitia Mkoa wa Mwanza.
Dida ni mwanaharakati mashuhuri wa haki...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.